Skip to main content

SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO, DK . MWINYI AFUNGUA BARABARA MAENEO HURU MICHEWENI

 


 NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameziagiza taasisi, serikali ya Mkoa na Wilaya kuhakikisha wawekezaji wanaajiri vijana wa maeneo ambayo watawekeza, ili azma ya Serikali kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi iweze kufikiwa.

 

Alisema kuwa, sio jambo zuri kuona mwekezaji anaajiri vijana wa mbali na kuwaacha vijana wa eneo husika, hivyo ni vyema lisimamiwe vizuri hilo, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na uwekezaji, hali ambayo itasaidia kukuza kipato cha wananchi na kuimarika kiuchumi.

 

Akizungumza kwenye uzinduzi wa barabara katika maeneo huru ya uwekezaji Micheweni Aprili 23, 20204, ikiwa ni katika shamra shamra za maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania Dk. Mwinyi alisema, Serikali ya awamu ya nane ya Mapinduzi Zanzibar imedhamiria kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi, hivyo ipo haja kwa wananchi kunufaika na uwekezaji utakaokuwepo.

 


Dk. Mwinyi alieleza kuwa, kuna mambo mbali mbali yanayofanyika kwa ajili ya kuinua kipato cha wananchi wa Pemba, ikiwa ni pamoja na kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa, bandari za kisasa, barabara zenye kiwango cha juu na miundombinu mengine ambayo itasaidia kuimarisha maisha yao.

 

Aidha alisema kuwa, ili uchumi uweze kukua kwa haraka, Wizara ya Uwekezaji isiwe nyuma bali ichangamkie fursa za uwekezaji, ili lengo la serikali liweze kufikiwa.

 

Akizungumzia Muungano Dk. Mwinyi aliwataka wananchi wa Zanzibar kuulinda na kuuthamini Muungano wa Tanzania, ili uweze kudumu na kuendelea kunufaika nao.

 

"Lazima tujivunie kuwa na Muungano huu na wala asitokee yeyote kuubeza kwa sababu kuna mengi tunayoyapata ya kimaendeleo kupitia Muungano wetu, hivyo hatuna budi kuulinda na kuudimisha," alisema Dk. Mwinyi.

 



Dk. Mwinyi aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano wao sambamba na kuishukuru kampuni ya ujenzi wa barabara hizo ya IRIS, kwa kazi nzuri waliyoifanya na kusema kwamba wataendelea kuwapa kazi zao.

 


Kwa upande wake mkandarasi aliesimamia barabara hizo za maeneo huru ya uwekezaji Micheweni mhandisi Suleiman Ali Abdalla alisema mradi huo mpaka kukamilika kwake umegharimu shilingi bilioni 16.9, ambapo awamu ya kwanza zilitumika shilingi bilioni 4 ambayo ilijengwa na wakala wa barabara na awamu ya pili ilijengwa na kampuni ya IRIS ambayo ilitumia shilingi bilioni 12.9.

 

"Mradi huu umesimamiwa na Mamlaka ya Uwekezaji ‘ZIPA’ ambapo tumeokoa fedha nyingi," alisema Mkandarasi huyo.

 

Nae Mkuu wa Mkoa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alisema kuwa, wana kila sababu ya kuendeleza Muungano ili uweze kudumu, kwani kuna maendeleo makubwa yaliyopatikana ndani ya miaka 60.

 

"Kuna mambo mbali mbali ya maendeleo ambayo yametekelezwa na Serikali ya awamu ya nane, ambapo Dk. Mwinyi amejipanga kusimamia imara ili kuhakikisha yanafanikiwa ipasavyo," alisema.

 

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya alisema, ushirikiano kati ya Serikali na wananchi, imesaidia kufanikiwa kila hatua, hivyo aliwataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali, katika kuwaletea maendeleo ya kiuchumi.

 

Alieleza kuwa, wananchi wa Micheweni wana mategemeo makubwa ya kupata maendeleo ya kiuchumi kutokana na wawekezaji watakaowekezwa katika maeneo huru pamoja na ujenzi wa bandari ya Shumba Mjini na ndio maana wanahamasika kuwaunga mkono, ili kuhakikisha wanafanikiwa.

 



Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Sharif Ali Sharif alisema kuwa, wanaendelea kupata matumaini makubwa ya kimaendeleo, kwani ujenzi huo wa barabara katika maeneo huru ndio utachapuza uwekezaji na wananchi watafurahia zaidi.

 

"Mpango wa Serikali wa kukiinua kisiwa cha Pemba kiuchumi naamini utafanikiwa kwani mambo mengi yameshaanza kutekelezwa na wawekezaji wameshaanza kujitokeza hii ni faraja kwetu," alieleza Waziri huyo.

 

Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni Shamata Shaame Khamis alisema kuwa, amefarajika sana kuona uchumi wa wananchi wa Jimbo lake wataimarika kiuchumi kutokana na uwekezaji utakaokuwepo.

 

Muungano wa Tanzania huadhimishwa kila ifikapo Aprili 26 ya kila mwaka, ambapo kauli mbiu ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania ni 'Tumeshikamana, tumeimarika kwa maendeleo ya Taifa letu'. 

 

                   MWISHO .

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch