Skip to main content

WASOMI WANAOSUBIRI UTEUZI WA RAIS WANAITENDEA HAKI ELIMU YAO?

 

                


NA HAJI NASSOR, PEMBA

KILA leo serikali hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, imekuwa ikitumia gharama kubwa na hadi kufikia kutoa mikopo, ili kuhakikisha wananchi wake wanapata elimu ya juu kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

Siamini kabisa, kwamba eti serikali hii itumie gharama ya kuwasomesha watu kisha wakirudi masomoni, waje wakae vibarazani wasubiri uteuzi wa rais, la hasha bali ni kuisaidia nchi kufikia uchumi wakati.

Maana wapo wasomi walioandika vitabu na tunavisoma  leo hii wakisema kuwa, ili nchi iendelee basi chachu yake kubwa ni kwa wasomi wa ndani kutumia elimu yao kwa ajili maendeleo.

Sasa leo nawauliza hawa wasomi wetu wenye chungu na darzeni ya digrii, kama sio masta na PHD wamalizapo vyuo vikuu na kurudi nchini, mbona hatuwaoni wakifanya jambo au wasubiri uteuzi wa rais?

Jamani wasomi wetu kama hili ni kweli kwamba mmelewa na kusubiri uteuzi wa rais ili ushike nafasi fulani, je kwa mtindo huo ndio tutaufikia uchumi wa kati.

Maana zipo nchi ambazo leo hii zinaendelea kutumiminia misaada ya hali na mali, je waliamka tu siku moja asubuhi na kuwa na uwezo mkubwa wa viwanda, jawabu sio sahihi.

Bali walifanya kazi kubwa ya usiku na mchana bila ya kujali kwamba waliajiriwa serikalini au walifikia uchumi mkubwa eti wasomi wake kwa kuteuliwa………..

Mbona haya hayaingii akilini mwa waliowengi, lazima wasomi wetu wa Zanzibar wajikurupushe na pengine hata kuanzisha umoja wao mithili ya Dayaspora, ili kuona wanaisaidia nchi na wananchi wake.

Hivi sasa kila chochochoro, kila mtaa na kila kijiji kama sio kila familia, utasikia pana kijana tena shababi ana mastar, PHD, digrii mbili na mwengine ni daktari mwenye elimu ya MDs kama sio specialization, lakini wote hawa wanafanyaje au ndio wanaongojea uteuzi?

Maana hawa kama wakiungana pamoja na kuitumia elimu yao ipasavyo, basi wanaweza kufanya jambo ambalo pengine serikali yengehitaji mtaalamu kutoka masafa mapana ya dunia.

Idadi ya wasomi wetu wanaohitimu kila mwaka na kubahatika kurudi nchini wala sio ndogo kihivyo, sasa kama wote hawa eti wanasubiri bomba la Ikulu, watangaazwe kisha ndio waanze kuonesha ujuzi wao wa kikazi, tumechelewa.

Kwani hamuwezi kukusanyika kwa mfano nyote mliosomea kilimo cha vitunguu au jinsi ya ukulima wa pilipili manga kisha mkaanzisha umoja wenu na kuendesha kilimo hicho cha kisasa kupitia mikopo itolewa na serikali, na kupunguza foleni ya ajira serikalini?

Mbona wapo wachache ambao hata hawaingii kwenye kundi la wasomi wanaotajika, leo hii wameshawaokoa vijana wetu kadhaa na wanaendelea kujiletea maendeleo yao.

Chonde chonde wasomi wetu, elimu mliokwenda kuichuma vyuoni sasa tuone matunda yake, maana tumekuwa tukiimba kila siku kuwa, mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe.

Hebu ondoweni fikra butu kuwa, kuiletea maendeleo nchi yako, kwamba eti lazima uajiriwe serikali au kiongozi wa nchi akupe shavu la uteuzi.

Kumbukeni kuwa, maandiko matakatifu yameshaeleza wazi kuwa, mwenye kujua hata aya moja basi awafikishie na wenzake, sasa wewe, yule na hao wanaosubiri uteuzi wa rais ndio waoneshe kazi, tutafika kwa mtindo huu.

Lakini hata wakuu wa taasisi kwa wale watendaji ambao tayari wamo serikalini, msisite kuwatumia mara warudipo vyuoni, maana mabadiliko huanza kwa mtu mmoja wakati mwengine.

Mbona hili la wasomi wetu kusahau uteuzi na kuanza sasa kuifanyia kazi elimu yao, linawezekana kwani hao walioendelea leo walikuwa na akili zipi na sisi tumekosa zipi.

                                        Mwisho 

     

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch