Skip to main content

SHERIA MPYA YA ZAECA IWE MKOMBOZI WANAWAKE KUINGIA KWENYE UONGOZI

 



  Na Nihifadhi Issa Zanzibar@@@@

Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imeweka wazi  haki za wanawake za kushiriki katika uongozi, ibara ya 21 inasisitiza kuwa kila raia wa jamhuri ya muungano ana haki sawa za kushiriki katika uongozi wa nchi aidha moja kwa moja au kwa  njia ya uwakilishi.

 Kwa  katiba ya zanzibar sehemu  inaeleza kwamba kila mtu apewe nafasi sawa katika kupata nafasi za uongozi kwenye serikali, aidha kwa njia ya moja kwa moja  ama kupitia wawakilishi wao waliochaguliwa kwa njia ya huru na haki.

Aidha  mpango wa utekelezaji wa beijing katika maelezo ya dhamira namba 7 imeeleza uezeshaji wa mwanamke na ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuangalia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha wanawake na wanaume wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ngazi zote za maamuzi

Licha ya hayo yote ambayo yanayompa nafasi mwanamke kushiriki kikamilifu nafasi ya uongozi lakini kuna changamoto mbalimbali zinazomkwamisha kufikia ndoto hizozakuwa kiongozi ikiwemo suala la rushwa

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MH Samia Suluhu Hassan mnamo june 22 2017 kipindi alipokuwa  makamu wa Rais  wakati akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa Kimataifa wa Ngazi za juuwa mapambano dhidi ya Rushwa uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam alisema “kupambana na rushwa ni jambo la msingi na muhimu kwani ni mbaya nan a imeharibu sana maisha ya watu, maendeleo ya kiuchumi , kisiasa na kijamii hivyo ni lazima ikomeshwe ili jamii iishi iishi maisha mazuri” alisema Mh Samia




Rushwa hutamalaki katika maeneo mbalimbali nchini ndio maana mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar ZAECA kuwekeza elimu ya rushwa kwa jamii hususan wanawake  ili kuwajengea uadilifu Zaidi katika kupambania haki zao.

 Mgeni Salami Suleiman Mkuu wa divisheni ya elimu kwa umma ZAECA Amesema uwepo wa sheria mpya  namba 5 ya mwaka 2023 ni maboresho ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar  kuhakikisha  rushwa na uhujumu uchumi haipati nafasi huku akieleza kuwa imekuja muafaka kwa wanawake kujisimamia na kuwa mabalozi katika kuelimisha wengine ili kuepukana na tatizo hilo

 

Akizungumzia sheria hiyo inavyomlinda mwanamke katika masuala ya  kufikia ndoto za  uongozi  amesema dhamira ya serikali ni kufikia usawa wa kijinsia wa  asilimia 50/50 ikiwa ni kufuata sheria na mikaataba mbalimbali iliyoiridhia ambayo imetoa haki kwa kila mtu kushiriki katika nafasi za uongozi.

Amesema sheria hiyo imekuja kuongeza nguvu na kusawazisha baadhi ya mapungufu ambayo awali yalikuwepo katika sheria   iliyopita kwani inasadikika kuwa  waathiriwa wakubwa wa rushwa iwe ya pesa, ngono au yoyoye ile ni wanawake na wengi hushindwa kukabiliana nayo na hupelekea athari mbalimbali katika maisha yao ikiwemo kutojiingiza tena kwenye kinyanganyiro cha kugombea nafasi za uongozi

“katika sheria hii mpya kuna kipengele cha usiri wa taarifa mfano mwanamke amekwaza katika kufikia ndoto zake kwa namna yoyote sheria ipo  rafiki yeye kupeleka taarifa zake na haitakiwi kutoka,

 

“kifungu cha 15  cha   sheria hii kinamtaka mfanyakazi wa zaeca wawe na usiri na pindi ikithibitika mahakamani mfanyakazi wa zaeca ametoa risi  anachukuliwa hatua ya kifungo miaka mitatu hivyo wanawake pamoja na makundi mengine wawe huru kuleta taarifa”alisema Mgeni

Katika sheria hiyo namba 5 ya mwaka 2023 kifungu cha 52 (1) kinaeleza mtu ambaye kwa namna yoyote atashawishi, atakubali na ataahidiau ataahidi mkufanya ngono au atamfanya mtu mwengine akubali au aahidi kufanya ngono kwa ajili ya kupata huduma au kutotoa huduma ametenda kosa

Aidha (2) ya kifungu hicho kinaeleza endapo ngono imefanyika kwa ajili ya mnufaika wa ngono hiyo afanye jambo amabnli lipo kinyume na sheria, adhabu yake ni kifungo kwa kipindi kisichopungua miaka saba lakini kisichozidi miaka kumi pamoja na faini isipongua shilingi milioni kumi na tano za kitanzania lakini isiyozidi milioni ishirini za kitanzania.

“Kwa vile wahanga wakuu ni wanawake kupitia     adhabu  hizi basi iwe rahisi mwanamke  akitokezewa na tatizo hilo afike zaeca hatua ichukuliwe ikitokea kila mfanya makosa hayo akafungwa miaka 7 tunaimanai vitendo hivyo vitapungua au kumaliza kabisa”alimalizia mgeni

 

 

 Makala hii imezungumza na mwanamke ambaye ameomba hifadhi ya jina lake anasema suala la rushwa lipo lakini waliowengi hawalizungumzi kwani wanahisi ni kujitia aibu   na kujidhalilisha mwenyewe hivyo wengine huamua kukaa kando.

‘’sitosahau kamwe suala la Rushwa limenifanya hadi leo hamu ya kuwa kiongozi kunitoka nimegombania karibia miongo miwili sikupata nafasi hiyo haikunikatisha tamaa nilijua ndio masuala ya ushindani,

“lakini nakumbuka tulienda mahali fulani katika masuala ya chama na kukawa na uchaguzi nami ni mmoja ya wagombania nafasi zile cha ajabu nikiwa nimelala alikuja kiongozi wa chama akanitaka niuvue utu wangu eti nitapata hiyo nafasi nilichang’anikiwa nikaanza kupiga kelele akatoka tangu siku hiyo nikaamua tu kubaki mwanachama wa kawaida” alisema

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar Dkt. Mzuri Issa Amesema wanawake na wasichana wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kufikia ndoto zao za kimaendeleo ikiwemo rushwa ya ngono na hawana pahali maalum wanapoweza kukimbilia.



“Elimu bado inahitajika na kazi ya kudhibiti vitendo vya rushwa sio ya ZAECA pekee bali inahitaji ushiriki wa kila taasisi hasa ukizingatia kuwa kinga ni bora kuliko tiba”alisema mzuri

Aidha Dkt. Mzuri anasema ”kuanzishwa kwa sheria mpya ya ZAECA kutafungua ukurasa mpya katika mapambano ya rushwa hasa ya ngono katika nafasi za kazi za kitaifa na za kisiasa na hasa kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025’’alifafanua

Mwanasiasa Halima Ibrahim anasema    ikiwa sheria hiyo mpya itafanyiwa kazi kwa uadilifu itatoa mwanya kwa wanawake kuhamasika kuingia kwenye uongozi “ kwani wataona sasa tumepata mtetezi zile kero tutasilisha sehemu husika na hivyoule usawa wa kijinsia tunaoulilia tutapata mwarubaini wake,

“binafsi napongeza sana juhudi hizi na natoa wito kwa wanawake wenzangu tusivumulie haya masuala ya rushwa ndio yanakwamisha juhudi zetu pengine mtu sifa zote unazo za kuwa kiongozi lakini unakatishwa tamaa kwa kitu kidogo tu tufike sehemu husika tusizembee uongozi ni haki yetu tupinaie tuufikie usawa wa 50/50”alisema Halima.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch