Skip to main content

AJIRA ZA WATOTO TUMBE PEMBA SIO TISHIO LA UVUNJIFU WA AMANI

 




NA HAJI NASSO,  PEMBA

 

ZANZIBAR ni muunganiko wa visiwa viwili Unguja na Pemba.

 

Kwa miaka mingi sasa visiwa hivi vimekua vikisifiwa katika suala uwepo wa amani ya kutosha visiwani humo.

 

Viongozi mbali mbali wa serikali, NGOs, mashirika na wadau wamaendeleo wamekua mstari wa mbele kuhimiza suala la amani na utulivu, kabla ya Uchaguzi, wakati na hata baada ya uchaguzi mkuu wa vyama vingi.

 

Tumekua tukizowea kuona uvunjifu wa amani hujitokeza zaidi kabla au baada ya kipindi cha uchaguzi mkuu wa vyama vingi, nakusahau muda mwengine na badala yake kutokea vurugu zinazoelekea kwenye mapigano.

 

Vipo viashiria vingi au sababu na maarufu vinavyopelekea uvunjifu wa amani kama vile kupindwa kwa demekrasia, kucheleweshwa kwa haki, ukosefu wa huduma za kijamii na ubaguzi.

 

Wengine husahau na wakati mwengine kupuuzia sababu za uwepo wa ajira za watoto kuwa zinaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini.

 

WAZAZI

Ali Mtwana Haji (57) ni mkaazi wa shehia ya Tumbe Magharibi,  anasema ajira za watoto sio chanzo cha uvunjifu wa amani, kama baadhi ya watu wanavyofikira.

 

Anasema ijapokuwa serikali inakataza  ajira, bado hakujatokea mapigano au mivutano katika maeneo watoto wanapofanyia ajira hizo.

 

“Mimi bado sijaona mikwaruzo yoyote bandarini kwetu, licha ya vijana baadhi ya siku kufukuzwa na kuwekewa vikwazo,”amesema.

 

Anasema tatizo ni kubwa bandarini kwao, nashangazwa na mikakati inayopangwa bandarini juu ya kuzuiliwa watoto kutokupara samaki, ilhali pesa wanazopata wanasaidia famili zao.

 

Mwaka Hamadi Mbwana mzazi (45) anasema ajira sio chanzo kwani kama inavyofiriwa, bali watoto wanachokipata hutumia na familia zao.

 

“Hatokua mwanangu akirudi anakuja na samaki na vijisenti kidogo, halafu ukamfukuza unataka akatafute pesa wapi, nakazi gani wakati hii ndio kazi nyepesi kwake,”anahoji.

 

Mjaka Hija Shaali (42) anasema kutokana na hali za maisha suala la ajira kwa watoto wao ni msingi mkuu wa kuendeleza familia zao.

 

“Naelewa kuwa ajira kwa watoto ni marufuku kuanzia kwa sheha hadi serikali kuu, na hua tunawakataza lakini hakujawahi kutokezea mivutano baina yetu na watendaji wa serikali,”anasema.

 

Anasema mwaka 2015 watoto walipofukuzwa, baadhi ya wazazi walipinga sana tukio hilo, huku akishutumiana na kuwekeana usahasama baina yao.

 

Mtumwa Rashid Kai (38) anasema ajira za utotoni chanzo cha uvunjifu wa amani, pale watoto wanapofukuzwa bandarini na wazazi kutokukubali na kuanza kujibizana.

 

“Tayari baadhi ya watu waliwawekeana uhasama na kusulushishwa, ili mradi watoto wao kuachiwa kuendelea na kazi zao za uparaji wa samaki,”alisema.

 

Ramadhan Hamad Juma (55)anasema ajira sio chanzo, bali ni mtu kama anataka kufanya matukio maovu anafanya bila ya kuwepo bandarini, kutokana na muda mrefu vijana wanapara samaki na hatujasikia mizozo yoyote.

 

WATOTO

Yussuf Hija Shaame (14)mkaazi wa Tumbe kaliwa,  anasema ajira za utotoni sio chanzo cha uvunjifu wa amani, na wapo muda mrefu bila ya kuhusishwa na matukio maovu bandarini hapo.

 

Amesema sisi wengi tuliopohapa kila mmoja anajuwa anachokifanya, licha ya baadhi ya wakati madalali hutufukuza ili tuwende skuli.

 

“Nisipokuja hapo basi nyumbani natetwa, ati watu watakula nini wadogo zangu, imekua ni kazi yangu ya kawaida kwa sasa ila muda wa skuli ukifika nishaondoka,”alisema.

 

Yassir Shaame Pandu (17) mkaazi wa chimba,  tuliwahi kufukuzwa ila baadhi ya wazazi walituombea tukaendelea kuwepo mpaka sasa, hapa sisi wengine tunajiepusha kuingia katika vikundi viovu huko mitaani.

 

“Kipindi tulipofukuzwa baadhi ya watu walitaka kupigana, kutokana na kutuzuia sisi kisingizio hatuendi skuli wala chuoni, kazi yetu kupara samaki tu”anasema.

 

Naye Chumu Ramadhan Heri (16) muuza Visheti bandarini Tumbe, anasema kutokana na hali ngumu ya familia yao, hanabudi kufanya biashara hiyo na fedha anazozipata zinasaidia nyumbani kwao.

 

“Hutokea baadhi ya siku watoto wanafurushwa hapa, zaidi muda wa skuli unapofika na wale wakaidi hukatazwa moja kwa moja kuwepo hapa,”amesema.

 

Pandu Jafar Ismail (18) anasema ajira sio chanzo cha uvunjifu wa amani, ni mtoto mwenyewe kama ni mkorofi basi atatimiza malengo yake popote pale na sio lazima bandarini hapa.

“Sisi tupo hapa muda mrefu wapo wanaokuja na wakiondoka fedha zao zinaishia kwenye madawa ya kulevya na mambo mengine,”alisema.

  WANUNUZI WA SAMAKI

 Ramadhani Haji Omar, anasema ukosefu wa elimu ndio chanzo cha wazazi kuwaruhusu watoto kujiingiza katika ajira, licha ya wengine kwenda kwa malengo binasfi, na wapo wanaokwenda kwa kusaidia familia zao kutokana na hali ngumu ya maisha.

“Wapo wanaokwenda kutafuta pesa na kwenda kutafuta dawa za kulevya, akeshalewa chochote atakachokifanya ni sawa kwake, ulevi ni baba wa maasi na hapo amani itaanza kuondoka kwa wenzake,”amesema.

Anasema bandari imekua ni kubwa, inawezekana watoto walianza wawili kipindi hiko, sasa inafika darasa zima lakini hatujawahi kuona uvunjifu wa amani bandarini hapa.

Mariyam Suleiman Mustafa mchuuzi samaki katika soko la Machomanne, anasema uvunjifu wa amani unatokea pale watoto wanapoondosha uwamifu katika utengenezaji wa samaki.

“Ingekuwa wazazi wanauelewa juu ya umuhimju wa elimu kwa watoto wao licha ya hali ngumu ya kimaisha iliyopo, basi sizani kama wange waruhusu watoto wao kujiingiza katika biashara yoyote katika umri mdogo kwa kisngizio tu maisha,” alisema.

WAVUVI WA SAMAKI

Juma Khamis Kambi anasema watoto wamekuwa ni wengi na hata wakikatazwa, wazazi wao wanakuwa wakali kutokana na baadhi yao kutumwa kwa ajili ya kusaidia familia zao.

“Ngalawa au madau yanapofika tu, basi utawaona wanakuja na biashara zao wengine huleta madafu au mafenesi, ili tuwapatie samaki na sisi tunafanya hivyo, wengine wanawauza baadae na wengine wanapeleka kwao,”amesema.

Katika hatua nyengine Kombo sheha Hassan amesema watoto waliopo wanakosa fursa zao za kielimu, kutokana na tamaa za wazazi wao kwa kitu kidogo wanachopata nao kuona ndio kazi kwa mtoto wake.

“bandarini hapa watoto wanaojishuhulisha na ajira ni wengi mmo na uvunjifu wa amani unaweza kuja pale unapowakataza watoto kupara samaki, kuosha madau, kubeba ndoo za madagaa au shazi la samaki,”anafafanua.

MADALALI WA SAMAKI BANDARINI

Abdi Khamis Juma anasema hakuna anayefurahishwa na hali iliyopo katika bandari ya Tumbe, ila ukosefu wa mashirikiano baina ya wazazi na madalali ndio sababu inayopelekea wimbi hilo.

“Baadhi ya Madalali wenzetu na Wazazi hawapo tayari katika hili, sisi wengine tunapoweka mikakati basi wengine wanaivunja na kutuona sisi wabaya,”amesema.

Anasema wapo wazazi wanawatuma watoto wao ndio wakawa wakali katika hili na kuwa tayari kupigana ili wasifukuzwe, hebu tizama mpaka jioni mtoto anafika shilingi  8,000 hadi shilingi 20,000 hutegemea na msimu.

 Naye mkuu wa madalali bandarini hapo Mtawa Khamis Haji, anasema watoto waliopo bandarini hakuna hata mmoja anayekwenda skuli, huku wazazi wao wakishindwa kuwafuatilia.

MASHEHA WA SHEHIA ZA TUMBE

Kaimu sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki Ali Omar Ali, anasema ajira hizo zinakuwa chanzo cha uvunjifu wa amani, kutokana na ukosefu wa elimu pamoja na umasikini kwa familia.

“Mtu akikosa elimu anaweza kufanya lolote hata kama linaweza kuvunja amani na anacho kitizama yeye ni maslahi yake binafsi, ndio mfano kama hawa wazazi wahaowaruhusu watoto wao kupara samaki,”anasema.

SHEHA wa shehia ya Tumbe Magharibi Massoud Khamis Kirando, anasema baadhi ya watoto wanaokwenda bandarini inakuwa ni maagizo  kutoka kwa baadhi ya wazazi wao kama sehemu ya kusaidia familia yao.

“Tunapowafukuza sisi huonekana ni maduwi wakubwa kwa wazazi wa Tumbe na vijiji vya jirani, yote ni kutokana na ukosefu wa elimu, ”amesema.

WADAU WA MAENDELEO

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Tumbe(JUMATU) Nassor Suleiman Nassor, anasema ajira zinakuwa chanzo cha uvunjifu wa amani pale usimamizi wa sheria zinapokuwa zinalegalega.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya kupunguza Umaskini na kuboresha hali za wananchi (KUKHAWA) Hafidhi Abdi Saidi, anasema unapomzuwia mtoto asiende kwenye ajira hizo katika umri mdogo,familia haitambuwi wamezuiliwa kwa sababu gani.

“Ukosefu wa elimu kwa watoto, unapelekea kuingia katika vikundi viovu ikiwemo wizi, udhalilishaji na uuzaji ama utumiaji madawa ya kulevya mwishokupelekea familia kugombana,”amesema.

VIONGOZI WA SERIKALI

Diwani wa Wadi ya Tumbe Ali Juma Shaibu, anasema umasikini wa familia ndio chanzo kikuu cha watoto kujiingiza katika ajira za utotoni na wanapokatazwa wazazi wanakua wakali.

“Hakuna siku ambayo watoto wanakua hawapo, siku zote wapo na wala hawaendi skuli, wakikatazwa wazazi wanakuwa wakali na kupelekea uhasama na kuchukiana.

MKUU wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, anasema mtoto anapojiajiri akiwa mdogo anakosa haki zake za msingi ikiwemo elimu.

Amesema kuwa ajira za utotoni zinaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani, kutokana na wazazi wanakuwa wabishani na viongozi wao serikali wanapokatazwa kutokuwaruhusu watoto wao katika ajira.

“Kutokana na wazazi kuwa wabishi juu ya suala la ajira za utotoni ndio maana watoto zaidi ya 7609 wamekatisha masomo na kundi kubwa wapo katika ajira za utotoni,”alisema.

SHERIA YA MTOTO NO:6/2011

Kwa mujibu wa sheria hiyo, imekataza mtoto kuajiriwa kinyume na sheria kumuajiri au kumtumia mtoto katika kazi zenye madhara.

MWISHO

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch