Skip to main content

VYOMBO VYA HABARI, DARAJA LA KUJENGA AMANI YETU ZANZIBAR VIKITUMIKA VIZURI

 



NA HAJI NASSOR,  PEMBA

IKUMBUKWE kuwa, mwaka 2010 na hasa baada ya marakebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilifuta nafasi ya Waziri Kiongozi, kuwa kama mtendaji mkuu wa serikali.

Na hapo sasa, ikamtambua Makamu wa Pili wa rais kuwa ndie atakaekuwa mtendaji mkuu wa serikali, ingawa imeongeza kiongozi mwengine anaitwaye Makamu wa Kwanza wa rais.

Huyu mwenyewe, hutokana na kile chama kilichoshika nafasi ya pili, kwenye chaguzi mkuu wa vyama vingi nchini, na Katiba ikimtaja kuwa atateuliwa na rais.

Kumbe wa Zanzibar suala la kuwa na serikali ya Umoja wa Kitaifa sio geni, wala huu mwaka 2020 sio mara ya kwanza, maana ilianza mwaka 2010.

Ingawa mwaka 2015, ilisita kidogo kwa sababu za hapa na pale, lakini mwaka huu tena, chini ya rais wa Zanzibar wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi akitokea chama cha Mapinduzi ‘CCM’ imerudi tena.

Na kwasasa, (marehemu) Makamu huyo wa Kwanza wa rais ni yule yule aliyeanza mwaka 2010, ingawa kwa sasa akihudumu ndani ya chama cha siasa cha ACT-Wazalendo.

Zanzibar imekuwa ikitofautisha na mataifa kadhaa ya Afrika kama vile Burundi, kwamba zinapotokezea hitilafu za ndani yenyewe, hukaa chini na kutatua jambo hilo.

Na ndio maana, kwa sasa ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa ‘SUK’ na hasa baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, viongozi wetu wapendwa Maalim Seif Sharif Hamad na Dk. Hussein Ali Mwinyi sasa wanafanya kazi pamoja.

Wote wakati wa kunadi sera zao, walishaawahidi wananchi wa Zanzibar kuwa, watahakikisha wanawaunganisha wazanzibari wote, kwa kuwaweka pamoja kwa upendo, ili kuchapuza maendeleo.

Nakumbuka sana mwezi Oktoba mwaka 2020, wakati alipokuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk. Hussein Ali Mwinyi, uwanja wa Gando Wete, aliahidi kuwaunganisha wazanzibari.

“Kama mkinichagua kuwa rais wa Zanzibar, pamoja na mambo kadhaa, pia nawaahidi kuwaunganisha wazazibari, ili kuona tunakuwa kitu kimoja na neema tuitumie wote,’’alisema Dk. Mwinyi.

Akaenda mabali zaidi, akisema mshikamano wa wazanzibari ndio jambo la mwanzo, maana wanapotengana inakuwa vigumu hata kuwatumikia, kwa kuwaletea maendeleo.

Maneno kama haya, pia yalitamkwa na aliyekuwa mgombea wa urais wa Zanzibar marehemu Maalim Seif Sharif Hamad kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, wakati akiwa kwenye uwanja wa mkutano Ditia Wawi Chake chake.

“Kwanza, mkinichagua nitahakikisha umoja, mshikamano, maridhiano ya wazanzibari ndio jambo la kwanza, na ndio kipaumbele changu kama mkinichagua,’’alisema wakati huo Maalim.

Akafafanua kuwa, wazanzibari ni watu wastaarabu, wapenda umoja, mshikamano na hawapendi kugawanywa, wala kuishi kwa chuki hivyo nae azma yake ni kuwaleta pamoja.

Haya ya viongozi wetu wapendwa, yamedhihirika Disemba 8, mwaka jana, kwenye hafla ya kuapishwa kwa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad ambae sasa ameshatangulia mbele ya haki.

Ambae aliweka mbele maslahi ya taifa na kuwaangalia wazanzibari wote waliopo nje na ndani, na kukubali kwa moyo mkunjufu, kuwa sehemu ya serikali ya Umoja wa wa Kitaifa Zanzibar ‘SUK’.

Wazee wa zamani wana msemo wao kuwa, waungwana wawili daima hawapoteani, na wengine wakasema chanda chema huvishwa pete, hapa utaona Dk. Mwinyi na Maalim Seif ni waungwana wawili waliopoteana na kisha kuonana.

Sasa Zanzibar kuanzia Disemba 8 ya mwaka 2020, inaendeshwa kwa mfumo wa serikali ya pamoja, kwa lengo la kuchapuza maendeleo ya wazanzibari wenyewe.

 Na ndio maana marehemu Maalim Seif amesema dhamira ya yeye na Rais wa Zanzibar, Dk. Husein Ali Mwinyi kufanya kazi kwa pamoja ni kuondoa yale madhaifu yote, ambayo hupelekea wazanzibari kutofautiana na kuleta chuki miongoni mwao.

Anasema, kuwepo kwa Serikali yenye muundo wa umoja wa kitaifa, ni njia moja ya kubaini sababu ya kupata dawa kulinda tena Zanzibar isirejee katika migogoro isio ya lazima.



VYOMBO VYA HABARI VINAFANYAJE KULINDA AMANI NA MARIDHIANO NA MIGOGORO?

Kwa Pemba, waandishi wa habari kuanzia mwaka 2002 waliamua kuanzisha Klabu yao, inayojulikana kwa jina la Klabu ya waandishi wa Habari Pemba PPC.

Ambapo pamoja na mambo mengine ni kutaka kuwajengea uwezo waandishi wa habari, waandaji wa makala ili kuripoti habari zilizoshiba.

Ndio maana hata hivi karibuni PPC katika kufanikisha hilo, ilishirikiana na Shirika la Internews na kuandaa mkutano wa kuwajengea uwezo waandishi namna bora ya kuandika habari za amani na maridhiano.

Mkutano huo wa siku moja, ambao ulifunguliwa na Mwenyekiti wake Bakari Mussa Juma, na kufanyika Chake Chake, aliwaambia waandishi kuwa unalengo la kuwajengea uwezo.

“Mkutano kama huu sio wa mwanzo wa kuwajengea uwezo nyinyi waandishi na lazima nilishukuru Shirika la Internews kwa kukubali kushirikian na sisi,’’anasema.

Mwandishi mkongwe Khatib Juma Mjaja, ndie aliwakumbusha mbinu waandishi hao, namna bora ya kuandika habari za maridhiano na amani.

“Tusitumie maneno ya kejeli, dharau, kukebehi tunapoandia habari, makala na utengenezaji vipindi kwani maridhiano yaliofikiwa Zanzibar yameangalia maslahi mapana ya nchi,’’alisema.

Moja kati ya eneo linalotegemewa mno na kila ili kufikisha ujumbe wa kwa haraka ni kwenye vyombo vya habari, kwa kule sauti na upeo wao kufika mbali tena kwa haraka.

Wapo wanaoamini kuwa chombo cha habari ni kama kisu au panga, kikitumika vibaya kinaweza kuwa janga na kusababisha taharuki, ingawa kikiwa kizuri huwa furaha na upendo kwa wote.

Hapa Meneja wa redio Jamii Micheweni Ali Massoud Kombo, anasema katika kuhakikisha wanayaenzi, kuyalinda maridhaino sambamba na kutunza amani na utulivu, wanaandaa vipindi mbali mbali.

Anasema, wao kama redio ya kijamii wamevutiwa na kupendezewa mno, na namna ya uwepo wa serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, akiamini ndio suluhisho kwa maendeleo ya kweli.

Anasema, wameanzisha kipindi chao ambacho huwa kizungumzia umuhimu na faida za maraidhiano kwa wazanzibari, sambamba na utunzaji wa amani kama chachu ya kufikia maendeleo hapa Zanzibar.

Kipindic hao huruka hewani kila wiki mara mbili, (Ijumaa na Jumatatu), ambapo jina la kipindi hicho ni ’itunze amani yako’ ambapo huwa baina ya dakika 30 hadi 45.

Anasema hutegemeana na aina ya wasemaji, ambapo kwa mfano kama wiki iliyopita, walikwenda hewani hadi dakika 55, walipoweka mada ya ‘umuhimuwa maridhiano’.

“Sisi tunazungumzia amani na maridhiano kwenye kipindi hicho, maana kilichofanywa na viongozi wetu ni jambo jema na hasa kwa maslahi ya wazanzibari,’’anasema.

Hapa anawakaribisha wanaharakati, wanasiasa, wanasheria na jamii yote kuzitumia dakika 45, bila ya malipo kuzungumza na jamii ya Micheweni, juu ya umuhimu wa kutunza na kuyaenzi maridhiano.

Pamoja na vipindi hivyo maalum, Meneja huyo wa redio Jamii Micheweni, anasema wamekua wakiandika habari za umuhimuwa maridhiano na nafasi jamii katika kuendeleza hilo na amani kwa ujumla.

Lakini sio redio Jamii Micheweni pekee, wanaoendesha vipindi vya aina hiyo, lakini kwa mujibu wa mtengenezaji vipindi wa kituo cha redio cha Istqama Othman Ali Juma, nao wanaendesha vipindi vya aina hiyo.

Anabainisha kuwa, kila siku wanamkusanyiko wa matukio kupitia jina la kipindi baraza ya ‘V.I.P’ ambapo ndani yake huelezea faida za kutunza amani na utulivu.

Wameamua pia kuelezea maridhiano kwa mfumo wa kuwaacha wasikilizaji wakipiga simu ‘live’, ili kuhakikisha wanatoa maoni yao, ingawa wote wanaonesha kuridhishwa na maridhiano hayo.

“Inaonekana wananchi kwa kule kuzingatia maslahi mapana ya Zanzibar, wanaunga mkono serikali ya Umoja wa Kitaifa wakiamini ndio msingi mkuu wa maendeleo,’’anasema.

Kaimu Meneja wa Redio Jamii Mkoani, Said Omar Said, anasema kwa muda mrefu ndani ya kituo chake, wanaendesha kipindi cha utawala bora, ambapo hukusanya mambo kadhaa yakiwemo amani na utulivu.

“Sasa baada ya kuwepo kwa maridhiano ya kisiasa Zanzibar, na sisi tumebadilisha mwelekeo, hivyo kila Jumanne huwa tunadakika kati ya dakika 30 hadi 45 tukigusia maridhiano,’’anasema.

Akiongeza kuwa, mfumo wa kipindi hicho huwa kwa mfumo wa kurikodi na wakati mwengine kwenda mubashara ‘live’ ili kuwapa nafasi wasikilizaji kutoa maoni yao.

“Wengi wa wasikilizaji wetu wanaonesha wamevutiwa mno na Malim Seif, kukubali kuingia kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa, ingawa wakiomba mamlaka husika kusimamia hilo,’’anasema.

Amesema wataendelea kutengeneza vipindi vya kuhamasisha jamii maridhiano hayo, kwa vile ndio mwarubaini wa kuwa na siasa za ustaarabu na kuvumiliana.

Juma Mussa Juma, anatengeneza kipindi cha sauti ya amani kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar ‘ZBC’, ambapo anasema hukusanya makundi mbali mbali.

Kwa mfano wiki iliyopita, aliendesha kipindi na vijana juu ya kujadili nafasi yao, katika kuitunza, kuiendeleza na kuiheshimu amani iliyopo Zanzibar.

Changamoto ambayo ipo masikioni kwa vijana, awali walidhani kua suala la amani na utulivu kwa ajili ya kipindi cha siasa, na mwanzo walikuwa woga kuzungumza baadae walielewe.

“Kwa sasa, najitayarisha kuongeza suala la maridhiano ndani ya kipindi hiki, ili kuzungumza na makundi mbali mbali juu ya umuhimu na faida za maridhiano yaliopo Zanzibar,’’anasema.

NINI KIFANYIKE KUENDELEZA MARIDHIANO, AMANI ZANZIBAR?

Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Harusi Miraji Mpatani, wakati akfungua mafunzo kwa waandishi wa habari kupitia mradi wa Jenga amani Yetu, alisisitiza haja ya kuridhiana.

“Migogoro huzaliwa baada ya jamii kutopenda kuridhiana, ambapo sasa hata viongozi wetu wakuu wameona ipo haja hilo kufanyika,’’alieleza.

Hata mradi wa jenga amani yetu, ni eneo moja la kuona makundi ya jamii yanapata uwelewa na sasa kufungua ukursa mpya.

Wapo wanaoona kuwa, elimu kwa jamii inahitaji kwani, bado wapo wanaodhani kuwa, suala la kuendeleza maridhiano ni jambo la kisiasa na sio utamaduni.

Haji Khamis Mussa wa Wawi, anasema elimu ya kuitambua vyema serikali ya Umoja wa Kitaifa, isambaazwe hasa kwao vijana, ili iwe rahisi kuwafahamisha wengine.

Ingawa hivi karibuni, Mufti Mkuu wa Zanzibar sheikh Saleh Omar Kaabi, wakati akifungua kongamano la viongozi wa dini ukumbi wa kiwanda cha Makonyo Wawi, alisema utamaduni wa maridhiano, upo wa asili.

Alibainisha kuwa, utamaduni wa wazanzibari tokea asili, walijengeka kwa kuvumiliana, kusameheana, kupendana, kukosoana na kuridhiana, ili jambo fulani liende mbele.

                        Mwisho  

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch