Skip to main content

‘PMTCT’ HUDUMA MWAFAKA YA KUZUIA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA

HUDUMA ya kuzuia maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ‘PMTCT’ ni huduma ambayo inawalenga akinamama wajawazito na wenza wao.

 

Huduma hii ilianzishwa, baada ya kuona kuwa asilimia 90 ya watoto chini ya miaka 15, wanaoishi na virusi vya Ukimwi inatokana na maambukizo kutoka kwa mama zao na asilimia 10 iliyobakia, ndio ambayo inatokana na sababu nyengine kama kusaidiwa damu na kubakwa.

 

Inakadiriwa vifo vya watoto chini ya miaka 15, vinavyotokana na virusi vya Ukimwi katika dunia ni 610,000, ambapo kati ya hivyo vifo 550,000 vimetokea katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania Zanzibar.

 

Maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, ni moja kati ya njia kuu zinazosababisha kuenea kwa kasi ya  maambukizi virusi vya Ukiwmi.

 

Maambukizi hayo hutokea katika nyakati tofauti kama vile, wakati wa ujauzito, wakati wa uchungu na kujifungua, wakati wa kipindi cha kunyonyesha maziwa ya mama.

Akinamama hao hasa wajawazito kwa asilimia 5 hadi 10 wamekuwa wakisababisha watoto wanaowazaa kupata maamimbizi.

Lakini inaonesha kuwa pia, asilimia 10 hadi 20 hutokea wakati wa uchungu na kujifungua jambo ambalo linahitajia uangalizi wa kutosha.

 

Kwa upande mwengine asilimia 20 hutokea wakati wa mama mara baada ya kujifungua anapomnyesha maziwa mtoto wake, ambao inawezekana alizaliwa akiwa hana maambukizi kuyapata

 

Ndio maana wataalamu wanasema ikiwa kutakuwa na   akinamama wajawazito 100, wanaoishi na virusi vya Ukimwi wataachiwa wajifungue na kunyonyesha bila ya kinga, basi asilimia 40 tu, ndio watakaowaambukiza watoto wao virusi hivyo na watoto 60 watabaki wakiwa salama na maambukizo hayo.

 

HUDUMA ZA ‘PMTCT’ NI NINI ?

Ni huduma inayotolewa kwa kila mjamzito kwa kupimwa maambukizi ya virus vya Ukimwi kwa lengo la kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

 

Mam mwenye maambukizi ya VVU anaweza kumuambukiza mtoto akiwa tumboni, wakati wa kujifungua na wakati wa kunyonyesha.

 

Kwa mujibu ripoti ya Idara ya Sera na Ushawishi ya Tanzania bara, inaeleza wastani ni akina mama wajawazito wenye VVU 65 kati ya 100 wanapata huduma ya PMTCT.

 

Hata hivyo namba hiyo ni ndogo katika mikoa ya Tanga, Rukwa, Mwanza, Morogoro, Mara, ambapo watoto hao wanapata matibabu ya kuzuia wasiambukizwe na mama zao.

 

Ni wanne (4)  tu kati ya 10 ikimaanisha kuwa sita (6) kati ya 10 hawapati huduma za aina hiyo.

 

Ingawa ripoti imetaja sababu kadhaa, zinazochangia hali hiyo ikiwa ni pamoja na, upungufu wa wafanya kazi wa afya kwa ajili ya kutoa huduma za PMTCT na zile za matibabu kwa watoto.

 

Ripoti ikaeleza kuwa, leo hii Tanzania kuna akina mama 118,000 wanaoishi na vvu kila mwaka, ambao wanawaambikiza watoto wao karibu 40,000 kila mwaka.

 

 Maambukizi haya ni sawa na watoto 118 wanaoambukizwa kila siku, na kama watoto hawa 40,000 wasipopata matibabu, nusu yao watapoteza maisha kabla ya umri wa miaka miwili.

 

 HUDUMA ZA ‘PMTCT’ ZILIANZISHWA LINI ?

Kwa Zanzibar huduma za kuzuia maambukizi ya virusi ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto zimeanzishwa tokea mwezi wa Aprili 2005.

 

Ambapo kwa ushirikiano baina ya Wizara ya Afya na mashirika ya maendeleo yakiwemo CDC, Columbia University, WHO, Medicos del Mundo, UNICEF walifanikisha hilo.

 


HUDUMA HIZI ZINA MALENGO GANI?

Kama ilivyo kwa huduma nyingine mbali mbali, pia huduma hizi nazo zinamalengo kaadhaa moja wapo ni kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

 

Aambapo njia hii hasa lengo lake ni kupunguza maambukizo kwa watoto wachanga, ili kuona tunapata kizazi ambacho kiko huru na virusi vya Ukimwi

 

Ambapo huduma hii inajumuisha mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na vipengele vya huduma ya PMTCT, ushauri nasaha kuhusu maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwamtoto.

 

Akizungumza na mwandishi wa makala hii, Kaimu Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba Ali Mbarouk Omar, alisema kipengele chengine kinachojumuisha ni kuchunguzwa damu ya virusi vya Ukimwi.

 

Aidha alieleza kuwa, jengine ni kutumia dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi,  kuimarisha boresha huduma za uzazi.

 

“Huduma hizi zinaumuhimu mkubwa maana unaweza kumpa uhakika mama mjamzito anaeishi na Virusi vya Ukimwi, kupata kizazi kilichosalama,’’anasema.

 

Mratibu wa kitengo shirikishi, kifua kikuu, homa ya ini ukomwa na Ukimwi Pemba Khamis Hamad anasema wanasayansi wamefanikiwa kupata dawa za kuwasaidia wagonjwa wa Ukimwi, ili kupungunza makali ya maambukizi (ARVs).

 

Anasema dawa hizi zimechangia kupunguza maambukizo na vifo kwa kiasi fulani, ingawa inakadiriwa watu 14,000 huambukizwa VVU kwa siku.

 

Huku ikielezwa kuwa, zaidi ya asilimia 95 ya maambukizo yanatokea kwenye nchi changa na zile zenye pato la wastani.

 

Na jumla ya maambukizo hayo hutokea kwa vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi miaka 49 wakiwemo wanawake kwa 50.

Anafafanua kuwa asilimia nyingine 50 ni watu walio chini ya umri wa miaka kati ya 15 hadi 24.

 

Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ linaripoti kuwa jumla ya watu 8,500 hufariki dunia kila siku kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.

 

Ambapo WHO linafafanua kuwa, zaidi ya asilimia 90 ya watu walioambukizwa wanaonekana katika nchi zinazoendelea, huku waengi wao hawajijui kama tayari wameambukizwa.

 

Eneo jengine Mraibu wa elimu ya mabadiliko ya tabia katika mradi wa afya kamilifu, kutoka shirika la Amref help Afrika Sunday Beebwa, anasema vyombo vya habari vinamchango mkubwa wa kuhakikisha kunazaliwa watoto wasio na maambikizi.

 

“Tayari tunaomama wajawazito katika familia zetu, namna ya wao kupata watoto wasio na maambukizi tumekuwa tukifanyakazi kwa karibu na vyombo vya habari ili kuelimisha hilo.

 

WAJIBU WA VIONGOZI

Kundi hili limetakiwa kushajiisha na kuelimisha jamii kuhusu huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi, katoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

 

Kaimu Meratibu wa Tume ya Ukiwmi Pemba Ali Mbarouk Omar, anasema ili waelewe huduma hii ipo na umuhimu wake na hivyo waweze kuitumia.

 

Lakini akawataka wanaume na akinababa kuzitumia ipasavyo huduma hizi kwani na wao zinawahusu kwa njia moja ama nyingine.

 

UKIMWI

Ukimwi ni ugonjwa uliogunduliwa kwa mara ya kwanza huko nchini Marekani mwaka katika 1981, huku mgonjwa wa  mwanzo akionekana eneo la Los Angeles nchini humo.

 

Ukimwi ulionekana barani Afrika ya katika mwaka 1982, kuanzia hapo ugonjwa huo ulitapakaa katika nchi za kusini, kaskazini, mashariki na magharibi ya Afrika.

 

Ingawa kusini mwa jangwa la Sahara hali ya Ukimwi ilionekana kuwa mbaya sana ukilinganisha na sehemu nyengine duniani

 

UKIMWI KWA TANZANIA

Wagonjwa wa mwanzo waligunduliwa mkoa wa Kagera katika mwaka 1983, ambapo miaka mitatu baadae, mikoa yote ya Tanzania ilikuwa tayari ina maambukizo ya virusi vya Ukimwi.

 

Lakini kwa upande wa Zanzibar, wagonjwa watatu wa mwanzo wa Ukimwi waligunduliwa katika 1986, eneo la hospitali ya Mnazi Mmoja mjini Unguja.

 

Maambukizo hayo ya Ukimwi yalienea sehemu mbalimbali ya visiwa hivi vya Unguja na Pemba na tokea mwaka 1986 hadi mwaka 2015, idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Ukimwi imefikia 13,000.

 

Lakini asilimia 1 ya wamama wajawazito wameambukizwa na VVU, na asilimia 86 ya maambukizi yako kati ya miaka 20-49, na watoto yatima zaidi ya 1500 wamerekodiwa kuwa wanaishi na maambukizi ya VVU.

 

Maraym Said Abdalla wa Chake chake anaeishi na VVU kwa miaka 17 sasa, tayari ameshajifungua watoto wawili bila ya VVU, baada ya kutumia njia elekezi za wataalamu wa afya.

 

Anasema, alikuwa karibu mno na wataalamu wa afya kila hatua ya kutafuta na kuulea ujazito wake, hadi siku aliyojifungua.

 

‘Ninao watoto wawili ambao niliwapata nikiwa na Virusi vya Ukimwi, lakini hasi sasa wako salama kama alivyo babayao,’’anabainisha.

 

Salim Ali Saleh ambae ni msimamizi wa mradi wa kuelimisha jamii ya watu wanaoishi na VVU juu ya suala la lishe ya binadamu kutoka ZAPHA+ Pemba, anasema mama mjamzito na hasa mwenye VVU hutakiwa karibu na chakula bora.

“Kama mama mjamzito ataacha kutumia chakula bora, mwilini huathiri mfumo mzima wa chakula na kusababisha lishe duni ambayo hudhoofisha na kuhatarisha afya yake,’’anasema.

                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch