Skip to main content

CHAPO: 'KARIBUNI WASAIDIZI WA SHERIA WAPYA CHAKE CHAKE'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-


MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake 'CHAPO' Nassor Bilali Ali, amewataka wasaidizi wa sheria wapya, wa majimbo ya wilaya hiyo, kufanyakazi kwa bidi, ili kuisaidia jamii, kupunguza matendo ya udhalilishaji.

Alisema, jamii inakabiliwa na majanga kadhaa pamoja na utumiaji wa dawa za kulevya, migogoro ya ndoa, ardhi na matunzo ya watoto, hivyo ni wajibu wao kuona hayo yanapungua.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kuwapokea wasaidizi hao wa sheria, alisema amefarajika kuona, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, imewapa mafunzo vijana hao.

Alisema, moja ya eneo la Zanzibar ambalo haliko salama na majanga mbali mbali ni wilaya ya Chake chake, hivyo wasaidizi hao wa sheria, wanayokazi ya kufanya ndani ya jamii.

‘’Karibuni sana kwenye jumuiya yetu hii, na sisi tumefarajika kuona, tumepata damu changa ya kupambana na majanga mbali mbali, ili tuwe na taifa lenye amani,’’alieleza.



Aidha Mkurugenzi huyo, alisema wakati wa utendaji wao kazi watakuwa karibu na wenzao waliowatangulia, hivyo ni jukumu lao, kuwashirikisha katika harakati zao.

Katika hatua nyingine, alisema kazi iliyofanywa na Wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora kupitia Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ya kuwa na mradi wa kuimarisha upatikanaji haki Zanzibar, ni jambo jema.

‘’Kupatikana kwa wasaidizi wa sheria 50 Unguja na Pemba na wale watano wa majimbo ya wilaya ya Chake chake, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huo,’’alieleza.

Hata hivyo, amewakumbusha wasaidizi hao wa sheria, kujiendeleza kielimu zaidi, ili hapo baadae wawe wanasheria kamili.

Nao wasaidizi hao wa sheria, walisema walikuwa na hamu kubwa ya kupata mafunzo hayo, na sasa kilichobakia mbele yao ni kuihudumia jamii.

Mtarajiwa msaidizi wa sheria Jimbo la Ziwani Nassra Bakar, alisema anachoomba ni ushirikiano wa karibu na wasaidizi wa sheria wakongwe, ili kufanikisha ndoto zake.

Kwa upande wake mtarajiwa msaidizi wa sheri Jimbo la Ole Tuheni Talibu, alimuomba Mkurugenzi huyo, kuangalia uwezekano, wa kuandaa mikutano katika majimbo yote.



Nae mtarajiwa msaidizi wa sheria Jimbo la Chake chake Wahid Kombo, alisema kazi anayoiona ya kuanza nayo, ni kukutana na wanafunzi wa madrassa, ili kuwapa elimu ya kujikinga na matendo ya udhalilishaji.

Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ iliyopo mkabala na Tume za Uchaguzi Chake chake, ambayo imeanzishwa mwaka 2016, moja ya malengo yake ni kuisaidia jamii kufikia upatikanaji wa haki, elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa maskini na watu wenye ulemavu bila ya malipo.

Mwezi Mei mwaka huu, jumla ya wasaidizi wa sheria 18 wa mjimbo ya uchaguzi ya Pemba, waliungana na wenzao 32 wa majimbo ya Unguja, kupata mafunzo ya awali ya wasaidizi wa sheria, yalioendeshwa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa ufadhili wa LSF.

                            MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch