Skip to main content

DIWANI WA KIUYU ADHAMIRIA KUMALIZA KERO NDANI YA WADI YAKE

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA 

 

DIWANI wa Wadi ya Kiuyu Pemba kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Nasra Salum Mohamed amesema, atahakikisha anatatua changamoto zote zinazowakabili wananchi ili kuleta maendeleo katika wadi yake.  

 Alisema kuwa, ametatua changamoto mbali mbali na anaendelea kushirikiana na wananchi kuziibua changamoto nyengine ili zipatiwe ufumbuzi kwa ajili ya maslahi yao na Taifa kwa ujumla. 

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika wadi yake alisema, baadhi ya changamoto alizotatua ni pamoja na kuhamasisha kujengwa vyumba vinne vya madarasa katika skuli ya Minungwini na vyumba vinne katika skuli ya maandalizi Kangagani.

 


Mambo mengine aliyoyatatua Diwani huyo ni kuchimba shimo la vyoo (chamber) katika skuli ya Minungwini, kuezeka vyumba viwili vya skuli ya Mjinikiuyu, kujenga matundu manne ya vyoo katika skuli ya tutu Penjewani na ujenzi wa kituo cha Afya Minungwini.

 

Diwani huyo alisema pia alitatua changamoto ya umeme katika kijiji cha Kigongoni, Kage, Kangagani, kupeleka maji katika kijiji cha Kambini, Penjewani na kusaidia kuchimba visima na kutoa michango ya ujenzi wa visima katika maeneo mbali mbali, ili kuona kwamba changamoto za jamii zinatatuka.

 

"Najitahidi sana kusikiliza kero za wananchi na kuzifikisha sehemu husika kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi, nashkuru sana tumefikia hatua nzuri," alieleza diwani huyo.



 

Diwani huyo alieleza, lengo la kugombea nafasi ya udiwani ni kutatua changamoto zilizopo ambazo zinawaathiri sana wanawake na watoto, hivyo aliona atapambana nazo kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi na wadi yake inapata maendeleo, jambo ambalo amefanikiwa kwa kiasi kikubwa.


 


Kwa upande wa mashirikiano na wananchi alieleza kuwa, wamekuwa wakikaa pamoja na kuibua matatizo yaliyomo kwenye wadi yao na kuzifikisha kwenye mamlaka husika kwa ajili ya kutatuliwa.

 

"Nawashukuru sana wananchi wangu kwa kunichagua na kuniunga mkono bega kwa bega, tunashirikiana pamoja na viongozi wengine wa jimbo, kwa kweli tunafanikiwa katika shughuli zetu," alisema Nasra. 

 

Harakati zake za kugombea uongozi Nasra zilianzia pale alipopewa elimu na Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) ya kuanzisha kikundi cha ushirika kupitia mradi wa WEZA ambapo alianza kujijengea ujasiri na kujiamini.

 

"Kwa kweli hapo ndipo nilipoanza kuwa mkakamavu na hatimae kuweza kusimama mbele za watu kujielezea, hii ilinifanyia niingie kwenye uongozi," alisema Diwani huyo.

 

Akielezea changamoto wanazokumbana nazo wakati wa kugombea ni kukatishwa tamaa kwamba hawawezi na kuambiwa watakuwa wahuni ingawa wanapofanikiwa wale waliowavunja moyo ndio ambao huwapa ushauri katika kutekeleza majukumu yao.

 

Kwa upande wao wananchi wa Jimbo hilo walieleza kuwa, wamekuwa wapeleka kero zao kwa diwani huyo, ambapo hukaa pamoja na kuzitafutia njia mbadala za kuweza kutatuliwa.

 

Mwananchi Fatma Jafar Faki alisema kuwa diwani huyo wanashirikiana nae bega kwa bega katika kutatua changamoto zinazowakabili, jambo ambalo linawapa faraja kubwa.

 

Nae mwananchi Asha Omar Rashid alieleza kuwa, pia amewapa ujasiri wa kwenda kufikisha barua za malalamiko sehemu husika baada ya kukaa nae pamoja kuandika kero zao na baadae yeye hwenda kulisemea na kulitilia mkazo.

 

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said alisema kuwa, wanaendelea kuwajengea uwezo wanawake na jamii, ili wawe na muelekeo chanya wa kushiriki kwenye vyombo vya maamuzi.

 

                             MWISHO.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch