Skip to main content

HIVI NDIVYO TAMWA -ZANZIBAR ILIVYOFANIKIWA KUWAJENGA WAANDISHI VIJANA, MASUALA YA WANAWAKE NA UONGOZI

 

Na Nihifadhi Abdulla, UNGUJA.

Jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa siku hadi siku kuhakikisha usawa wa kijinsia unachukua nafasi yake kwa kupitia mikataba ya kimataifa, kikanda, sera, sheria, matamko na mbinu nyengine tofauti

Mpango wa utekelezaji wa beijing katika maelezo ya dhamira namba 7 imeeleza  uezeshaji wa mwanamke na ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuangalia uwiano wa jinsia ili kuhakikisha wanawake na wanaume wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ngazi zote za maamuzi


Aidha Mkataba wa kikanda wa nchi za kusini mwa afrika kifungu cha 12 kinasisitiza ushiriki sawa wa wanawake kufikia asilimia 50/50 kwenye nyanja za maamuzi, pia kifungu namba 13 kinaeleza kuwekwa mikakati madhubuti ya kuwawezesha wanawake kushiriki katika mchakato mzima wa uchaguzi na upigaji kura na kuondosha mila na desturi potofu zinazopingana na maendeleo ya mwanamke katika siasa na uongozi


Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Zanzibar ni taasisi inayotetea mambo mengi ya haki ikiwemo za wanawake katika kuhakikisha kunakuwepo na fursa sawa na kufikia lengo la uongozi wa 50 kwa 50. 


Waswahili husema “kidole limoja hakivunji chawa” katika mipango ya TAMWA ya kuwawezesha wanawake kuingia katika uongozi imeamua kushirikiana na waandishi wa habari Vijana visiwani zanzibar ili kuunga nguvu ya pamoja kuhakikisha lengo linafikiwa.



Mkurugenzi wa chama hicho dkt. Mzuri issa anasema TAMWA wameamua kushirikiana na waandishi hao kwani wananchi wanaviamini vyombo vya habari na vinawafikia waliowengi wa wakati mmoja


Alieleza kuwa kwa kuhakikisha waandishi vijana wanafanya kazi ya kuelimisha jamii kuhusu usawa wa kijinsia kwa uweledi waliwajenga kwa kuwapa mbinu zitakazowasaidia kuandika na kutangaza yatayoibua upatikanaji wa haki hiyo




“waandishi wa habari wanauwanja mpana na wanayajua mengi hivyo tumeamua kushirikiana nao kwa kuwapatia kwanza mafunzo namna bora ya kuandika na kuhamamsisha masuala ya wanawake katika uongozi, “wananchi waliowengi wanaamini vyombo vya habari na wanajifunza pia kipi kimejiri kwa mfano kila sehemu iwe radio, tv, mitandanao ya kijamii na magazeti wakisikia masuala ya 50 kwa 50 wanawake na uongozi tunaimani wanahamisika zaidi” alifafanua dkt. Mzuri

Afisa mradi wa kuwawezesha waandishi wa habari vijana kuandika habari za wanawake na uongozi kutoka TAMWA zanzibar (YMF) Tatu Ali Mtumwa amesema waandishi wa habari Vijana wamekuwa chachu ya maendeleo kwa kuhamasisha usawa wa kijinsia ili kufikia 50/50 kwa wanawake na wanaume katika ngazi za maamuzi.

“tumeamua kulenga zaidi kwa vijana kazi hii inataka moyo ya kupambana na kujitoa ili wawe waandishi bora na wa mfano kuanza sasa na majukumu yao yote ya kila siku kuwa wahamasishaji wa masuala haya ya wanawake na uongozi na mengineyo yenye lengo kutetea haki na kuleta maendeleo”alisema Tatu


Aliendelea kusema kuwa tamwa imewajenga waandishi hao kuandika kazi zao kwa kuzinagtia mikataba Na wawe wajuzi wa kutumia tamwiku ili iwe rahisi kulinganisha hali iliyopo na inayotarajiwa “sio kama mwanzo hawaandiki lakini tumeona haja ya kuwapatia ujuzi zaidi wa kutumia matumizi sahihi takwimu kutumia, mikataba na matamko mbalimbali kwani hiyo ni kielelezo tosha kwamba mwandishi anaandika kitu ambacho anauhakika nacho”alifafanua.

Berema Suleiman ni miongoni mwa waandishi wa habari vijana anasema awali alikua akifanya kazi zake kikawaida bila ya kutumia tawimu “baada ya kupata elimu kutoka TAMWA mwanzo iliniwia vigumu lakini sasa naona utofauti kwani kazi ambayo inavielelezo huwa na mvuto haichoshi kusoma wala kusikiliza

‘‘Hii imenifanya kujua mambo mengi mfano suala la masheha kumbe ni asilimia ndogo sana ya wanawake mwanzo niliona ni kitu cha kawaida tu sasa nikiaandaa kazi zangu sipati shida kuwasilisha kwa jamii kwani huwa imeshiba takwimu na pia natumia mikataba au sheria kuithibitishia jamii kwamba kitu ninachowasilisha kipo sahihi kisheria’’alieleza Berema

Mbali na hayo TAMWA Zanzibar imeamua kuchukua juhudi mahususi za kuandaa tuzo ili jamii itambue mchango wa wanawake na uongozi katika sekta mbalimbali ili kuinua hali za wanawake na kuongeza ushiriki wao katika masuala ya uongozi katika ngazi zote za maamuzi kama ilivyoelezwa katika katiba ya nchi, mikataba, na itifaki mbalimbali za kimataifa.

Kwa muda wa miaka mitatu mfululizo sasa hutolewa tuzo hizo za umahiri wa uandishi wa habari za wanawake na uongozi zinazoangazia maeneo mbalimbali ya kupigania haki ya wanawake na mabadiliko ya kufikia 50/50

Kwa mwaka huu tuzo hizo zilitolewa machi 9, 2024 katika ukumbi wa SHAA uliopo mkoa wa mjini magharib ambapo jumla ya kazi 529 ziliwasilishwa kutoka vyombo vya habari mbalimbali vya Zanzibar ikiwa na dhamira ya endelevu inayoakisi waandishi wa habari kuongeza sauti za wanawake na kuchangia katika maendeleo yao.

Katika mkutano mkuu wa wanachama wa TAMWA Zanzibar uliofanyika April 4, mwaka huu huko Tunguu Dkt. Mzuri alisema juhudi za TAMWA za kuwajengea uwezo waandishi wa habari vijana zimezaa matunda.

“vijana wetu wa YMF wengi wamewasilisha kazi za kushindanisha na asilimia kubwa walioshinda katika vipengele vile ni wao hii inaonesha dhahiri kuwa tayari wameanza kubobea kwani ushindani ulikuwa mkubwa na wengine ni marra yao ya kwanza kushindanisha kazi zao

“Hatujakosea kuekeza nguvu kwao kwani tayari matunda yameonekana huu usiwe mwanzo kwao bali waendeleze juhudi hizo kama sehemu ya masiha yao katika kuwatetea wanawake kupata haki yao ya uongozi na kufikia usawa wa kijinsia” alieleza Dkt. Mzuri.

Hassan Mselem kutoka Pemba amesema akiwa mwandishi wa habari kijana TAMWA imemjenga kujiamini katika kazi zake kwa kumuelekeza namna bora ya kuandaa vipindi kwani mwanzo hakuwa mtumiaji wa takwimu huku akieleza kuwa taasisi zinazotetea ghaki za wanawake zinapaswa kuiga juhudi za TAMWA.

“binafsi naipongeza TAMWA kuwa miongoni mwa wanufaika wa mradi hii imenisadia kufanya kazi zangu kwa uweledi tofauti na mwanzo na ikanipelekea kupata ushindi katika tunzo za uandishi wa habari mahiri za takwimu kuhusu masuala ya wanawake na uongozi yalioandaliwa na wenyewe TAMWA

“juhudi hizi zinapaswa kuigwa na taasisi nyengine katika kuhakikisha lengo hasa la usawa wa kijinsia linafikiwa kwa bila ya kuibua na kuonesha uwezo wa mwanamke katika kuongoza hatutofika tunapopataka” alimalizia Hassan

Zuhura Juma Said ambae ni mwandishi kijana alieibuka mshindi katika tuzo hizo kupitia mtandao wa kijamii amesema kabla ya mafunzo hakuwa na uelewa mpana wa masuala ya wanawake na uongozi na mara nyingi alikua akiandika habari kuhusu changamoto zinazowakwamisha wanawake kufikia ndoto za uongozi.

“kiukweli awali nilikua naandika vinavyokwamisha wanawake kuwa viongozi lakini sasa naandika hata kazi wanazozifanya ambazo zinaonesha utendaji na uwajibikaji wao hivyo jamii inaona uwezo wa mwanamke katika uongozi, “naishukuru TAMWA kwa kunipika bila wao nahisi nisingefika hapa wamenipa fursa ambayo nimeona manufaa yake naomba huu usiwe mwanzo iwe ni endelevu kwa wengine ili nao wapate kuandika habari ama makala zenye ubora” alimalizia zuhra

Mradi uliotekelezwa na TAMWA Zanzibar kwa kushirikiana na shirika la National Endowment for Democracy (NED) wa kuwawezesha waandishi wa habari vijana YMF kuandika habari za wanawake na uongozi umewashirikisha waandishi vijana ishirini na nne (24) kutoka Unguja na Pemba.

mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch