Skip to main content

ABDALLA HUSSEIN WA PEMBA, ULEMAVU MCHANGAYIKO HAUKUWA UKUTA KUPATA ELIMU

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA

ABDALLA Hussein Rashid, ni kijana mwenye ulemavu wa mchanganyiko, sasa yuko darasani, akijumuika na wenzake kusaka haki yake ya elimu.

Hakuna aliyefikiria kwamba, kijana huyo engefikia darasa la kumi (FII) skuli ya sekondari Kinyasini, maana changamoto ya mwendo, ukosefu wa mkalimani yote ameyavaa.

Abdalla miaka 18, alizaliwa akiwa na mguu mmoja, huku akiandamwa na uziwi na ulemavu wa matamshi, ambapo mama yake mzazi hakuwa na tamaa ya kupata elimu kwa mtoto wake.

SAFARI YA MAISHA YA ABDALLA

Baada ya kuzaliwa miaka 18 iliyopita kijijini kwao Kwale Gongo Wete Pemba, mama mzazi alianza safari ya kila hospitali, ili kuhakikisha tatizo la mguu linapona.

“Nilifika na mwanangu hospitali ya Unguja, baada ya kuzimaliza za Pemba, ingawa kisha, akiwa ni miaka mitatau alianza kutumia mguu wa bandia,’’anaeleza mama yake.

Mama yake Abdalla, bibi Time Kombo Juma ambae huyo ni mtoto wake wa wanne , anasema safari ya mtoto wake, ilikuwa ni ya kukata tamaa zaidi kuliko mafanikio.

Mguu wake wa bandia, aliyopewa baada ya miaka mitano, alilazimika kuuwacha kutokana na kuendelea kumuumiza sehemu ya kifundo cha mguu.

Ambapo, kutokana na kukosa shilingi 500,000 za kununua mguu mwengine kwa wakati huo, sasa kijana wake alianza kutumia magongo maalum.

“Magongo yalikuwa yanamsaidia kwenda safari zake za hapa na pale, na hadi pale alipoanza madrassa mwaka 2012 na kisha mwaka 2014 alipoanza safari ya elimu ya msingi,’’anasema.

ABDALLA NA SAFARI YA ELIMU

Mwaka 2015, wakati akiwa na usaidizi wa magongo, alilazimika kutembea kilomita 5 kila siku za kwenda na kurudi skuli, masafa yaliopo nyumbani kwao hadi skuli ya Kinyasini.

 “Ilinibidi kila siku nitoke mapema mno kwenda skuli, kwa sababu magongo kama visaidizi hupati kwenda haraka haraka, lakini sikuwa kuchelewa skuli hata siku moja,’’anasema.

Nikiwa karibu na mama yake mzazi, akinisaidia ukalimani kwa Abdalla ambae kwa sasa ni mwanafunzi wa darasa la 10 (FII) skuli hiyo ya Kinyasani, anasema hamu yake ni kuwa fundi.

Nipotaka kujua ufundi wa aina gani, anasema ule unaokusanya masuala ya umeme iwe redio ama simu, kazi ambayo kwa sasa anendelea kuonesha utundu wake.

Mara anaporejea kutoka masomoni, hukusanya redio, Baskeli na simu mbovu kuanza kuzirekebisha na zipo anazofanikiwa, na kujiingiza fedha japo ndogo.

Changomoto anasema anyoivaa akiwa masomoni kuanzia darasa la kwanza hadi leo hii akiwa darasa la kumi, ni kukosa mkalimani wakati mwalimu akisomesha.

“Wenzangu wananiacha nyuma mno, na kila mwaka mimi huwa mwanafunzi wa mwisho, maana inabidi nimuangalie mwalimu mdomo mwanzo mwisho,’’anasema.

Tunu yake kwanza ni kuona anasonga mbele na kufikia hadi chuo kikuu, ili aisaidie familia yake, ambayo anasema imefanya juhudi kubwa hadi leo kufikia elimu ya darasa la 10.



Abdalla ni kijana wa aina ya pekee kutokana na kutopenda kukata tamaa, na kuwataka wenzake hasa wenye ulemavu ,atambue wajibu wao.

“Kama skuli yangu ya Kinyasini yengenipatia mkalimani kuanza darasa la kwanza hadi leo hii, mbona mimi ningewabeba wote wanafunzi darasani,’’anafafanua.

MWANAFUNZI MWENZAKE

Amour Hamad Issa anasema ,ubongo wa Abdalla uko vyemo mno, ingawa changamoto iliyopo ni ya wizara ya elimu kwa kukosekana kwa wataalamu.

Pamoja na kwanza pia Abdalla ni kiziwi, lakini yapo baadhi ya masomo mimi kama darasani sikwenda ananifahamisha yeye.

RAFIKI WAKE WA MTAANI

Omar Hassan Ali, anasema mara Abdalla anaporudi skuli, anautamaduni hadi leo  kukimbilia  madrasa, na amekuwa na juhudi kuliko mtu mwengine mtaani kwetu.

Kazi kubwa ambayo huwenda ikamganda hapo baadae ni ufundi, mara anatengeneza tv, simu, redio na hata suala la kuchonga chonga haliko mbali nae.

“Kama serikali inawajali kwa vitendo watu kama Abdalla, suala la mitihani ya darasani kwao isiwe kigezo cha kufaulu na kufeli, bali waangaliwe wanachofanya,’’anashuri.

MAMA MZAZI

Anasema kwa alipofikia mtoto wake hadi darasa la kumi na mwishoni mwa mwaka kufanya mitihani, ni hatua moja kubwa.

“Kwakweli kama asipofaulu hatujajua tufanye nini, maana kutokana na hali yetu ya kimaisha, tunahitaji msaada wa hali na mali ili afikie ndoto zake,’’anasema.

Akili yake inatuma na kushika vizuri mno, lakini sasa miundombinu ya elimu kwa ajili ya watu kama Abdalla, haipo skuli ya Kinyasini.

MWALIMU WAKE

Asha Mbaruok Rashid ndio mwalimu wake skulini hapo, anapochukulia elimu kijana Abdalla mwenye ulemavu mchanganyiko, anasema changmoto ni kutokuwepo mwalimu mwenye mbinu.

“Ijapokuwa skuli yangu ina walimu 12, lakini hakuna hata mmoja aliyewahi kupata mafunzo ya utaalamu wa kuwasomesha wanafunzi wenye ulemavu kama Abdalla,’’anasema.



Bidii, nidhamu, heshima na hamu ya mwanfunzi Abdalla, imekuwa ikikatishwa tamaa na wizara, kwa kule kutokuwepo kwa waalimu wenye sifa.

“Darasa analosoma Abdalla linawanafunzi 42, lakini kila mwaka tukipima matokeo yeye anakuwa anashika mkia, inasikitisha,’’anasema.   

 MWALIMU WA MADRSAA

Mwalimu wa Madrasa anayosoma Abdalla, ustaadh Omar Hussein Rashid anasema, licha ya vikwazo vinavyomkabili, lakini anabidii na anaonesha anahamu ya kusoma.

“Pamoja na ulemavu mchanganyiko, lakini kwa sasa mas-hafu ameshakaribia kuumaliza, na ameshasoma juzuu 18, na anaendelea na hajakatisha,’’anasema.

WANAFUNZI WENZAKE

Nao wanafunzi wanaosoma na Abdalla, walisema hana shida wamekuwa wakishirikiana nae, licha ya kwamba kuna baadhi ya wakati hawamuelewi vizuri, lakini wamekuwa wakimpa ushirikiano makubwa.

JIRANI WA ABDALLA

Said Asaa, anasema kuwa kwanza wanawashukuru wazazi wa Abdalla kuwa hawajambaguwa mtoto wao huyo, na wanampatia kila haki yake ikiwemo ya elimu.

 Licha ya ulemavu alionao Abdalla, lakini ukimuangalia unaona ni mtu mwenye uwezo mkubwa na bidii ya jambo analohitaji kulipata, na ni muelewa kuliko vijana wengine.

Hata hivyo mzee huyo aliwashauri wazazi wenye watoto kama hao, kutowabaguwa kwani Mwenyeezi Mungu ameshawajaalia waupokee mtihani huo.

BARAZA LA TAIFA LA WATU WENYE ULEMAVU

Mratibu wa baraza la  taifa la watu wenye  ulemavu kisiwani Pemba Mashavu Juma Mabrouk, anasema  suala la uhaba wa walimu mjumuishi bado ni tatizo.

Hivyo ameishauri  wizara ya elimu kuwapa kipaumbele walimu ambao wamesomea fani ya ukalimani, wakati zitakapotokea ajira ili kuona changamoto hiyo imeondoka.

‘’Niishauri wizara ya elimu wakati itakapotoa nafasi za ajira kuwajiri walimu wengi waliosomea elimu mjumuishi, ili kuona wanafunzi wenye ulemavu kama wa Abdalla nawao wamefaidika na elimu,’’ anaeleza.

WIZARA YA ELIMU

Kaimu Mratibu Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha ‘EMSM’ Pemba Halima Mohamed Khamis, anasema ujio wa dhana hiyo, ndio iliyokomboa watoto wenye ulemavu na wale wenye mahitaji maalum, sasa kupata haki yao ya elimu.

Awali watoto wenye ulemavu wa aina mbali mbali, waliachwa bila ya kupatiwa elimu, kuanzia ngazi ya jamii na serikali kuu.

Lakini ilipofika mwaka 1991, serikali kupitia wizara ya Elimu, ilianzisha madarasa maalum, kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa akili, ambapo kwa Pemba ni skuli za Michakaini na Pandani msingi.

Kisha mwaka 2006, sasa kukazaliwa dhana ya elimu mjumuisho, ambayo ni ule mpango wa kuwaweka darasa moja, kati ya wanafunzi wenye mahitaji maalum na wale wengine.

Mpango huo ulianza kwa kusua sua, maana ulikuwa mpya kwa wanafunzi wenye mahitaji na wale wengine, ambapo hadi sasa, wapo waalimu watano wenye  Master’ 10 wenye shahda ‘Degree’ wakati wenye diploma 20 na 68 ngazi ya cheti wote wana fani ya Elimu ya Mahitaji Maalum ‘SNE’

‘’Licha ya takwimu hiyo, lakini bado tunashida ya walimu mjumuisho, hivyo tunaiomba wizara husika kuliweka somo la lazima katika vyuo, ili kila mwalimu akitoka chuoni aweze kusomesha wanafunzi wenye ulemavu,’’anasema.



Wanafunzi wenye uoni hafifu 803, wenye usikivu hafifu 690, wenye ulemavu wa matamshi 405, wenye vichwa vikubwa na vidogo 22 wakiendelea na masomo katika skuli mbali mbali kisiwani Pemba.

Kundi jengine ni wenye umbilikimo 13, mgongo wazi saba , ulemavu wa akili 111, ulemavu mchanganyiko 113 na ulemavu wa viungo wanafunzi 91.

 SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU

Haki ya elimu, imetajwa kwenye kuanzia kifungu cha 9 hadi cha 10 sheria ya watu wenye ulamvu Zanzibar nambari 9 ya mwaka 2006.

“Chuo kitachotoa mafunzo lazima kizingatie mahitaji maalum kwa watu wenye ulemavu, ikiwemo mtaala, alama, mitahani, vifaa husika,’’ndivyo sheria inavyoeleza.

 Ingawa sheria iko kimnya juu ya hatua zinazofaa kuchukuliwa na mtu mwenye ulemavu, iwapo amekwenda chuoni au skuli na hakuna miundombinu rafiki.

Abdalla alizaliwa miaka 18, kijijini kwao Kwale Gongo wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, akiwa ni mtoto wa 4 kutoka  kwa familia ya bwana Hussein Rashid.

MWISHO.

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch