Skip to main content

MNG'ARO WA KANZU, KOFIA ZINAZOVALIWA IJUMAA ZIENDANE NA ROHO ZA WAVAAJI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-

AMA kwa hakika katika siku saba za wiki, waislamu huvaa mavazi ya stara wakiamini kuwa ndio maamrisho ya Muumba hasa kutokana na kuwepo aya na hadithi zinazoeleza hayo.

Suala ka kujistiri kwa waislamu ndio la kwanza katika maisha yao ya kila siku, na wengi wao hufanya hivyo kwa siku zote ingawa kwa siku ya Ijumaa huvaliwa kanzu nyeupe na kofia.

Uislamu ndio njia ya maisha sahihi kwa mwanadamu, maana kila kitu kilichopo duniani kimeelezwa ndani ya uislamu, jinsi ya kutenda au kuacha kutenda jambo hilo.

Roho za watu na kusaidiana nalo halikuachwa ndani ya uislamu na kumbe sio mavazi pekee kama wengine wanavyofikiria kwa kule kuvaa vazi hilo kila siku ya Ijumaa.

Ndio maana leo naja kwenu waislamu kuwataka ule mng’aro wa kanzu na kofia zenye kupendeza zinazovaliwa siku ya Ijumaa ni vyema zikaendana na roho za watu.

Maana uislamu wala haupendi kuona mvaaji wa kanzu na kofia nzuri na kukimbilia msikitini mapema, ikawa nafsi yake imetawaliwa na choyo, roho mbaya na ubaguzi.

Iweje mtu ikifika Ijumaa ajitie kanzu yenye kung’aa na kofia yenye kupendeza lakini huyo huyo, yeye na jirani yake ni kama paka na moshi?

Au ndio wale tunaowaita waislamu wa mavazi, lakini mioyo yao iko wazi kwa kutosema na majirani zao, au ndugu wa baba na mama lakini ikifika Ijumaa kanzu aliovaa utasema huyu ni Al-haji wa Makka.

Hebu tukaeni na kufikiria ni kwenye uislamu tunatakiwa tukae na kuishi na wenzetu, au ibaki yatosha kuvaa kanzu na kofia nzuri na pengine hata kuwahi Masjidi mapema, lakini kwenye nafsi, bado kuna moshi wa husda na choyo.

Hebu tuzionee huruma kanzu na kofia zetu tunazovaa Ijumaa, ili kesho na keshokutwa zisijetusuta, maana roho zetu haziko nyeupe kama yalivyo mavazi yetu.

Ingependeza zaidi kuona roho na nafsi zetu zinaendana na kanzu zetu tunazozivaa siku ya Ijumaa, ambayo ni sikukuu kwa waislamu, badala ya roho zetu kuwa nyeusi mithili ya maji ya mkondoni au lami.

Na pengine sasa ingekuwa jambo jema zaidi kuona, swala zetu zinaanzia kwa ndugu, jamaa, wazazi, marafiki na majirani zetu kwa kuishi nao kama uislamu ulivyoagiza, ili sasa tukivaa zile kanzu zetu zifanane na matendo yetu.

Haingii akili na wala haikubaliki ndani ya uislamu kuona jirani mmoja hasemi na mwenzake, kwa sababu wanazozijua mwenyewe, iwe kwa sababu ya rangi, kabila, eneo analotoka au hata chama, maana uislamu hakuna neno ubaguzi.

Sasa lazima tujikite katika kuisaka pepo kuanzia ndani ya nafsi zetu kwa kuzisafisha badala ya kujipendezesha kwa mavazi, na pengine hapo mtu kujiona ameshaokoka, ingawa hajui hali za jirani yake.

  Yote kwa yote mavazi yetu hasa kwa siku ya Ijumaa yanayopendeza na kung’aa basi yaendane na roho na nafsi za mvaaji.

Lakini hata na masheikh na wanazuoni wetu, mnayonafasi ya kulisemea hili kwa mnaowaongoza, maana inawezekana wapo wanaofikiria kuwa uislamu ni mavazi.

Lakini ni fardhi au lazima kwa muislamu mwanamke na mwanamme kusaka elimu tena hadi China, ili kujitambua na kujielewa, maana mavazi na imani ni vitu viwili tofauti.

Mimi naamini kila kitu kinawezekana ikiwa kila mmoja atatekeleza wajibu wake, tena bila ya kusubiri kusimamiwa, huku akiamini kuwa mtenda wema ajitendea nafsi yake.

                        Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch