Skip to main content

DC: CHAKE CHAKE 'TENGENEZENI MAZINGIRA RAFIKI SASA KABLA YA UZEE'

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

JAMII nchini, imeshauriwa kutengeneza mazingira rafiki sasa ikiwemo utoaji wa huduma kwa nusu gharama, ili ndugu na jamaa zao watakapofikia umri wa uzee, iwe rahisi kuyatumia mazingira hayo, bila ya vikwazo.

Ushauri huyo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alipokuwa akizungumza na wanajumuia ya Wazee na wastaafua Zanzibar ‘JUWAZA’ kwenye mkutano wa mashauriano wa utekelezaji wa haki za wazee na wastaafu, uliofanyika Chakechake.

Alisema, hivi sasa kila mmoja hajaona umuhimu wa kuweka mazingira hayo rafiki na ya kudumu, kwa ajili ya wazee waliopo sasa, hadi hapo umri utakapofika na kuanza kukumbana na changamoto.

Alieleza kuwa, kila mmoja na kwa nafasi yake, awe serikalini au tasisi binafsi, anapaswa kutengeneza mazingira sasa, ili akifikia uzee, apunguze vikwazo kwenye shughuli zake.

“Kwa mfano hata hospitali zetu, zianze sasa kuweka madirisha maalum kwa ajili ya wazee, wenye vyombo vya usafiri waanze na nusu nauli, au kuondoa foleni kwa wazee kwenye misururu ya kupiga kura,’’alipendeleza.



Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya alisema, kwa upande wake serikali, imekuwa ikijitahidi kuweka mikakati ya kuwasaidia wazee hao, ikiwa ni pamoja na pencheni jamii.

“Ndio maana hata sasa kunamchakato unaendelea kuona wanaonufaika na pencheni jamii ya shilingi 20,000 kila mwezi sio lazima utimize miaka 70 hata kati ya 65 na 60, iwe wote wananufaika,’’alieleza.

Hata hivyo alipendekeza kuwa, wakati umefika sasa kwa wazee wa Zanzibar, kuwa na nafasi maalum ya uteuzi ndani baraza la wawakilishi, ili waelezee changamoto zao.

Katibu wa ‘JUWAZA’ Ghanima Othman Juma, alisema wanataka wapewe kipaumbele kila eneo, kuanzia ngazi ya shehia, jimbo, wilaya mkoa na taifa.



“Kwa mfano, tunapofika kipindi cha kwenda kwenye uchaguzi, tushirikishwe, utungaji wa sera mbali mbali, uandaaji wa bajeti ya nchi na hata suala la uteuzi wa miradi,’’alipendekeza.



Nae Mjumbe wa Kamati tendaji wa ‘JUWAZA’ Amina Shaaban, alisema wamekuwa wakiwafuata viongozi kadhaa, ili kuona wazee wanakuwa na ahuweni ya maisha.



“Hivi sasa, tumeshapanga kuonana na Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar, kunachangamoto tunataka kumfikishia, maana hata hili suala la pencheni jamii inayotolewa sasa, ni juhudi za JUWAZA,’’alieleza.

Akiwasilisha mada kwenye mkutano huo, mtoa mada Omar Mohamed Ali, alisema wazee wanamchango mkubwa kwa taifa, hasa kwa uwelewa wao.

Wakichangia mada kadhaa, wazee hao akiwemo Daud Ali Hamad kutoka Konde, alisema bado kuna changamoto kwenye ulipaji wa fedha za pencheni jamii, kwa kupewa wengine ambao hawajatimiza miaka 70.


Mzee Omar Ali Khamis alisema, Mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar ‘ZSSF’ haujawatendea haki wa kukosa kuwaongezea pencheni yao, licha ya kulitumikia taifa kwa muda mrefu.



“Hata ‘ZECO’ na ‘ZAWA’ kwenye huduma zao hawajawajali wazee, iwe kwenye malipo au kuingiwa huduma, kunauzembe unafanyika,’’alieleza.

Sensa iliyofanyika ya watu na maakazi ya mwaka 2012, ilionesha Zanzibar kuna wazee wenye umri wa miaka 60 na kuendelea wapatao 58,311 wanawake 28,424 na wanaume 29,887.

Eneo jengine imeonesha kuwa, falimia 17 kati ya 100 zilizopo Zanzibar zinaongozwa na wazee, huku wazee 60 kila 100 imegungulika hawapati mapato ya kujikimu.

                     Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch