Skip to main content

SHEHA WAWI: 'KAMATI YANGU YA UTATUZI MIGOGORO IKO 'FIT' AWAPA NENO WANANCHI'

 

 

 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

UONGOZI wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, umesema uko makini na utatuzi wa migogoro ya madai, na kuwataka wananchi wanaposhindwa kupata sulhu wenyewe, kuwafikishia migogoro hiyo, kwa kuikabidhi kamati yake ya utatuzi wa migogoro.

Sheha wa shehia hiyo Sharifa Waziri Abdalla, alisema kwa sasa anayokamati makini na yenye watu wenye uwezo mzuri wa utatuzi wa migogoro, hivyo ni fursa ya kipekee kwa wananchi, kuitumia kamati hiyo.

Alieleza kuwa, kwa sasa anao wasaidizi wa sheria wenye sifa kubwa katika utatuzi, askari shehia, wajumbe wake ambao wameshapata elimu ya utatuzi wa migogoro, jambo ambalo linampa faraja.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, leo Aprili 23, 2024 Sheha huyo alieleza kuwa, haifai kwa jamii, kuifikisha migogoro hiyo ya madai mbele ya vyombo vya sheria, kabla kwanza kupitia kwenye kamati yake.

Alifahamisha kuwa, utaratibu uliokubalika ni kwamba, migogoro yote ya madai, lazima kwanza yasikilizwe ngazi ya shehia na kisha uamuzi upatikane, na ikiwa pande moja haikuridhika, inaweza kuvifikia vyombo vyingine.

‘’Wananchi wa shehia ya Wawi, sasa njooni na migogoro yenu ya madai kupitia kamati yangu, maana ninaowatendaji makini, ambao wanaweza kuonesha njia ya kufikia sulhu,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine Sheha huyo wa shehia ya Wawi, aliwataka wananchi hao, kuendelea kufuatilia mikutano mbali mbali ya wazi, inayoitishwa na kamati yake, ili kupata elimu ya sheria.

‘’Wasaidizi wa sheria, askari shehia wanaungana na wajumbe wangu kuendesha vikao mbali mbali, kwa ajili kutoa elimu au tahadhari ya jambo, ni wajibu wananchi kuhudhuria,’’alifafanua.

Hata hivyo, aliwakumbusha wajumbe wa kamati yake, kuongeza ufahamu wa masuala mbali mbali yanayojitokeza katika jamii, ili wanapotoa elimu iweze kuzaa matunda.

Wakati huo huo Sheha huyo, aliikumbusha jamii kuacha kuzifanyia sulhu kesi zote za jinai, zikiwemo za udhalilishaji, na atakaebainika kufanya hivyo, hatua za kumfikisha mbele ya vyombo vya sheria zitafuata.



‘’Hata kwa wajumbe wa kamati yangu, hili jambo la kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji halipo, hivyo na jamii iendelee kukemea, maana kufanya hivyo kunadhoofisha mapambano dhidi ya ukatili,’’alieleza.

Kwa upande wake Msaidizi wa sheria wa shehia ya Wawi na Mgogoni Fatma Hilali Salim, alisema changamoto kubwa katika utendaji wao wa kazi, ni jamii kutohudhuria mikutano wanayoiitisha.

Alieleza kuwa, wamekuwa wakikosa elimu na maagizo muhimu kwa kule baadhi yao kutohudhuria mikutano wanayoiitisha, jambo ambalo linachelewesha kufikia malengo yao.

‘’Mikutano yetu huzungumzia elimu ya sheria mbali mbali, kama za ardhi, udhalilishaji, wizi, migogoro ya ndoa, matunzo ya watoto, namna ya ukamataji na hata mirathi, hivyo wananchi wakipuuza wanakosa elimu,’’alifafanua.

Katibu wa sheha wa shehia ya Wawi Sham Haroub Said, aliwataka wananchi kuhakikisha kila mmoja, anakuwa mlinzi kwa mwenzake, ili kuona hakuna anaezifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.

Wanachi wa shehia hiyo, wamewataka wenzao kuhakikisha wanahudhuria mikutano mbali mbali inayoitishwa shehiani humo, ili kufikia lengo la utunzaji amani.

Mkuregenzi wa Jumuiaya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema bado wanampango wa kuwanoa zaidi wasaidizi wa sheria, ili kuwasaidia wananchi.



Mratibu wa CHAPO Mohamed Hassan Abdalla, alisema kwa sasa wanaomradi wa upatikanaji haki, ambapo pamoja na shughuli nyingine utakutana na baadhi ya masheha kujenga ukaribu zaidi na ofisi yao.

                                       mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch