Skip to main content

JUWALAZA YAIWATA WANANCHI KUJIFUNZA LUGHA YA ALAMA

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::

JAMUIYA ya wakalimani wa lugha ya alama Zanzibar ’JUWALAZA’ imeitaka jamii kujiunga na jumuiya hiyo, ili kujifunza lugha ya alama, ili kukidhi haki ya mawasiliano kwa watu wenye ulemavu wa uziwi.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia simu, leo Novemba 18, 2022 Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Kheir Mohamed Simai alisema, bado jamii haijaona umuhimu, wa kujifunza lugha ya alama, na kuwasaidia viziwi katika mawalisiliano.

 

Alieleza kuwa, kundi la viziwi katika jamii ni sawa na kundi jengine lolote, ambalo linahaki ya kuwasiliana baina yao na kundi jengine, ingawa wao ni kwa kutumia lugha ya alama.

 

‘’Mawasiliano ya wenzetu hawa ni maalum, hivyo kila mmoja ana haki ya kuhakikisha anawasiliana nao, ili kutumiza utu na ubinadamu, lakini jambo la kwanza ni kujifunza lugha ya alama,’’alieleza.

 

Aidha Katibu mkuu huyo, alisema Jumuiya tokea mwaka 2019, imekuwa na utaratibu wa kufanya maadhimisho ya siku ya wakalimani, ingawa kwa mwaka huu. siku hiyo imesogezwa mbele kwa siku moja.

 

‘’Novemba 18 kwa vile ni Ijumaa, tumeona bora tuendeshe dua maalum, kwa ajili ya kuwaombea dua viongozi, watetezi wa haki za watu wenye ulemavu, pamoja na waasisi wa Umoja wa watu wenye Ulemavu Zazibar, akiwemo maalim Khalfan Hemed Khalfan,’’alifafanua.

 


Katika hatua nyingine, Katibu mkuu huyo wa Jumuiya ya wakalimani Zanzibar Kheir Mohamed Simai alisema, wazazi na walezi ndio kundi la mwanzo, kuhakikisha wanawalinda na kuwapatia haki zao viziwi.

 

Mjumbe wa Jumuiya hiyo kisiwani Pemba, Asha Suleiman alisema, bado jamii haijaona umuhimu wa kuwashirikisha viziwi katika mipango na mikakati ya kimaisha.

 

Alieleza kuwa, wenye uziwi hawaonekani kua wanamchango wowote katika jamii, hivyo huanza kubaguliwa kuanzia kwenye haki ya msingi ya mawasiliano.

 

‘’Utaona kiziwi anahitajia huduma katika eneo fulani, lakini kwa vile muombwa huduma hakujifunza lugha ya alama, huishia kumcheka na kumdharau, jambo ambalo sio sahihi,’’alieleza.

 

Issa Haji Mjanakheri wa Kangangani wilaya ya Mkoani, wenye uziwi alisema, amekuwa akipata shida wakati anapotaka huduma, hasa kwenye ofisi za umma.

 

Aisha Omar Ali wa Mtambile, alisema ni vyema suala la ufahamu wa lugha ya alama, likawa lazima kuanzia ngazi ya jamii hadi taifa.

 

‘’Ingawa sasa kuna ahuweni kwenye ZBC tv, tunaona kuna mtaalamu wa lugha ya alama, na hasa kwenye taarifa ya habari au shughuli za kitaifa akiwasiliana na viziwi,’’alieleza.

 

Siku ya wakalamani huadhimishwa kila ifikapo Novemba 18, ya kila mwaka, ambapo kwa mwaka huu, itaadhimishwa Novemba 19, eneo la Unguja ukuu na mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa wa kusini Rashid Hadid Rashid.  

 

Upande mwengine ni kuwa, siku ya Ukalimani wa lugha ya alama duniani, ilianzishwa na Umoja wa Mataifa UN, mwaka 2017, ambapo Umoja huo, ulipitisha siku hiyo kwa sababu ya shirikisho la wakalimani duniani ‘FIT’ wamekuwa wakiitumia siku hiyo, kuadhimisha siku ya wakalima na wafasiri tangu mwaka 1991.

 

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu Ibara ya 21 (b) inaeleza kuwezesha matumizi ya lugha ya alama, maandishi ya braille kuongoza na kuweka mawasiliano mbadala kwa njia nyingine na mfumo wa mawasiliano watakaoamua.

 

Aidha sheria nambari 9 ya mwaka 2016 ya haki na fursa ya watu wenye ulemavu Zanzibar kifungu cha 15, ni lazima mawasiliano kwa watu wenye ulemavu utolewe kwa njia mbali mbali, ikiwemo la nukta nundu na lugha ya alama.

                            mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...