Skip to main content

VYAMA VYA SIASA VYATAKA MARDHIANO, AMANI ILIYOPO ZANZIBAR ISHESHIMIWE

 




NA ALI SULEIMAN, PEMBA

TAREHE 6 Disemaba mwaka jana, ilikuwa siku pekee ya kihistoria kwa wazanzibari kuzaliwa upya kisiasa.

Hii ilikuwa ni kufuatia kitendo cha rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi, kumteua Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Makamu wa Kwanza wa rais.

Kitendo hicho cha kikatiba, kilihusisha uungwana, ubobevu wa kisiasa, ukweli, nia ya kimaendeleo, utayari wa kuwaunganisha wazanzibari, kwa viongozi wetu hawa wawili.

Maana walishasema wazee wa zamani kuwa, muungwana ni vitendo, na chanda chema huvishwa pete, haya yanashabihiana mno na hapa kwetu Zanzibar kwa tendo hilo.

Maana viongozi wetu wakuu, marehemu Maalim Seif Sharif Hamad na Dk. Hussein Mwinyi ambao kwa upande mmoja ni viongozi wa vyama vya siasa, kwa kule kuungana kuunda serikali ya pamoja.

Ingawa uundaji wao wa serikali hii ya Umoja wa Kitaifa, umeelezwa ndani ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kufuatia marekebisho ya 10, pia yaliofanywa mwaka 2010.

Awali, Zanzibar ilishaanza mingurumo ngurumo ya kutaka kuchafuka kwa amani yetu, na hasa baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa vyama vingi, mwaka jana 2020.

Na inawezekana wapo mabeberu, wakoloni wa kileo, wafitinishaji na wasiotakia mema Zanzibra, walitamani kuona tunarudi kule, ambako tumeshakupita.

Maana, wazanzibari walishavuuka kwenye kugomeana, kutengana, kupigana, kubaguana, kuwekeana chuki, na sasa kuanzia baada ya uchaguzi mkuu na kuendelea, hayo yameshazikwa.

Na ndio maana, sasa serikali yetu ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeshatimia, kwa kule kuwa na serikali hiyo, ingawa yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa umaarufu ‘SUK’.

Ni mfumo, ambao upo kikatiba, ambapo Makamu wa Kwanza inaelezwa kwenye Katiba hiyo kuwa, atatoka ndani ya chama kilichoshika nafasi ya pili, huku Makamu wa Pili akitoka kwenye chama anachotoka rais.

VYAMA VINASEMA JE JUU YA MARIDHIANO HAYO

Hapa Makamu wa Kwanza, ambae kisiasa anatoka chama ACT-Wazalendo, marehemu Maalim Seif Sharif Hamad, alisema haikuwa kazi rahisi mpaka yeye kukubali kuingia kwenye mfumo huo wa serikali.

Mara zote, anapokutana na makundi ya wazazibari, husema bila kigugumizi kuwa, alikubali hilo baada ya yeye kupokea ushauri kutoka kwa wazanzibari kadhaa, wakiwemo wanachama wake.

Alikuwa akielezwa faida ya kushirikiana kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa na hasara ambayo wazanzibari wengeipata kwa miaka mitano ijayo.

“Mimi nimeingia kwenye maridhiano haya kwa ajili ya kuiweka Zanzibar yetu, katika mawanda mapana ya kutokomeza chuki, hasama, kubaguana, kutoaminiana na hasa kwa vile, sote ni wa wamoja,’’aliwahi kusema wakati wa uhai wake.

Hata hivi karibuni, alipokutana na wananchi wa wilaya ya Mkoani, marehemu Maalim Seif alisema alichoangalia yeye kwanza ni kurudisha umoja wa wazanzibari, ambao walikwisha uzoea kuishi kwenye amani na utulivu.

Anafafanua kuwa, ikiwa maradhiano yameshafikiwa na viongozi wakuu, sasa asibakie mwengine kupalilia chuki, hasama, utengano na ubaguzi, kwani hivyo sio asili ya wazanzibari.

Hata alipokuwa wilaya ya Micheweni Pemba, Makamu huyo wa Kwanza alirejea kauli yake, ya kuwataka wananchi wa Zanzibar kuunga mkono maridhiano hayo.

Anasema kila mmoja ni mshindi, na kila mmoja ana haki na fursa sawa kama mwenzake, hivyo hakuna sababu kwa wenye mamlaka kuwabagua wengine.

“Sasa tunaishi kwenye maruidhiano, yanayoambatana na amani na utulivu, kama kuna sheha, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa na wengine watende haki kama anavyosimamia Rais Mwinyi,’’anafafanua.

Hata Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, akizungumza mara baada ya kumuapisha Makamu huyo wa Kwanza, alitaka maridhiano hayo yaungwe mkono.

“Leo tumeshamuapisha Maalim Seif Sharif Hamad, na Zanzibar sasa imeshazaliwa upya, ni wajibu wetu wananchi kuunga mkono hili, maana ndio hatua ya kwanza ya kuelekea kwenye Zanzibar mpya,’’anasema.

Lakini Dk. Mwinyi, hata alipokuwa akizungumza kwenye siku ya maadili, alirudia kauli yake ya kuwataka wazanzibari kuhakikisha kuwa, wanayalinda kwa gharama yoyote maridhiano hayo.

Alikwenda mbali zaidi, akisema kila mmoja kwa alipo awe mwandishi wa habari, kiongozi wa dini, kiongozi wa chama cha siasa na vyama vya wafanayakazi, lazima hili walikumbuke.

Akawatanabahisha wazanzibari, kuwa azma yake na viongozi wenzake ndani ya serikali yenye mfumo wa umoja wa kitaifa ,wanayo dhamira ya kweli ya kuwatumikia.

Anasema, mipango, mikakati na mbinu za kuhakikisha wanageuza maisha yao, ipo vyema wanachotakiwa kwao ni kuwajibika, kama anavyowakumbusha wasaidizi wake.

“Kila mmoja afanye kazi kwa bidii, hamasa, ukweli, uwazi, uwajibikaji, ili haya maridhiano tuliofikia sasa yawe fursa ya kufikia uchumi wa bluu,’’anasisitiza.

Katika upande mwengine Kaimu Katibu Mkuu wa chama cha wananchi CUF Zanzibar, Mbarouk Seif Salim, alisema suala la maridhiano ni jambo jema, hasa kwa makundi yaliokosana katika jambo fulani.

Ingawa alisema, suala la maridhiano ya Zanzibar, wengetamani mno kushirikishwa kwa vyama vyote vya siasa , ingawa kwa upande wa kushiriki kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa ni jambo la vyama vya CCM na ACT-Wazalendo.

“Mimi naona maridhiano ni jambo jema, lakini yengependeza zaidi, hata vyama kama CUF, CHADEMA, AAFP, ADC, Demokrasia Makini, navyo vyengeitwa na kushirikishwa,’’anasema.

Aliyekuwa mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama cha ‘ADC’ Hamad Rashid Mohamed, amesema kwanza anaunga mkono maridhiano hayo, kwa vile ADC haipendi kuona hata damu ya kunguni, ikimwangika.

 

Anasema, maridhiano yaliofikiwa Zanzibar ndio mbolea ya kweli ya kuchapuza maendeleo, na itapelekea maendeleo yatakayopatikana siku zijazo, kila mmoja kuwa mlinzi, kwa vile atakuwa ameshiriki kwa njia moja ama nyingine.



Anasema amefurahishwa mno na uwepo wa maridhiano na hasa kwa vile Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi ni mkweli, mjasiri, mpenda maendeleo na mwenye nia thabiti ya kuipata Zanzibar mpya kiuchumi.

“Mimi niwatake wakuu wa vyama, ambavyo hadi sasa vinashindwa kuridhia makubaliano yaliofikiwa na viongozi wetu, waweke kando tofauti zao za kisiasa na tuungane kuwajengea watoto wetu Zanzibar mpya.

Kama hayo, pia yanaungwa mkono kupitia ADA-Tadea kwa aliyekuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwa chama hicho, Juma Ali Khatib, akisema kasi ya maendeleo ya Zanzibar, itatiwa mbolea na maridhiano hayo.

Khatib ambae pia kwa sasa ni Mjumbe wa kuchaguliwa na rais wa baraza la Wawakilishi, anasema suala la maridhiano, yaliofikiwa Zanzibar ni ukomavu wa kisiasa kwa wazanzibari.

Anasema zipo nchi kadhaa wananchi wake wamekuwa wakizihama baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, kutokana na mchafuko na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ‘civil war’ ingawa Zanzibar hali ni shuwari.

“Sisi ADA-Tadea kwanza tunaunga mkono maridhiano hayo, tukiamini kuwa, maendeleo ya kweli, uchumi wa bluu na Zanzibar ya viwanda, haiwezi kujengwa kwenye machafuko, chuki na kubaguana,’’anafafanua.

Mwenyekiti wa Chama cha UMMA Mkoa wa kusini Pemba Mrayam Saleh Juma, anasema suala la kuwepo kwa maridhiano hayo ni jambo jema, kwani wakosanao ndio wapatana nao.

Anasema, kwa upande wao watahakikisha wanawaelimisha wananchi, ili kuona maridhiano yaliofikiwa Zanzibar, yanakuwa endelevu, kwa maslahi mapana ya wazanzibari wenyewe.

Anasema, ingawa zipo kasoro zilizojitokeza, lakini sasa ni vyema kwa wananchi wa Zanzibar, kuungana pamoja ili kuhakikisha wanaijenga nchi yao, kwa maslahi mapana ya taifa.

“Sisi kama Chama cha UMMA, tunayaunga mkono maridhiano hayo, maana bila shaka waliofikiria kukutana ni kwa ajili ya maslahi ya watu wote,’’anafafanua.

Ingawa nae alipendekeza, ni vyema maridhiano hayo yasitafsiriwe kama vile ni ya vyama viwili ya ACT na CCM, bali ni vyama vyote na wazanzibari wote.

Hata Mwenyekiti wa chama cha wakulima ‘AAFP’ Said Soud Said, amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari, akiwataka wazanzibari kuunga mkono maridhiano hayo.

MAKUNDI MENGINE YA KIJAMII YANASEMAJE

Mufti wa Zanzibar sheikh Saleh Omar Kaabi, amewasisitiza viongozi wa dini ya kiislamu na wale wa kikiristo, kuendelea kuzitumia nyumba za ibada, kuhubiri umoja, mshikamano, maridhiano na amani, kwani huo ndio utamaduni wa waumini.

Akizungumza hivi karibuni, kwenye kongamano la amani, lililofanyika Chake chake na kuandaliwa na Kamati ya pamoja ya viongizi wa dini Zanzibar, suala la kuishi kwa upendo, umoja, mshikamano, maridhiano na kusameheana ndio nguzo kuu kwa waumini.

“Sisi viongozi wa dini, ambao kila siku tunakutana na waumini wetu kwenye nyumba za ibada, tuendelee kuwanasihi kuishi kwa upendo, amani, maridhiano na mashikamano,’’alieleza.

Mapema Father Damas Mfoi, kutoka Kanisa Katoliki Unguja, anasema, umoja na mshikamano unahusisha dini zote, hivyo hakuna haja ya kubaguana.

Alisema, kila dini inahimiza umoja, mshikamano na kuishi kwa kusaidiana, hivyo ni vyema wakashirikiana, ili jamii ya Zanzibar isigawanyike, kwa sababu ya kuamini dini waipendayo.

“Sisi wajumbe wa Kamati ya pamoja ya viongozi wa dini Zanzibar, tunashirikiana bila ya kujali imani zetu, lazima na wananchi wote, tuwahubirie amani, maridhiano na upendo,’’alieleza.

Kwa upande wake Father Zeno Marandu kutoka Kanisa la Roman Katoliki ‘RC’ Chake chake, anasema ushirikiano ndio msingi mkuu wa maisha ya mwanadamu.

“Lazima tuishi pamoja, tuishi kama kiwili wili kimoja, na imani zetu za dini zisitugawe, kwani hakuna dini inayohimiza chuki wala mfarakano,’’alieleza Zeno.

Akaenda mbali zaidi, akashauri kuwa maridhiano yaliofikiwa kwa viongozi wakuu wa vyama vya siasa kufanya kazi pamoja, ni silaha ya kumshinda adui.

Sheikh Nassor Hafidh Mohamed wa Mkoani, alisema maridhiano yaliofikiwa, kila mmoja yanamgusa kwani amani na utulivu ni tunda la watu wote.

Hivi karibu Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba ‘PPC’ kwa kushirikiana na shirika la Intenews, liliwawezesha waandishi wa habari, kuandika habari za maridhiano na amani.

Ambapo kwenye mkutano huo wa siku moja, mwandishi mwandamizi Khatib Juma Mjaja, aliwakumbusha waandishi hao kuwa wabunifu wa uteuzi wa maneno.

Anasema, hata kalamu ya mwandishi wa habari, inaweza kuviza maridhiano na amani iliyopo Zanzibar, ikiwa hawatokuwa waangalifu.

“PPC kwa kushirikiana na Internews wameona ni bora kuwajengea uwezo nyinyi waandishi wa habari hapa kisiwani Pemba, katika kipindi nchi ikiwa kwenye maridhaino musiwe chanzo cha kuharibu yale yaliofikiwa na viongozi wetu wakuu,’’alisema.

Waandishi wa habari Kheir Juma Basha na Juma Mussa Juma, walisema, jambo lililofanywa na PPC na Internews ni jema.

                    Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch