Skip to main content

CHAPO: ‘ANZENI MAPEMA KUWAONESHA NJIA ZA KUWA VIONGOZI WATOTO WA KIKE’

 


 

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

 

WAZAZI wanawake wa kijiji cha Jamvini shehia ya Ndagoni, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao, ili kuwaonesha njia za wao kuwa viongozi mapema, ikiwa ni pamoja na kuwalea bila ya ubaguzi.

 

Ushauri huo umetolewa na Masaidizi wa sheria Jimbo la Ziwani, shehia ya Wesha Khadija Said Khalfan, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwenye mfululizo wa mikutano ya kutoa elimu, inayoratibiwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’.

 

Alisema, njia moja wapo ambayo inafaa kuafutwa kwa wazazi hao, ni kuacha ubaguzi wa malezi kama vile kubagua kazi ndani ya familia zao.

 

Alieleza kuwa, kazi kama za kwenda dukani, kushughulikia mifugo, kubeba kuni zinatakiwa zisitolewa kwa ubaguzi, bali watoto wa kike wafanyishwe, ili kukataa dhana ya ubaguzi.

 

Msaidizi huyo wa sheria alieleza kuwa, njia nyingine ambayo inaweza kuwatayarisha watoto wa kike kuwa viongozi wa baadae, ni kuwashirikisha katika mambo yanayofaa ikiwa ni pamoja na madrassa au skuli anayotaka kusoma.

 

‘’Sio vibaya hata kidogo mtoto wa kike, akaulizwa atanaka kusoma madrassa au skuli ipi, na wakati mwingine hata kutaka ushauri wake, juu ya aina ya mlo wa siku,’’alieleza.

 


Aidha alifafanua kuwa, hata kwa upande wa madrassa na skuli, anaweza kukabidhiwa uongozi kuanzia wa darasa moja hadi wa skuli nzima, kama njia moja wapo ya kumzoesha mapema.

 

‘’Kwa mfano skuli kuna nafasi ya Rais, makamu wa rais, spika na naibu wake na hata nafasi za uwaziri, zote hizi mwanafunzi wa kike anaweza kuzoeshwa mapema,’’alishauri.

 

Katika hatua nyingine, Msaidizi huyo wa sheria wa shehia ya Wesha Khadija Said Khalfan, alisema hakuna sheria wala katiba yoyote ulimwenguni, inayomzuia mwanamke kuwa kiongozi.

 

Alielelza kuwa, Katiba zito mbili zimeweka mazingira ya usawa mbele ya sheria na kwamba kila mtu anayo haki ya kugombea, kuchagua na kuchaguliwa pindi akitimiza vigezo na masharti ya kisheria,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, amewakumbusha wanaume kwamba ndio wenye jukumu kubwa la kuzilinda familia kuanzia watoto wao hadi wa jirani.

 

Alieleza kuwa, hipendezi kuona wazazi hao, wanaelekeza nguvu zao zaidi katika kutafuta maisha pekee, bali waelewa kuwa, sasa ulimwengu umebadilika na yapo majanga ambayo huwakumba watoto.

 

Kuhusu kupinga ukatili na udhalilishaji wa kijinsia, aliitaka jamii kila mmoja, kuwa mlinzi kwa mwenzake, ili kuhakikisha hakuna anayezifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.

 

Kwa upande wake Mkaguzi Msaidizi wa Polisi anayefanyakazi katika shehia ya Ndagoni na Wesha Khamis Ali Khamis, aliwakumbusha wanawake hao, juu ya wajibu na haki yao ya kushiriki katika kuomba uongozi ndani ya nchi yao.

 

Alieleza kuwa, wanawake hawajaumbwa kwa ajili ya kuwapigia kura wagombe pekee, bali hata wao wenyewe wanatakiwa kuomba nafasi mbali mbali kwa mujibu wa uwezo wao.

 

‘’Kwa mfano, mnaweza kuomba nafadi za uwakilishi, ubunge, urais lakini pia kwa wenye mamlaka, wanawajibu wa kuwateua kashika nafasi mbali mbali kama za uwaziri na katibu mkuu,’’alieleza.

 

Nae Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Ndagoni Shuwarika Ali Mohamed, alisema bado elimu ya kuomba nafasi mbali mbali majimboni kwa wanawake iko chini, hasa vijijini.

 

‘’Kwa mfano hata ndani ya vikundi vyetu vya wanawake wenyewe, wapo wanawake wamekuwa wazito kujitokeza kuomba au wakiteuliwa kuzishika nafasi hizo,’’alifafanua.

 

Maryam Issa Haji na mwenzake Bimkubwa Mwalimu Mwadini, waliwashauri waalimu wa skuli na madrassa, kuwapa nafasi za uongozi wanafunzi wa kike, ili waanze kujiozesha mapema.

 



Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari za Wanawake Tanzaania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Fat-hya Mussa Said, alisema wamekuwa wakiendesha miradi kadhaa, yenye lengo la kuwaonesha njia wanawake haki ya kugombea uongozi.

 

Mjumbe wa timu ya wanaume wa mabadiliko Pemba, sheikh Abdalla Nassor Mauli, alisema suala la uongozi kwa watoto wa kike, linakubalika katika maeneo wanayoyatawala wenyewe.

                                   MWISHO

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch