Skip to main content

WAZAZI WENYE WATOTO THAMARAT NISSAI WAKUMBUSHWA JAMBO

 



NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@

UONGOZI wa skuli ya kiislamu Thamaratu-nnisai iliyopo Machomane wilaya ya Chake chake Pemba, imewakumbusha wazazi na walezi, kulipa ada zao kwa wakati, ili kurahisisha ufanisi wa usomeshaji skulini hapo.

Akizungumza na wazazi na walezi wenye wanafunzi skulini hapo, Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bimkubwa Habibu, alisema wapo baadhi ya wazazi, bado wamenakuwa wazito kulipa ada za watoto wao.

 

Alieleza kuwa, hilo linachangia uzoroteshaji wa skuli hiyo, ikiwemo usomeshaji na hata malipo ya mishahara ya waalimu walipo skulini hapo, ambao wanazitegemeza ada hizo.

 

‘’Nyinyi wazazi na walezi, ambao mmewaleta watoto wenu skulini hapa, jambo la kwanza mhakikishe suala la ada halichelewi, maana ndio tegemezi kuu, kwa maendeleo yote ya skuli hii,’’alieleza.

 

Aidha Mwalimu Mkuu huyo amewakumbusha wazazi na walezi hao kuwa, wakumbuke kuwa, skuli hiyo hina mfadhili, anaeiendesha bali inategemea mno ada watakazozilipa kwa ajili ya watoto wao.

 

Akizungumzi kuhusu changamoto inayoikabili skuli hiyo, Mwalimu mkuu huyo alisema ni ukosefu wa huduma ya umeme, vikalio, maji safi na salama na madara mingine kubali na vumbi.

 

Alisema kua wanafunzi wanapata shida kutokana na miundombinu katika skuli hiyo, kwani skuli bado haijapata ufadhili kwa ajili ya kuendelea majengo yake na wanafunzi wakasoma kwa utulivu.

 

"Katika skuli hii hatuna viti vya kukalia wanafunzi, hatuna compyuta, huduma ya nishati ya umeme, na kwa sasa jingo tunalotumia linahitajia ukarabati mkubwa, kwa hivyo tunaiomba serekali na wafadhili wingine kututupia jicho,"alifafanua. 

 

Aidha alisema kua kulingana na muendelezo mazuri wamatokeo ya wanafunzi wao, wataanzisha darasa la tisa (kidato cha kwanza) kuanzia mwaka 2024, wakati hapo awali walikua  wanafundisha mwisho darasa la saba pekee.

 

Hata hivyo alieleza kua kwaupande wa watoto wa elimu ya maandalizi, watakao wandikishwa mwaka 2024, watasoma madrassa hapo hapo, pale utakapofika muda wakuondoka skuli wao watabakia kwa ajili ya kusoma qur-an.

 

"Tutakua tunawanapatia chakula cha mchana na baadae wataanza kusoma qur-an kuanzia muda wa saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni na kurejema majumbani,"alifafanua.

 

Kwaupande wake Msaidizi mwalimu mkuu wa skuli hiyo Amina Salim alisema kua, wazazi na walezi wajitahidi kuleta kuongeza ushirikiano baina yao na waalimu kwani, kufanya hivyo kutasababisha kuwatia nguvu na hamasa waalimu katika ufundishaji wao.

 

"Kuna ada mbalimbali ambazo wazazi  wanatakiwa kulipa kwa wakati, zikiwemo za kulipia usafiri wagaro, dakhalia, mitihani, siku ya wazazi ‘parent day’  pamoja na ada ya safari kwa wanafunzi,’’alifafanua.

 

Aidha alisema kua kuanzia mwaka 2024, wazazi watatakiwa kulipia ada kupitia mifumo ya kibenki, kwani kufanya hivyo  kunaweza kuepuka usumbufu unajitokeza baina ya wazazi na walimu, hasa juu ya deni la wamafunzi.

 

Wakitoa maoni yao baadhi ya wazazi na walezi akiwemo Omar Ali, alitaka kujua watakapoanzisha kidato cha kwanza, wanafunzi watakua na walimu wa kutosha ambao wataweza kuwasaidia katika masomo yao ya kila siku.

 

‘’Mimi nataka kujua, maana kila skuli inauhaba wa waalimu, na sisi Thamarat Nissai, tunao waalimu wa kutosha na watakaosomesha masomo yote na kwa wakati,’’alihoji mzazi huyo.

 

Nae mzazin Burhan Said, aliuomba uongozi wa skuli hiyo, kuanzishwa kwa kamati ya wazazi, ili kusaidia kupanga mikakati mbali mbali, ili kuihuisha skuli hiyo na chamngamoto kadhaa.

 

" Tukiwa kama sisi wazazi tutaunda kamati, ili kila mmoja kama anamtu ambae yupo juu kidogo kimaisha, akamuelezea changamoto zetu na akazisikiliza basi tutaweza kupata maendeleo mazuri yale ambayo walimu wetu wanayalilia kwamuda mrefu,"alieleza. 

 

Aidha aliwashukuru walimu wa skuli hiyo ya Thamarat Nnissai kuweza kufikiria kuweka madrassa ya qur-an ambayo itawasaidia watoto kupata utulivu wa kutafuta elimu.

 

‘’Naelewa kuwa, skuli hii na hasa waalimu wengi ni wanawake, hivyo sasa iwe fahari kwanza, hakuna mchanganyiko na wanaume lakini sasa iwape kasi na ari ya kufanyakazi,’’’alishauri.

 

Skuli hiyo ambayo ilianzsishwa mwaka 2014 ikiwa inawanafunzi wanane, wa waalimu wawili wanakwe, hadi sasa inao wanafunzi 206 na walimu 13, ambao wote ni wanawake na madarasa tisa.

 

                          Mwisho

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch