Skip to main content

ZIJUWE HAKI ZA MUAJIRIWA ZISIZOTANGAAZWA KWA KINYWA KIPANA NA MUAJIRI

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

KANUNI ya Utumushi wa Umma ya Zanzibar ya mwaka 2014, imeundwa na vifungu wastani wa 134.

Kanuni hii, ni zao la sheria ya Utumishi wa Umma ya Zanzibar, ambayo nayo ilitungwa na Baraza la Wawakilishi, kwa lengo la kubainisha na kuweka wazi haki, wajibu wa watumushi wa umma.

Kanuni hii, imekuja kufafanua na kuweka taarifa kwa upana zaidi kwa watumishi wa umma wa Zanzibar, ili kuongeza kasi, ari, hamasa na juhudi za kuwahudumia wananchi.

Kanuni hii ya utumushi wa umma ambayo ilisainiwa Mei, 29 mwaka 2014 kazi iliyofanywa na aliyekuwa Waziri wa nchi ofisi ya rais, kazi, na utumishi wa umma Zanzibar Haroun Ali Suleiman.


UTEKELEZAJI WA KANUNI HIYO

Watumishi waliowengi wa umma Zanzibar, kwao kanuni hii imekuwa maarufu na kuitekeleza kwenye vifungu vichache ambavyo, pengine vinamsaidia mwajiri na sio mwajiriwa.

Kwa mfano, wengi wa watumushi wa umma, wanaelewa kuwa kanuni hiyo inavifungu vya kuhimiza kufika kazini saa 1:30 na kuondoka saa 9:30 kama sio vyenginevyo, kwa wale watumishi wanaonyonyesha.

Lakini vifungu vyengine maarufu kwa watumishi wa umma ni cha 58 kinachogusa likizo la mwaka, kifungu cha 61 cha likizo la uzazi iwe pacha au mtoto mmoja, kifungu cha 59 cha haki ya likizo la dharura pamoja na ya muda na kile cha 60 cha likizo ya maradhi.

Kwenye kanuni hiyo, kifungu chengine ambacho ni maarufu kwa watumishi wa umma, ni bwana mkubwa, yaani kupewa mshahara, ruhusa ya kuondokewa/filiwa baba, mama, mke, mtumishi mwenyewe au mtoto.

Vifungu hivyo na vyengine vimekuwa maarufu, maana watumishi wanapoajiriwa wamekuwa wakielezwa na muajiri, ingawa vyengine huelezwa pole pole, kadiri matukio yanapotokea.

VIFUNGU VIZURI VISIVYOTANGAAZWA HADHARANI

                    NA BAADHI YA WAAJIRI

Kwa uwingi wa vifungu vya aina hiyo, vilivyomo ndani ya Kanuni ya Utumushi wa Umma ya Zanzibar ya mwaka 2014, leo tosheka na vifungu vifuatavyo, ili kuvijua uzuri wake.

Kifungu cha 15 kinachoelezea upandishwaji daraja kwa watumushi wa umma, ambapo kifungu kidogo (1), kinaeleza kuwa ‘kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 64 cha Sheria, Katibu Mkuu au Mkuu wa taasisi, atapendekeza kwa Tume ya Utumishi husika kumpandisha daraja mtumishi yeyote wa umma’.

Kifungu kikazidi kufafanuwa kuwa, mtumushi huyo ni mwenye sifa na ujuzi wa nafasi zinazotarajiwa kujazwa kwa masharti yafuatayo, ikiwa ni pamoja na nafasi hiyo, iwe inafahamika katika miundo ya kada za utumishi.

Na mtumishi wa kujaza nafasi hiyo achaguliwe kwa mujibu wa masharti ya Sheria, ambapo kupandishwa cheo kutafanyika kwa mtumishi atakayethibitika kuwa, anao uwezo wa kushika madaraka katika nafasi zilizowazi na inayohitaji kujazwa.

Kifungu chengine, ambacho kama hakitangaazwi sana vile na muajiri, ni kile cha 17, ambacho kinampa haki mtumishi wa umma, aidha kukataa au kukubali cheo alichopandishwa.

Ingawa inamtaka mtumishi huyo, ikiwa anataka kukataa cheo hicho, afanye hivyo kwa muajiri wake, kwa muda usiozidi mwezi mmoja, baada ya kuarifiwa kwake juu ya cheo hicho.

Kifungu chengine ni kile cha 26, ambacho kimempa haki mtumishi mjamzito kikieleza kuwa, ‘ni marufuku kwa Katibu Mkuu au Mkuu wa taasisi baada ya kupata uthibitisho kutoka kwa daktari, kwa usalama na kwa afya ya mtumishi huyo, kumpangia kazi za usiku au za ziada.

Kifungu hicho kikaenda mbali zaidi kikieleza kuwa, ‘ni marufuku kuajiri au kumpangia mtumishi wa kike kufanya kazi katika eneo lolote, lenye kutumika madawa ya kemikali za sumu, benzino au mionzi, ambayo yatapelekea kuathiri uzazi au ujauzito wake.

Utamu mwengine uliomo kwenye kanuni ya utumishi wa umma ya mwaka 2014, ni kwa wale wenzetu wenye ulemavu, maana kifungu cha 30, kinaeleza wazi kuwa, ‘itakapotokezea watu wa makundi maalum wana sifa sawa na watu wengine, katika masharti ya ajira, kipaumbele kitatolewa kwa watu wa makundi maalum.

Kipo kifungu cha 62 nacho sio maarufu sana, kinachompa haki mume, ambae ni mtumishi wa umma, cha mapunziko ikiwa mke wake hata amabe sio mtumishi amejifungua, kupumzika.

Kifungu hicho kinachoundwa na vifungu viwili vidogo kinafafanua kuwa, ‘mtumishi wa umma ambae mkewe amejifungua, ataruhusika kupewa likizo ya malipo, kwa muda wa siku tano za kazi.

Vifungu hivyo pacha vikaeleza kuwa, ’likizo hilo litachukuliwa ndani ya siku saba, baada ya mtoto kuzaliwa na halitoathiri likizo yake ya mwaka, na litatolewa kila baada ya miaka mitatu.

Zuri zaidi kanuni haikuwasahau wale, watumishi wenye mke zaidi ya mmoja iksema kuwa, ‘mtumishi mwenye mke zaidi ya mmoja atastahiki likizo la kila mke atakapojifungua, hata hivyo, endapo atakaekuwa anajifungua kila mwaka ni mke huyo huyo, mmoja atastahiki likizo hilo kila baada ya miaka mitatu.


HALI IKOJE KWA WATUMISHI?

Mkuu wa shirika la Magazeti Pemba Bakar Mussa Juma, anasema amekuwa akiwapa ruhusa wafanyakazi ambao wake zao wamejifungua.

‘’Hivi sasa kunamfanyakazi yuko mapunziko ya siku tano za kazi, na mwengine ameripoti Septemba 15, mwaka 2022 akitokea kwenye mapunziko kama hayo,’’anasema.



Anasema vifungu hivyo anaona sio maarufu kwa sababu havitumiki mara kwa mara, ingawa kubwa zaidi ni watumushi kutozisoma kanuni husika

Fauzia Mussa Alawi, asiyeoona ambae ana shahada uhasibu, anasema kanuni ya kuwapa kipaumbele watu wenye ulemavu katika uajiri, haitekelezwi kwa kina.

‘’Mimi nishawahi kufanya usaili nikiwa na wanaume wawili na mimi peke yangu, lakini mwisho wa siku sikuajiri na aliajiriwa mwanamme,’’alieleza.

Mfanyakazi wa wizara ya Habari Pemba Ali Suleiman, anasema sasa ana watoto wanne, ingawa ni mtoto mmoja pekee, ndio alipata haki ya kupata mapunziko ya siku tano kwa mke wake kujifungua.

‘’Ni kweli muajiri, zipo haki nyingine huzikalia kwa watumishi wao, na wanachojua wao ni kutimiza wajibu kwa mtumishi ikiwemo kufika kazini na kuondoka kwa wakati,’’anasema.

Aisha Hassan Mzee mtumishi wa wizara ya elimu, anasema inawezekana haki nyingi watumishi hawazijui, kwasababu wanaposmeshwa haziguswi.

Halima Iddi Omar anayefanyakazi wizara ya Maji kwa miaka 28 sasa, anasema hakumbuki kupandishwa daraja kama kanuni ya utumishi wa umma, inavyoelekeza.

Aliyekuwa Afisa Utumishi wizara ya Ardhi Pemba Fatma Salim Matta, anasema aliwahi kutoa mishahara ya watumishi wake wanne kuikabidhi kwa familia, wenyewe baada ya kufariki.

‘’Sisi huwa makini kwenye haki za wafanyakazi au wategemezi wao, na ndio maana, tumeshawahi kuitekeleza kanuni hiyo, baada ya watumishi wanne kufarika kwa wakati tofauti,’’alieleza.

IPA 

Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar 'IPA' kimekuwa kikiwasisitiza waajiri kuwasomesha watumishi wa umma kanuni na sheria za kazi, ili waepuke kuingia kwenye migogoro.

''Kwa mfano mwishoni mwa mwaka huu watumishi 1400 wa wizara ya elimu wakiwemo waalimu walisomeshwa sheria saba zinazohusu utumishi, hili ni jambo jema,''alisema muwezeshaji kutoka IPA Abubakr Nuhu. 

ATHARI YAKE

Mfanyakazi wa wizara ya elimu Pemba, anasema moja ni kuwatayarisha watumishi kuwa wizi wa mali za umma.

''Ikiwa haki za wafanyakazi hasa ngazi za chini hazitekelezwi na kwa wakubwa zinatekelezwa, ni kuwatengeneza watumishi kuwa wizi, ili kufidia haki zao, blaming claim of right,''anasema.

Aisha Sudi kutoka wizara ya Miundombinu, anasema athari nyingine ni kuwadumaza watumishi na kuwanyima haki na fursa watumishi wa umma. 

NIN KIFANYIKE

Watumishi wa umma wamesema ifike wakati sasa, muajiri kuweka darasa maalum kuwasomesha kanuni watumishi, hata kabla ya kuajiriwa.

Muwezeshaji kutoka Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar IPA Khamis Nassor, anasema watumishi lazima wajifunze kujisomesha kanuni na sheria.


                 Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch