Skip to main content

MAJUKUMU YA NYUMBANI CHANZO CHA MWANAMKE KUTOGOMBEA UONGOZI

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WADAU mbali mbali kisiwani Pemba wameitaka jamii kuacha kuwatupia majukumu mengi wanawake ambayo yanasababisha kushindwa kuingia kwenye hatakati za kugombea nafasi za uongozi.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti wadau hao walisema kuwa, si vyema kumuachia manamke majukumu ya nyumbani pekee na badala yake wasaidiwe, ili na wao wapate nafasi ya kuingia katika masuala ya uongozi.

Walisema kuwa, mzigo mzito wa nyumbani wanaoachiwa akina mama umekuwa sababu kubwa ya kuwakwaza na kushindwa kushiriki katika shughuli za jamii, uchumi, siasa na maendeleo, hivyo kuna haja kwa akinababa kushirikiana nao kuleketeza majukumu hayo Pamoja ili na wao wapate uhuru wa kuingia kwenye uongozi.

“Hata katika dini yetu ya Kiislamu mwanamke hatakiwi kuachiwa pekee mzigo mzito wa nyumbani, hivyo ni vyema tukawasaidia ili wapate kufanya shughuli nyengine za kujiletea maendeleo yao, familia na taifa,” walisema wadau hao.

Mdau Saumu Ali Abeid, mkaazi wa Fuoni Unguja alisema, uzito wa kazi za nyumbani unaomzunguka mwanamke ni pamoja na kupika, kushughulikia usafi wa nyumba, malezi ya watoto, kumhudumia mume na wakati mwengine wazee wa mume na wa kwake mwenyewe. 

‘’Katika hali kama hii sio rahisi kwa mwanamke kujiingiza katika harakati za kugombea uongozi kwa sababu mwanamke anayezongwa na kazi nyingi za nyumbani hushindwa kushiriki kwenye vikundi na kutoa mawazo yake ambayo yangempa ujasiri, maarifa na kujiamini kuwa anaweza kuongoza wenzake au jamii,” alifahamisha. 

Mwananchi ambae hakutaka jina lake litajwe wa shehia ya Kipangani Wete alisema, mzigo wa kazi za nyumbani aliokuwa nao mwanamke umepelekea kuwepo wanawake wachache katika vyombo vya maamuzi. 

Hii ndio moja ya sababu ya kushindwa kutatuliwa changamoto kadhaa zinazotukabili, kwani panakuwa hakuna mtetezi wa hali ya wanawake katika vyombo vya maamuzi,” alieleza.

Kwa upande wake Salama Mohamed wa Ole Pemba, alieleza kuwa mara nyingi mrundiko wa kazi za nyumbani unawazuia wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi.

Mkurugenzi wa mradi wa kutoka PEGAO Pemba Hafidh Abdi Said alifafanua kuwa, kazi nyingi za nyumbani zinasababisha wanawake wengi kutoshiriki katika uongozi na kusema kwamba iwapo kama jamii itaendelea kuwaachia mzigo mzito akinamama basi hata maendeleo ya nyumbani yatachelewa kupatikana.

‘’Tokea mwanamke anapoamka ni kazi mpaka jioni huwa hana hata muda wa kupumzika au kufanya mambo mengine nje ya kuta ya nyumba yake’’, aliongeza.

Katibu Kanda ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Pemba, Habib Ali Khamis alieleza kuwa, wanawake wanakosa msaidizi, hivyo hata anapokwenda kwenye vikao anachelewa na hatimae kukosa ajenda zilizozungumzwa na huishia kuwa msikilizaji tu.

Nae mwalimu Saleh Nassor Juma ambae ni Katibu wa ACT Wazalendo Mkoa wa Chake Chake kichama, alieleza kuwa, elimu inahitajika zaidi ili akinamama wagombee na kazi za nyumbani isiwe kikwazo kwao kuwa viongozi.

Wakati wanaharakati wanaendelea kupigania haki za wanawake ikiwemo kushiriki katika uongozi, bado baadhi ya wanawake wanakabiliwa na changamoto zinazosababisha kutokuingia katika harakati za uongozi, hivyo ipo haja ya kutatuliwa kwa ajili ya kumrahisishia shughuli zake.

                                                 MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch