Skip to main content

WATETEZI HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA WATOA NENO HUKUMU YA MAHAKAMA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

WATETEZI wa haki za watu wenye ulemavu kisiwani Pemba, wamepongeza hatua ya Mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji, mkoa wa kaskazini Pemba, kumuhukumu kutumikia chuo cha mafunzo miaka 7, mshtakiwa Nuhu Kombo Nuhu, baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti, kijana mwenye ulemavu wa akili.

Walisema, uamuazi wa mahakama hiyo, kutenda haki katika kesi hiyo ambayo ilishaanza kukumbwa na changamoto hasa ya mshtakiwa kujifanya ana umri wa miaka 17, lakini hatimae haki ilitendeka.

Wakizungumza na mwandishi wa habari kwa nyakati tofauti, baada ya hukumu hiyo, walisema kitendo alichokifanya mshitakiwa huyo, cha kumlawiti kijana (19) mwenye ulemavu wa akil, sio cha kibinadamu na kinafaa kulaaniwa.

Mmoja kati watetezi hao, Safia Saleh Sultan kutoka Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, alisema kama mahakama zintaendelea na masimamo huo, kundi la watu wenye ulemavu litaheshimaka.

Alieleza kuwa, watu wenye ulemavu hasa wa akili, lazima waangaliwe vyema wanapotoa ushahidi, na ikiwezekana wasaidiwe ili kunyoosha maneno vizuri.

Nae Mratibu wa Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ‘ZAPDD’ Khalfan Amour Mohamed, alisema ingawa hatia hiyo ni ndogo, lakini imesaidia kwa kundi la watu wenye ulemavu.

‘’Sio kawaida sana kukutana na kesi za watu wenye ulemavu kushinda, maana yale mazingira waliyonayo, huwa ni kichaka kuziua kesi, lakini kwa hii kwa kiasi fulani tunapongeza,’’alieleza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jumuia ya wasioona Zanzibar ‘ZANAB’  Pemba Suleiman Mansour, alisema ushirikiano kati ya wazazi wa kijana mwenye ulemavu wa akili, na vyombo vya sheria, ulichangia kutiwa hatiani kwa mshitakiwa huyo.

Mwakilishi wa kundi la vijana wenye ulemavu, katika baraza la vijana Zanzibar Katija Hamad, alisema hatua iliyochukuliwa na vyombo vya ulinzi na usalama, imesaidia kupatikana kwa haki.

‘’Bado niendelee kuwasisitiza wazazi na walezi, kuwawekea ulinzi maalum watoto wao wenye ulemavu, maana wadhalilishaji sasa wameamua kulikimbilia kundi hilo,’’alisema.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib, amekuwa akirejea tamko lake, la kuwataka wazazi kukataa kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji, na badala yake waviachie vyombo vya sheria kuamua.

Wazazi wa mtoto aliyelawitiwa, walisema hawakuamini kuwa haki ya mtoto wao ingepatikana, kutokana na changamoto walizopitia, ikiwa ni pomoja na mshitakiwa kupunguziwa umri.

‘’Awali mshitakiwa tuliambiwa ni mtoto, hivyo kesi yake ilishaanza kusikilizwa mahakama za watoto, lakini baada ya vipimo ikaonekana ni mtu mzima, hadi sasa kufikia kufungwa miaka saba,’’walisema.

Nuhu Kombo Nuhu (19) mkaazi wa Kijichame wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba, sasa anaendelea kutumikia chuo cha mafunzo kwa miaka saba (7), na kulipa fidia ya shilingi milioni 1, baada ya kupatikana na kosa la kumlawiti, kijana mwenzake mwenye ulemavu wa akili miaka 19.

Hakimu wa mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoa wa Kaskazini Pemba, Abdulrahman Ali Abdul Rahman, alisema kesi hiyo imesikilizwa ikiwa na mashahidi wa watano, ambao ushahidi wao ulitosha kuishawishi mahakama kumtia hatiani.

Tukio hilo lilitokea Disemba 13, mwaka 2021, majira ya saa 1:30 asubuhi eneo la Kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba, ambapo mshitakiwa huyo, alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.

Kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 116 (1), cha sheria Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.

                      Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch