Skip to main content

RC: SALAMA: KIONGOZI WA MFANO, AWAONESHA WENGI KUFIKIA NDOTO ZAO

 



NA AMINA AHMED, PEMBA @@@@


UNAPOZUNGUMZIA nafasi ya mkuu wa  mkoa mwanamke kwa Pemba, kamwe huwezi kuliacha jina la Salama Mbarouk Khatibu.

 

Salama hakumbukwi tu kwa nafasi hiyo, kwa wale wanaofuatilia historia yake, kwanza alianzia nafasi ya kuhudumu ukuu wa wilaya za Chake chake na Micheweni kwa nyakati tofauti.

 

Wapo wanaokumbuka ngarambe zake na jitihada zake za uongozi, wakati ule wa awamu wa saba, alipokuwa mkuu wa wilaya ya Chake chake kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Micheweni.


Kiongozi huyu mwanamke anachukuwa mfano wa mwanamke Hajar na Ibrahim, ambae nae bila ya kujali changamoto na maneno ya kukatishwa tamaa, aliutumika umma.

Hajar, ambae alikuwa mwanamke jasiri, mwenye nia nzuri, aliyeihama nchi yake, ili aende akaishi kando ya nyumba ya Mungu katika ardhi, kame isiyo na maji wala manyasi ili amwabudu Muumba.

HUYU HAPA MKUU WA MKOA KASKAZINI PEMBA
Salama Mbaroku Khatib, nae ni kama mfano huo, ndivyopale anapoamuwa kutekeleza majukumu yake ya uongozi ndani ya mkoa wa Kaskazini Pemba kwa vile hajali muda, juwa wala mvua.

 

Kwake salama anasema, anachotamani jua linapozama ni kukamilisha majukumu yake, na hasa ya kuwahudumia wananchi kama dhamira baada ya kula kiapo kushika nafasi hiyo.

Akizungumza na mwandishi wa Makala hii, anasema ndoto zake ni kuona Mkoa huo wananchi wake wanaishi bila ya shida za dhahiri, mfano huduma za kijamii.

 

‘’Mimi nimekula kiapo kuhakikisha wannachi wa wilaya za Micheweni na Wete wanaishi kwa utulivu na huduma za kijamii za lazima ninawafuata wao,’’anasema Salama.

 

Salama Mbarouk Khatib ni mwanamke pekee aliteuliwa kuongoza mkoa wa kaskazini  kwa mara ya kwa za kati ya wakuu wa mikoa 14 waliopita kabla yake.

Ndio pekee ambae rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliyekambidhi kijiti cha uongozi kwa nafasi hiy, kati  ya wakuu wa mikoa watano waliopo Unguja na Pemba.

 

Anasema alichokifanya Dk. Mwinyi ni utekelezaji kwa vitendo vile vifungu vya kila mmoja ana haki sawa na mwenzake, vilivyomo kwenye Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania yam waka 1977 na ile ya Zanzibar yam waka 1984.

 

Ambapo katiba hizo, kama ukizichungulia kwa kina, zimeweka haki sawa kati ya mwanamke na mwanamme, (50 kwa 50) iwe kwenye uongozi au haki nyingine za kikatiba.


"Kwanza nimshukuru sana Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kuniamini na kunikabidhi wananchi wa mkoa wa kaskazini Pemba, 272, 091, wakiwa wanaume 131, 484 na wanawake 140, 607 (sensa 2022),’’anasema Salama.

 

Kwake nafasi hiyo, anaona umempandisha ndege ya kufungua ukurasa mwengine katika kitabu chake cha historia, ambapo anaona kila anapokutana na changamoto, huzigeuza kuwa fursa.

 

Kumbe RC Salama ni mkuu wa mkoa wa 15 kwa mujibu wa uteuzi, ingawa kati ya hao, wote walikuwa ni wanaume, jambo ambalo linaonesha mabadiliko na wanawake kupanda chati.

 

WAPI ALIANZIA SALAMA?
Kwake anasema, hakuwa mjuzi wala mtaalamu wa kuongoza nafasi yoyote, lakini alichofundishwa wakati wa kusimamia majukumu yake, ni kujiamini.

‘’Siri kubwa niwaambie wanawake wenzangu kikubwa ni kujiamini na tunapopata nafasi inatubidi tuitendee haki ipasavyo, ndivyo wanavyofanya hata hao wanaume”, anasema.

Baada ya kutoka wizara ya wanawake na watoto, na kupata uteuzi wake wa kwanza kuwa mkuu wa wilaya ya Chake chake, anasema aliiingia na hofu ya kawaida kama mwanadamu, ingawa alipaya ushirikiano wa kutosha.

 

Anasema, kama mgagaa na upwa hali ugali mkavu, basi yeye alikuwa akigagaa na watumishi wenzake na kusikiliza ushauri, na kufanya uamuzi wa pamoja wakati huo.

 
Mashaallah, Allah amjaalie mafanikio mema,  wepesi na utayari  wake katika utendaji kazi kabla ya kuteuliwa kuongoza nafasi hiyo kumechangia kufika hapa alipo sasa.

 Anasema ingawa alianza kupikwa na kupikika, wakati akiwa  Ofisa Mipango, wizara ya wanawake na watoto Pemba, hivyo hata alipoteuliw akushika nafasi hiyo, ilikuwa rahisi kiasi.

" Nilikuwa najiamini na naitendea haki kazi niliopewa sekta niliyopangiwa sikuwa na hofu wala woga, pakutolewa uamuzi kama kiongozi nilikuwa natoa, pakushauri nilikuwa nashauri pia,’’anakumbuka.

 


 Anasema miongozo, sera na sheria ndio zinazomlinda kila mtumishi, ingawa suala la kujiamini na kuacha hofu katika kazi ndio mwarubaini kwake, unaopmpa uhakika wa kuwatumikia wananchi.


Jukumu la uongozi alilonalo huku akiwa ni mke, lakini pia mama wa familia, haliathiri utendaji wake kazi, hivyo ni kusema maisha ya uongozi hayaathiri  familia yake bali yanaongeza
heshima na  mashirikiano.

Anasema kila kitu ni kujipanga na kukipangilia, lakini mimi kwa nafasi zote nilizowahikushika hadi hii ya Mkuu wa Mkoa, sioni dhiki na kuihudumia familia yake.

 

Kwake haamini kuwa, mwanamke akipewa nafasi inaweza kumshinda kwa sababu ya familia, bali anachokiona ni ikiwa atakosa kujipanga na kujipangilia inaweza kuwa changamoto.

" Mimi ni mama ambae nina mume na nina watoto, serikali inanitegemea lakini niseme kwamba kikubwa ni kujifahamu tu , kuwa wewe ni kiongozi na nyumbani wewe ni mama ambae unastahiki kufanya majukumu yako,’’anasema RC Salama.

 
Anaeleza kuwa wananchi wameamka sasa hivi hawaangalii jinsia wanaangalia utendaji kazi aliwaasa wanawake wenzake kutuogopa fursa wasizichezee wafanyekazi kadri ya uwezo wao na suala hilo linaweza kuwapa fursa kusonga mbele.

 

Anasema licha ya watu wachache kumtia midomoni, katika utowaji wa maamuzi ya kiutendaji, katika uongozi wake  hakulipokea suala hilo kama ni kikwazo kwa upande wake.

" Kuna baadhi ya watu wanaotaka wakuendeshe vile wanavyotaka wao kwa maslahi yao binafsi, jambo ambalo kwangu silipi kipaumbele naamua kwa kufuata sheria,’’anafafanua.

Kwake anaona ukifanyakazi kwa dhati, hasa ndio changamoto na kasoro zinapoonekana na ukikosa kasoro wewe sio binaadamu au ukizikataa.

 

 kwahiyo nakubali kushauriwa  lakini zaidi na  angalia ule ushauri ninaopewa je hautokweda kinyume na sheria za serikali,  jee
una maslahi ya taifa, hautoathiri serikali ndipo naufanyia kazi kikubwa ninachoangalia ni hicho", alisema.

 


ANAOFANYA NAO KAZI RC SALAMA
Mgeni Khatib Yahya mkuu wa wilaya ya Micheweni, anasema kuwa  kiongozi huyo ndie ambae alikuwa anajifunza mambo mengi kutoka kwakwe.

Anasema alipokuwa Mkuu wa wilaya ya Wete kabla ya kuhamishiwa Micheweni, alivuna mambo mengina na mazuri na hasa suala la kujiamini.



Kwake alikuwa ndio kioo, katika kufanikisha majukumu yake ya kila siku, na hatomsahau tena maana, alimfundishi wa vitendo aina ya uongozi na kuongoza.

 "Najifunza siku hadi siku mambo mazuri  kutoka kwa mkuu wa Mkoa Salama Mbarouk Khatib, ananishauri ananipa maelekezo  kama msaidizi wake na natekeleza majukumu yangu vyema kwa kufuata nyao zake zaidi za uthubutu,’’anasema.

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakar, wanaotaka kuona kuwa mwanamke anaweza kuongoza katika mazingira yoyote, wafike mkoa wa kaskazini Pemba.

 

Kwake mkuu huyo wa Mkoa anamuona mtu wa tofauti, ambae ana nia thabiti ya kweli katika kuitumikia nafasi hiyo na wananchi, bila ya kujali mvua, usiku wala jua kali.

 

‘’Sisi wakati mwengine tunafikiria kwa mvua inavyonyesha jambo fulani, mkuu wa mkoa atalighairisha, lakini mara unamuona huyo amefika sehemu,’’anasifia mkuu wa wilaya Wete.

  

 WANANCHI
Aziza Makame Abass Mkaazi wa  Limbani wilaya ya Wete, anasema kuwa jitihada  inazofanywa na mku huyo wa mkoa, katika kuleta maendeleo, zinaonekana.

Anasema maeneo mengi aliyarithi yakiwa na changamoto za ukosefu wa huduma za kijamii kwa uhakika, ingawa kwa sasa kila eneo hali inridhisha.

 

"Kwanza binafsi nampenda anavyofanya kazi nikisikiliza radio jamii nisipomsikia jioni basi asubuhi nitamsikia anazungumzia  jambo lolote  tunajuwa hasa wa kama tuna kiongozi sio wengine ambapo hata kuwasikia, ni shida,’’anasema.

Nassra Salum Mohamed ambae ni diwani wadi wa Kiuyu, anasema Mkuu wa mkoa wao, ni anakipaji cha uongozi, kuzungumza na hata kuamua jambo, na ni vyema wanawake wengine wakajifunza kwakwe.

 

‘’Hata sisi madiwani tukisikia tuna kikao na mkuu wa mkoa, inabidi kama unachangamoto unataka kuisilishwa kwa, uifanyia uchambuzi wa kina, vyenginevyo itakurudia mwenyewe,’’anasema.


Salim Ali wa Wete, anasema anazipongeza juhudi za kupata viogozi wanawake zilizochukuliwa na mashirika na asasi mbali mbali, zilizopigania nafasi ya uongozi kwa mwanamke.

 

‘’Nasikia kuna chama Chama Cha waandishi wa Habari  wanawake Tanzania ‘TAMWA’ Zanzibar na wengine wamekuwa wakiwawezesha wanawake, nawaambia kwa mkoa wa kaskazini Pemba wamefanikiwa,’’anasema.

WANAHARAKATI

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hya Mussa Said, anasema wanaijivunia mno, uongozi wa Mkuu huyo wa Mkoa hasa kwa vile alikuwa kwenye kapu la wanaharakati.

 


‘’Salama alikuwa anashikia bango kuwa, wanawake wanapopata nafasi za uongozi wasizibeze, na bahati nzuri imemuangukia yeye, sasa tunaona macheche yake kwenye uongozi,’’anasema.

 

Aisha Himid Vuia, anasema alichokifanya Dk. Mwinyi cha kuwapa nafasi nyingi wanawake, ni matokeo ya kelele za wanaharakati, ambapo hakuna mwanamke kiongozi aliyezubaa.

 

Khalfa Amour Mohamed, anasema wamekuwa wakishirikiana na Mkuu huyo wa mkoa katika shughuli kadhaa na hajawahi kukataa, maana anapenda kushirikiana na makundi ya kijamii. 

HALI HALISI YA WANAWAKE NA UONGOZI
Zanzibar kwa sasa  kasi ya wanawake kuingia katika uongozi imeongezeka ukilinganisha  na miaka iliyopita ambapo TAMWA viongozi wanawake katika Baraza la wawakilishi ni asilimia  36 ambayo ni sawa na wanawake 28  kati ya wawakilishi 84 waliopata  nafasi hiyo.


Ni wanawake 22 pekee ambao ni viongozi wakuu  kati ya nchi   na mataifa ya  nchi 123 kwa idadi hiyo bado jitihada zinahitajika katika kuona mwanamke anapata fursa sawa katika vyombo vya maamuzi.

 

Mkuu huyo wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarok Khatib, aliteuliwa kushika nafasi hiyo Disemba 1, mwaka 2020 na kula kipambo Disemba 3, mwaka huo huo pamoja na wakuu wa mikoa wenzake.
                                    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch