Skip to main content

RC KUSINI PEMBA: 'TUJIPE MNAUPIGA MWINGI MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-


MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahoro Massoud, amesema mchango na juhudi za kupambana na ukatili na udhalilishaji, zinazofanywa na Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE, kama zitaungwa mkono, matendo hayo yanaweza kuwa historia hapo baadae.

Alisema, moja ya tasisi inayofanya kazi ya kushirikiana na jamii na ngazi ya serikali ni TUJIPE, hivyo ni wakati kwa wadau wa haki za wanawake na watoto, kuwaunga mkono katika mapambano hayo.

Mkuu huyo wa Mkoa, aliyasema hayo Gombani Chake chake leo Juni 6, 2022, wakati akizungumza kwenye kongamano la kujadili changamoto za vitendo vya ukatili na udhalilishaji, lililoandaliwa na ‘TUJIPE’ kwa ufadhili wa the foundation for Civil Society.

Alisema, wanaofikiria kuwa serikali pekee inaweza kumaliza matendo hayo ndani ya jamii amekosea, bali juhudi kama za TUJIPE na wengine, wakiungana ni njia moja wapo ya kupunguza matendo hayo.

‘’TUJIPE mmekuwa mkinialika mara kwa mara, katika mikutano au makongamano na hata uzinduzi wa miradi ya kupinga ukatili na udhalilishaji, ni mwanzo mzuri na wengine waige,’’alieleza.

Aidha Mkuu huyo wa mkoa, ameikumbusha jamii kushirikiana na vyombo vya sheria, katika mapambano hayo, ili kuona watuhumiwa wanatiwa hatiani.



‘’Haipendezi kuona mahakama inamuita mzazi, au mlezi au mwengine, ambae anaweza kutoa ushahidi na kukataa, na kufanya hivyo, ni kudhoofisha juhudi za serikali na wadau wake,’’alifafanua.

Mapema Mratibu wa ‘TUJIPE’ Pemba Tatu Abdalla Msellem, alisema wamekuwa wakiendesha mradi wa kupinga ukatili na udhalilishaji kuanzia mwaka 2019, ambao kwa sasa umeshasambaa shehia 13 za wilaya ya Chake chake na Micheweni.

‘’Moja ya eneo la mradi huo ni kuwaelimisha wanafunzi, namna ya kujikinga na vitendo vya ukatili na udhalilishaji, na ndio maana vipo vilabu 13, kweye skuli kadhaa,’’alieleza.



Katika hatua nyingine, Mratibu huyo alisema moja ya changamoto inayozorotesha kumaliza vitendo hivyo, ni ucheleweshaji wa hukumu.

Kwa upande wao wakuu wa wilaya za Micheweni na Chake chake, walisema kama serikali imeshazirekebisha sheria, sasa kilichobakia kwa jamii, ni kushirikiana na vyombo husika, ili washtakiwa waadhibiwe.

Mkuu wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alisema juhudi na ushirikiano wa pamoja unahitajika kila wakati, ili inapotokezea matukio hayo, iwe rahisi kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Nae Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, alisema ndani ya kipindi cha uongozi wake, atahakikisha watuhumiwa wa matukio hayo, wanafikishwa mahakamani.



Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Richard Tatedei Mchomvu aliwataka wanaharakati, kuiangalia upya sheria ya Mtoto nambari 6, yam waka 2011 ya Zanzibar.

‘’Pamoja na uzuri wa sheria ya Mtoto, lakini vipo vifungu ambavyo havizungumzii adhabu kwa wazazi wanaofanya uzembe juu ya malezi, sasa hapa napo lipo tatizo,’’alishauri.

Akiwasilisha mada ya hali halisi ya matukio hayo, Wakili wa serikali Ali Amour Makame, alisema changamoto wanayokumbana nayo, ni waathiria kukataa kutoa ushahidi.

‘’Sasa watoto wanaolalamikia kubakwa ama kulawitiwa, wanapokwenda vituo vya Polisi hutoa maelezo mazuri, lakini wanapofika mahakamani, huyakana maelezo yao,’’alieleza.

Kaimu Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan na Mratibu wa Chama cha Waandishi wa habari Tanzania ‘TAMWA’-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, walisema kesi zinazowahusu wanyonge, hupata hatia mara moja.

‘’Jamii inatulalamikia kuwa, kesi ikimuhusu mfano mteule wa rais au mwenye fedha zake, mara zote wanasema haipati hukumu ya kifungo, na wanatueleza bado hakuna utayari,’’alisema Kaimu Mratib wa ZLSC.



Baadhi ya washirikia wa kongamano hilo, akiwemo Azizi Simai Alawi wa Wawi, Mohamed Ali Hassan waliishauri ‘TUJIPE’ kutoa elimu hiyo ngazi ya skuli na madrassa, ili kuwafikia watoto moja kwa moja.

Sheha wa shehia ya Kichungwani Yussuf Ali Salim, Mkurugenzi wa ‘KUKHAWA’ Hafidh Abdi Said na mwananchi Hasina Hassan Kaduwara walisema, bado hakuna adhabu kali kwa washtakiwa wa makosa hayo.

                Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch