Skip to main content

VIONGOZI WA DINI WANANAFASI YA KUNOGESHA AMANI, NA KUEPUSHA MIGOGORO ZANZIBAR IKIWA...

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

OFISI ya Mufti Zanzibar ni moja kati ya Idara zinazomilikiwa na serikali ya Mapinduzi, ambapo miongoni mwa majukumu yake ni kusimamia, kuratibu na kutoa uamuzi ‘fat-wa’ kwa yale mambo husika.

Ofisi hii, katika kufanikisha shughuli zake imekuwa ni wadau wake mbali mbali, iwe ni wa ndani au nje ya Zanzibar, ikiwa tu wadau hao, wana malengo na maazimio yanayofanana.

Kwa mfano, ofisi hii ya Mufti kwa upande wa kisiwani Pemba imekuwa ikifanyakazi karibu mno na taasisi isiyo ya serikali ya ‘Marafi wa Zanzibar’ ‘Friend of Zanzibar’ pamoja na taasisi ya Interfarce.

Taasisi hizi, zimekuwa zikifanya shughuli mbali mbali wanazoshirikiana na Ofisi ya Mufti kwa upande wa Pemba, ili kuhakikisha, jamii ya watu wa Pemba kwa ujumla wao, wanaishi kwa amani na maridhiano.

Friend of Zanzibar, kuanzia tokea mwaka 2010 na Interface kuwanzia mwaka 2015, zimekuwa bega kwa bega na ofisi hii, kwa kuwajengea uwezo wananchi, waelewe maana na amani na maridhiano, faida zake, athari za kuikosa tena sio tu kwa ajili ya uchaguzi mkuu, bali hata kwenye maisha ya kila siku.

Tasisi hizi, zimekuwa zikikutana mara kwa mara na makundi mbali mbali, kama vile ya waandishi wa habari, maimamu, masheikh, waalimu wa madrssa, makundi ya vijana na wanawake wa kiislamu.

Aambapo yote kwa yote, ni kuona jamii inakuwa na tabia ya kuvumilia, kusameheana, kuhurumiana, kupendana, kusaidia na suala la kuishi kwa amani.

Ndio maana, kwa mfano tasisi ya marafiki wa Zanzibar iliendesha mkutano wa umuhimu wa kutunza amani na kuhimiza maridhianuo, ambao ulihusisha makundi ya vijana, wanawake, masheikh na maimamu iliyofanyika baina ya tarehe 5 Disemba hadi 7 mwaka huu mjini Chake chake.

Mkutano huo wa siku moja, ambao uliandaliwa na kufadhiliwa na taasisi ya ‘Marafiki wa Zanzibar’ ulikuwa na lengo la kuwakumbusha viongozi hao, umuhimu wa amani katika maisha ya kila siku.

Ingawa pia uzoefu unakubali kuwa, kila unapomalizika uchaguzi mkuu suala la amani huwa tete, hivyo mkutano huo pia ulilenga kuona amani inakuwa endelevu.

Aliyeufungua mkutano huo, alikuwa Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar anayefanyia kazi zake kisiwani Pemba, sheikh Mahamoud Mussa Wadi, ingawa kabla ya kufanya tukio hilo, Kaimu Katibu wa Mufti Pemba Sheikh Said Ahmad, aliwaeleza washiriki kuwa, mkutano huo ni ile mikutano iliyoanza kabla ya uchaguzi, kufanyika tena karibu na uchaguzi na huo.

Sheikh Said, amasema Ofisi ya Mufti kwa kushirikiana na taasisi ya ‘Friend of Zanzibar’ imekuwa mstari wa mbele, kuona suala la amani inakuwa ndio utamaduni wa wananchi wote, kwa vile faidi yake hutumiwa na wote.

“Suala la amani, utulivu, maridhiano na mshikamano sasa liwe ndio utamaduni wetu, maana hata viongozi wetu wakuu hapa Zanzibar sasa wanafanya kazi pamoja,’alieleza.

Anasema ikiwa kila kiongozi wa dini na kwa nafasi yake atahimiza umoja, mshikamano, maridhiano, kusameheana, kupendana suala la kuchafuka kwa amani Zanzibar litakuwa ndoto.

Katibu wa taasisi ya friend of Zanzibar sheikh Abubakari Kabwogi, ambae nae alisema suala la amani ni tunu muhimu katika nchi yoyote.

Anasema, pamoja na changamoto ndogo ndogo zilizojitokeza kabla na wakati wa uchaguzi, lakini amani iliyopo leo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020,  imechangiwa kwa kiasi kikubwa na viongozi wa dini ya kiislamu.

Anasema kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na viongozi hao kwa kule kuwaelimisha wafuasi wao, ndio maana leo ambapo uchaguzi umeshamalizika kisiwa cha Pemba kinaendelea kuwa amani.

Anawakumbusha masheikha hao kuwa, kila jamii inakuwa na migogoro, akimaanisha ndio sehemu ya maisha ya kila siku na wale ambao wameshafiriki ndio pekee ambao hawana tena migogoro.

Ingawa Katibu huyo anasema uboro wa jamii yenye migogoro kisha ni kukaa chini na kupatana, kama ilivyofanyika kwa sasa ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibra ‘SUK’.

Katibu huyo aliwaambia viongozi hao, wao ndio pekee ambao wako karibu mno na waumini kuliko kiongozi yeyete yule, kwa kule kukutana nao mara tano (5) kwa siku, kwenye nyumba za ibada.

‘Fursa ya kukutana na waumini mara tano kwa siku, itumieni ili kuwaeleza umuhimu wa amani na maridhiano yaliopo Zanzibar, kwani huo ndio utamaduni wa wazanzibari,’’anasema.

Hata hivyo amesifu kazi kubwa inayofanywa na Ofisi ya Mufti, akisema kuwa, kama kunakuwa na vyombo ambavyo wanazionyesha kazi hizo nje ya Pemba, basi kila mmoja engefurahia.

Sheikh Mahamoud Mussa Wadi, wakati akifungua kongamano hilo, aliwakumbusha washiriki kuwa, kongamano hilo ni endelevu ya mikutano inayofanywa na ofisi hiyo, ikishirikiana na taasisi ya marafiki wa Zanzibar.

Aliwataka viongozi hao, sasa kwa vile uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, umeshamalizika, ni wakati wa kushirikiana na serikali iliyopo madarakani, katika kuleta maendeleo ya taifa.

“Viongozi wetu sasa wanafanyakazi pamoja, je sisi viongozi wa dini ya kiislamu tunafanya nini ikiwa hatutoshirikiana nao kupata maendeleo ya kweli,’’alieleza.

Naibu huyo anasema, kila mmoja awe muumini wa dini ya kiislamu au wa dini nyingine anahitaji maendeleo popote alipo, sasa ili kufikia hayo, tuweke pembeni itikadi za vyama vyetu na kushirikiana na Serikali yetu ya Umoja wa Kitaifanya kazi nayo.

Kwenye eneo jingine, aliongeza kuwa ubora wa mwanadamu anaekoseana na mwenzake, hupendeza zaidi kama akiomba radhi, mashama, na anaeombwa kusahamehe ni bora.

Naibu Mufti akazidi kusisitiza kuwa, ni vyema kwa jamii kuacha kufuata matamanio ya shetani ‘ibilisi’ kwani hupenda mno yale mazuri kuyageuza kuwa mabaya, na mabaya kuyafanya kuwa mazuri kwa lengo la kuupoteza umma.

Kaimu Katibu wa Ofisi ya Mufti Pemba Sheikh Said Ahmad Mohamed, kubwa anawataka viongozi wa dini ya kiislamu kuwaeleza wafusi wao juu ya umuhimu wa kuvumiliana, kupendana, kusamehena na kuombana msahama, ili kuhakikisha amani haichafuki tena.

Alikemea tabia ya viongozi wa dini, wakiwemo maimamu na makhatibu kushabikia vyama, kwani kufanya hivyo kunaweza kukawagawa wafuasi wao.

Anasema, sasa kilichopo mbele yao hasa baada ya kuwepo kwa maridhiano ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa ‘SUK’ ni kuhubiri umoja, mshikamano, amani na utulivu.

“Hatuna budi kuungana na viongozi wetu wa nchi, sasa wenyewe wanafanya kazi pamoja, sasa kilichobakia kwa sisi viongozi wa dini, kuhakikisha hatuwi chanzo cha machafuko,’’anafafanua.

 Anasema, wapo wanaovitumia viriri vya msikiti kama majukwaa ya kutoa misimamo yao, au kuonesha mapenzi juu ya chama fulani, jambo linaloweza kusababisha mgawanyiko na kuanza kuchafuka kwa amani na kisha kuzuka migogoro msikitini.

Mapema, sheikh Saleh Abdull Adam wa Mkoani Pemba, aliwasisitiza wenzake, kuacha kuonesha wazi wazi mahaba na mapenzi ya vyama vyao vya siasa kwa jamii, kwani kufanya hivyo, kunaweza kupelekea kuwagawa wafuasi.

“Wakati huu, sisi viongozi wa dini na masheikh lazima tujuwe kuwa wajibu wetu ni kuwaunganisha wananachi, iwe kwa kutumia hutuba au mihadhara,’’anasema.

Lakini hata Khamis Salum Ali wa wilaya ya Chake chake, alisema ijapokuwa sasa mfumo wa vyama vingi unaonekana kuwa ni tatizo, lakini sio haki kwa viongozi wa dini kuwagawa waumini.

“Kwa mfano, mfumo huu wa vyama vingi, leo umepelekea kuwepo kwa maridhiano, umoja, mshikamano sasa je sisi masheikh tuvuruge haya, hili sio sahihi,’’anasema.

Kwa upande wake sheikh Juma Haji Hamad wa wilaya ya Wete, alisema, ili kuhakikisha maradhiano yaliofikiwa Zanzibar yanadumu, ni vyema kuanzisha kamati (kikundi) kwa viongozi na wanataaluma wote, kuanzia ngazi ya shehia.

“Hili lililofikiwa na Kiongozi mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo na rais wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi, linataka kusimamiwa kuanzia kule kwenye shehia hadi taifa,’’alipendekeza.

Sheikh huyo, anasema huu sio wakati wa kufukua makaburi kama anavyosema rais wa Zanzibar, hivyo hivyo na huku kwenye siasa, kama nchi imetulia tushirikiane kuijenga Zanzibar.

Haji Haji Khamis Mbwana, imamu wa msikiti wa Ijumaa Micheweni, alisema sasa wakati umefika kwa kuanzishwa vilabu vya amani na ushirikiano katika kila skuli ya Zanzibar.

Lakini, sheikh huyo akaenda mbali zaidi, akisema kama sasa taifa limeshatulia, sio busara na wajiepushe viongozi wa dini kutumiwa na wanasiasa, kwani inawezekana kutumiwa huko wakatoka nje ya maadili na kusababisha jazba.

Mara baada ya kumaliza kula kiapo hapo Disemba 8, mwaka 2020, cha kuwa Makamu wa Kwanza, Maalim Seif Sharif Hamad, alisema kilichomsukuma kuitaka nafasi hiyo, ni kuiangalia Zanzibar kwanza.

“Zanzibar kwanza kisha chama, hivyo sisi ACT, kwanza tumevutiwa na aina ya uongozi wa rais wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi, pili ni kuendeleza maridhiano ya wazanzibari,’’anasema.

Mara baada ya shughuli hiyo, rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema Zanzibar itajengwa na wazanzibari wenyewe.

“Leo tukiwa ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa, sasa kilichobaki kwa wananchi na kuyaenzi, kuyaendeleza, na kuyaheshimu maridhiano hayo,’’anasema.

Zanzibar kufuatia marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, iliweka kwenye sehemu yake ya pili, kifungu cha 39 kilitaja kuwepo kwa Makamu wawili.

Ambapo kifungu cha 39 (3), kimesema Makamu wa Kwanza atatakiwa awe na sifa ya kuwa Mjumbe wa baraza la Wawakilishi na atateuliwa na rais, baada ya kushauriana na chama anachotoka Makamu huyo.

Ambapo kifungu kidogo cha (5) cha Katiba hiyo, kimesema Makamu huyo wa Kwanza, atakuwa ni Mshauri mkuu wa Rais katika kutekeleza kazi zake.

Aidha kifungu cha (6) kimemtaja kuwa rais pia atamteua Makamu wa Pili wa rais, kutoka miongoni mwa wajumbe wa baraza la wawakilishi, kutoka katika chama anachotoka rais.

Watanzania na Zanzibar kwa ujumla wanatarajia kuingia tena kwenye uchaguzi wa awamu wa saba, wa mfumo wa vyama vingi hapo mwaka 2025.

Huku hayo yakifanyika, hivi karibuni aliyekuwa Afisa Mdhamini wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale Pemba Khatib Juma Mjaja, alisema dhana ya utunzaji wa amani  inawahusu mno waandishi wa habari.

Hayo aliyabainisha kwenye mkutano wa siku moja, ulioandaliwa kwa pamoja baina ya Klabu ya waandishi wa habari Pemba PPC na Shirika la Internews.

Ambapo baadhi ya waandishi walioshiriki kwenye mkutano huo, walisema PPC na Internews wamefikiria jambo jema kuwakumbusha namna ya kuandika habari za maridhiano hasa kipindi hiki Zanzibar ikiwa imezaliwa upaya.

                                 Mwisho

 

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch