Skip to main content

VIJANA PEMBA WATAKA MARIDHIANO ZANZIBAR YAENZIWE KWA VITENDO KUKINGA NA MIGOGORO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA


 

…..hii sio mara ya kwanza, kwa gwiji wa siasa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, kuwa Makamu wa Kwanza wa rais ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 

Kabla ya kufutwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2015, Maalim Seif, kwa wakati huo akihudumu na Chama cha Wananchi CUF, alishika nafasi hiyo kutoka 2010 hadi 2015.

 

Wakati huo Dk. Ali Mohammed Shein wa Chama cha Mapinduzi (CCM), akiwa Rais wa awamu ya saba, akipokea kijiti hicho kutoka kwa muasisi wa maridhiono hayo Amani Abeid Karume.

 

Maalim, ameamua kurudi tena kuwa Makamu wa Kwanza, kwa sasa akiwa pamoja na rais wa awamu ya nane, wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

 

Kwa ustaarabu, uvumilivu, ukongwe wa kisiasa na kuweka mbele zaidi maslahi mapana ya wazanzibari, ndio maana Disemba 8, mwaka 2020, Zanzibar ilizaliwa tena upya.

 

Upya wake, unakuja maana licha ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kuanzia mwaka 2010 kutaka kuwepo kwa serikali ya Umaja wa Kitaifa, ‘SUK’ lakini hitilafu za hapa na pale mwaka 2015 ‘SUK’ haikuwepo.

 

Leo hii tukiwa ndani ya ‘SUK’ ni furaha na mbwembwe za wazanzibari, kwa kule viongozi wetu wakiamua kufanyakazi pamoja tena bila ya kujali vyama vyao, kwa hakika hili ni jambo jema mno.

 

Hapa sasa tunajufunza kuwa, Dk. Mwinyi ameshapandisha tanga la safari ya kuiongoza Zanzibar chini ya muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ‘SUK’ ukiwa unaendelea.

 

 Ni punde tu, tangu taifa hilo lenye mamlaka ya ndani, kutoka katika uchaguzi mkuu, uliomazika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka 2020.

 

Historia ya Umoja wa Kitaifa

Siasa za Zanzibar, daima huanza na moto mkubwa wa ushindani wa kisiasa na kisha kumalizika kwa maridhiano na maelewano makubwa.

 

Ndio maana, wazee walishasema wagombana nao ndio wapatanao, maana kwa Zanzibar kupatana ni pahala pake, kwa kule wananchi wake walivyoshiba demokrasia ya kwli.

 

Kumbe hata kabla ya Mapinduzi ya 1964, Zanzibar chaguzi zake zilikuwa za ushindani mkubwa, ambapo kisha baada ya kurudishwa tena kwa mfumo wa vyama vingi 1992 ushindani wa kisiasa, ukarudi kama awali.

 

Kwa wazanzibari, kama walivyo watu wa mataifa mengine, nao hukosana hapa na pale, ingawa wao hawawatumii wasuluhisi kutoka nje, bali wenyewe tu, basi na mwafaka hupatikana.

 

Moja ya jambo kubwa lililoafikiwa ni kuwepo kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, huku lengo kuu likiwa ni kuwaleta pamoja wazanzibari, ili waijenge nchi yao.

 


 Ndio maana, hata Makamu wa Kwanza wa rais wa Zanzibar, Jemedari Maalim Seif Sharif Hamad, akasema kilichowasukuma kukubali kushirikiana na serikali, ni kuwaleta pamoja wananchi na sio chengine.

 

“Leo tumeshafungua ukurasa mpya wa umoja, mshikamano, maelewano kwa wazanzibari sote, bila ya kujali vyama vyetu vya ACT, CCM wala CHADEMA kilichopo mbele yetu ni kuwaleta pamoja wazanzibari,’’alisema Makamu wa Kwanza hivi karibuni.

 

Kila mmoja ni shahidi kuwa, uchaguzi mkuu wa vyama vingi ule wa mwaka 2010, na 2015 na huu wa 2020 ulifanyika kwa amani kubwa tena bila fujo lolote, kwa kule viongozi wakuu kufahamiana.

 

 Uteuzi wa Maalim Seif umepokewa vipi?

Vijana wa kisiwa cha Pemba, wanasema kwanza ni jambo jema na zuri, kwa mkongwe huyo wa siasa kukubali kuingia ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa ‘SUK’.

 

Wanasema kauli za Rais wa Zanzibar, Makamu wa Kwanza, Makamu wa pili katika kuendeleza mbele Zanzibar, lazima zienziwe na zitunzwe kwa vitendo na kila mmoja.

 

Omar Khamis Haji miaka 26 wa Mtambile anasema, wameyapokea vyema maridhiano hayo, na sasa kilichobakia ni kwa kila mmoja, na kwa nafasi yake ayatekeleze kwa vitendo.

 

Kama alivyo Omar, na hata Khamis Muhidini Juma 30 na Fauzia Kheir Hassan miaka 21 wa Kipapo, wanasema kilichobakia wao kama vijana, ni kuhamasishana ili kuendeleza mbele maridhiano hayo.

Hata Mohamed Khamis Juma miaka 34 wa Wete Limbani, anasema, maendeleo ya vijana hayatopatikana, ikiwa nchi haina maridhiano miongoni mwao.

 


“Sisi tunawategemea viongozi wetu, watusafishie njia za kutimiza ndoto zetu, sasa kama hakuna maridhiano, umoja na mshikamano ni vigumu kusimama,’’anasema.

 

Hata Siti Mohamed Omar wakati akizungumza kwenye kongamano la amani lililofanyika Wesha hivi karibuni, alisema wameridhishwa mno na uwepo wa serikali ya Umoja wa Kitaifa.

 

“Hii ni ishara kubwa kuwa, sasa ile Zanzibar yenye neema itafika pahala pake, maana matakwa ya Kikatib ya uwepo wa serikali ya Umoja wa Kitaifa yameshafanyika,’’anasema.

 

Mwenyekiti wa Jumuiya sauti ya Vijana Pemba Said Mussa Rashid, anasema vijana wako wazi kuona maridhiano hayo yanafanyiwa kazi.

 

Anasema, watahamasishana kama vijana, kuona kwanza umoja, mshikamano, amani na maridhiano hayo yanakuwa endelevu kwa maslahi mapana ya taifa.

 

Hivi karibuni, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar sheikh Mahamoud Mussa Wadi, akifungua kongamano la amani kwa vijana, alisema wao wana nafasi kubwa ya kutunza amani na utulivu.

 

Anasema vijana ndio kundi kubwa na lisilotabirika katika nchi yoyote, sasa lazima waelewe nafasi yao, na kuhakikisha hawaitendei vibaya nchi yao.

 

“Sasa uchaguzi mkuu wa vyama vingi umeshamalizika, na viongozi wameshapatikana na serikali ya pamoja imeshaundwa, ni wajibu wa vijana sasa kusaka fursa,’’alieleza.

 

Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba Ahmed Khamis Makarani, anasema lazima vijana wasikubali kutumiwa ovyo ovyo, hasa kwenye kuelekea kuyatia doa maridhiano na amani ya Zanzibar.

 

Kamanda huyo, aliwasisitiza vijana, kuwa wanapoilinda amani iliyopo, ndio mwenye kazi ya boda boda, kilimo, afya, uvuvi na usanii ataifanya kwa ufanisi.

 

“Sasa uchaguzi umeshamalizika, kila mmoja kwa nafasi yake na alipo, awe balozi mzuri wa kuilinda amani, maridhiano na hasa hawa vijana maana ni wepesi kuharibika,’’anasema.

 

Kwani hata rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, katika hutuba zake mbali mbali amekuwa akirudia kuwa, katika mazingira ya sasa ya siasa za Zanzibar, muundo huo wa serikali utasaidia pakubwa.

 

Anasema, kwani neema ambayo aliwahidi wananchi kwenye kampeni, haitowafikia ikiwa, nchi hiyo wananchi wake hawako kwenye mshikamano wa kijamii na utulivu wa kisiasa.

 

“Ndugu zangu, lazima tuelewa kuwa, amani, maridhiano na mshikamano ndio jambo moja kubwa na la kwanza, katika kufikia maendeleo ya kweli,’’anafafanua.

 

Hata Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, baada ya kula kiapo kushika nafasi hiyo, alisema hatovumiliwa yeyote, ambaye ataleta chokochoko za kuwagawa wazanzibari na kurudisha uhasama miongoni mwao.

Amewataka wananchi visiwani Zanzibar, kudumisha amani na umoja uliopo na kuwabeza wale wote wanaopinga umoja uliopo nchini, ili kuipatia nchi ya Zanzibar maendeleo kwa haraka.

Amesema kuwa, kuwepo kwa Umoja na Ushirikiano kwa wazanzibari, ni jambo muhimu katika nchi na kuwataka watu waachane na itikadi za mambo ya kisiasa katika masuala ya kusimamia maendeleo yao.

“Kama tukiwa wamoja ni rahisi nchi yetu kupiga hatua kimaendeleo, katika nyanja zote na kuwa mfano wa nchi nyingi za bara la Afrika,”ameeleza Maalim Seif.

Sambamba na hilo, Makamu huyo wa Kwanza wa Rais amewataka wazanzibar, kuacha ubaguzi wa rangi au wa kisiasa, kwani mbora mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mchaji zaidi.

Pia Maalim Seif, amesema dhamira ya yeye na Rais wa Zanzibar, Dk. Husein Ali Mwinyi kufanya kazi kwa pamoja ni kuondoa yale madhaifu yote, ambayo hupelekea wazanzibari kutofautiana na kuleta chuki miongoni mwao.


Amesema, kuwepo kwa Serikali yenye muundo wa umoja wa kitaifa, ni njia moja ya kubaini sababu ya kupata dawa ya kuilinda Zanzibar, isirejee tena katika migogoro isio ya lazima.

Kundi jengine ambalo limekuwa lipewa tahadhari, ili mardhiano yasiingie doa pamoja na vijana, lakini pia waandishi wa habari na kalamu zao.

Na ndio katika kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa weledi katika kuandaa vipindi, makala na habari Kituo cha Huduma za Sheria Zanzjbar ZLSC, kwa ufadhili wa EU chini ya tasisi ya Search for Common Ground na LHRC iliendesha mfunzo ya siku kadhaa kwa waandishi w ahabari.

Kwenye mkutano huo uliofanyika mjini Chake chake, waandishi waliohudhuria mkutano, waliahidi kuwa wabunifu na weledi ili kuhakikisha maridhiano na amani inamea Zanzibar.

Meneja kituo cha redio cha Zenj FM na Zenj TV, Is-haka Mohamed Rubea alipongeza hatua ya PPC na Internews kukutana na waandishi wa habari.

Nae Khadija Mahmoud Chande mwakilishi wa Channel Ten, alisema ukumbusho na mbinu walizopewa zimewapa ufahamu mkubwa.

Akizungumza kwenye mkutano huo Afisa Ufuatiliaji na tathmini wa mradi wa Jenga Amani Yetu Khamis Haroun Hamada, alisema wameamua kuwajengea uwezo waandishi, ili waandae vipindi na makala kwa uweledi.

                                    mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch