Skip to main content

FCS: YAVUTIWA NA PACSO UTEKELEZAJI MRADI 'URAIA WETU'

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

TAASISI ya The Foundation for Civil Society ya Tanzania bara 'FCS' imesema inaendelea kuridhishwa na utendaji kazi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’, katika utekelezaji wa mradi ‘uraia wetu’ hasa kwa kule kuwanganisha wadau husika.

Hayo yameelezwa na mwakilishi wa taasisi hiyo Neil Ngala, wakati akitoa salamu zake, kwenye mkutano wa siku moja, wa kuibua changamoto za kisheria na sera, zinazokwaza wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, uliofanyika Gombani Chake chake.

Alisema PACSO, imekuwa ikiendelea vyema na utekelezaji wa mradi huo, jambo ambalo limeanza kutoa taswira ya mafanikio yaliyotarajiwa, ikiwa ni pamoja na kuibua changamoto za kisheria na sera.

Alieleza kuwa, mradi huo ambo unatekelezwa na taasisi za PACSO, CYD na JUWAUZA kama hatua ya kitaifa, PACSO imekuwa ikifanya vyema kwa kule kuwakutanisha wadau hisika.

‘’Sisi FCS, tumekuwa tukijivunia mno kila tunapofanyakazi na ‘PACSO’ maana kile ambacho wanakifanya, matunda yake yanaonekana mapema hata kabla ya mradi kumalizika,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mwakilishi huyo alisema, lazima asasi za kiraia zifanyekazi kwa karibu na jamii, ikiwa ni njia mwafaka ya kufikia yale walioyaazimia kuyafanya.  


Kwa upande wake, Afisa kutoka Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ kupitia mradi wa ‘uraia wetu’ Suleiman Baitan, alisema moja ya jambo la muhimu, katika utekelezaji wa miradi, ni kuwa na kundi husika, wakati wa utekelezaji.

‘’Ili asasi ya kiraia ifikie ndoto zake, isisahau kuelekeza kundi husika ‘target group’ wakati wa utekelezaji wa mradi wowote, kama inavyoonesha kwenye andiko, hii ni njia rahisi wakati wa kufanya tathmini,’’alieleza.


Katika hatua nyingine mwakilishi huyo wa JUWAUZA, alisema wamekuwa wakifanyakazi kwa karibu mno na ‘PACSO’ katika mradi huo, na hasa baada ya kuibuliwa changamoto za kisheria.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mratibu wa miradi kutoka Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema mkutano huo ni muendelezo wa vikao mbali mbali, wanavyovifanya na wadau wao.

‘’Kikao kama hichi, kilishawahi kufanyika, na kuibuliwa changamoto za kisheria zinazowakwaza wanawake kutogombea, watu wenye ulemavu kutopata haki zao mahakamani,’’alifafanua.



Akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa ‘PACSO’ Nassor Salim Majid, aliwataka washiriki wa mkutano huo, kuzungumza kwa uwazi, ili malengo ya kikao hicho yafikiwe.

Alieleza kuwa, ndani ya jamii zipo changamoto za kisheria kadhaa ikiwemo masuala ya udhalilishaji, matunzo ya watoto, migogoro ya ardhi ambapo yote hayo yanaikwaza jamii.




Nae Mwakilishi wa Jukwaa la Katiba Tanzania ‘JUKATA’ Thobias Messange, alisema mbinu za kufanya ushawishi moja wapo ni kufanya utafiti, kujua kasoro za kisheria, kanuni na kisera kabla ya kuanzisha jukwaa la ushawishi.

‘’Mwanaharakati anaetaka kufanya ushawishi, sio vyema kukurupuka, lazima ajue kwa upana, anachotaka kukifanyia utetezi, na wakati mwingine hata kuwatumia wanasiasa,’’alifafanua.



Akichangia mada kwenye kikao hicho, Mkurugenzi wa Jumuiya ya wazalishaji karafuu Zanzibar ‘ZAPCO’ Abubakr Mohamed Ali, alisema woga wa watetezi na wanaharakati huchangia kutofikiwa mwisho kwa wanachokitetea.

‘Suala la kufanya uchechemuzi linahitaji ujasiri, kusoma kidogo, kujua sheria na kanuni na kujiamini na wakati mwingine, hata kuweka kando tamaa, maana kama haya yakijitokeza hakuna uendelevu wa jambo,’’ alieleza.



Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA -Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema bado uwanaharakati unakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo, kutokujua mbinu halisi.




Nae Dina Juma Makota kutoka ‘PEGAO’, alishauri kuwa wakati wa upangwaji wa mikakati na mbinu za kufanya ushawishi na utetezi, makundi maalum, yasiwekwe pembeni.

Mkutano huo wa siku moja, kupitia mradi wa ‘uraia wangu’ umeandaliwa na PACSO kwa ufadhili wa The Foundation for Civil Society kupitia Umoja wa nchi za Ulaya.

                  Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch