Skip to main content

LFS YAKUNWA UTOAJIA MSAADA WA KISHERIA ZANZIBAR

 

NA HAJI NASSOR, ZANZIBAR@@@@

MWAKILISHI wa taasisi ya LFS, Wakili Alphonce Gura, amesema kwa sasa Zanzibar, imekuwa sehemu ya kujifunzia katika utoaji wa msaada wa kisheria kwa nchi za Afrika Mashariki.

Alisema, hayo yamejitokeza tokea lilipomalizika jukwaa la pili la Msaada wa kisheria mwezi Disemba mwaka 2022, lililofanyika Zanzibar, na kuibuliwa maazimio ambayo yalilenga kutekelezwa.

Wakili huyo, aliyasema hayo Novemba 20, 2023, wakati akitoa salamu za LSF, kwenye jukwaa la tatu la Msaada wa kisheria, lililofanyika ukumbi wa mikutano Chuo cha Utalii Maruhubi mjini Zanzibar.

Alisema, kwa nchi za Ruwanda, Burundi, Unganda, Kenya na hata Tanzania bara, Zanzibar kwa sasa, imekuwa kinara na sehemu ya kujifunzia, kwa upekee na ubora wa utoaji wa msaada wa kisheria.

‘’Sisi LSF, tunaridhishwa na tunapongeza mno kazi inayofanywa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, kwa kuongeza wigo na kusababisha kuchukua nafasi ya kwanza, kwa utoaji wa msaada wa kisheria,’’alieleza.



Katika hatua nyingine, Wakili huyo na Mwakilishi wa LSF Alphonce Gura, alieleza kuwa, amevutiwa mno na kaulimbiu ya mwaka huu, juu ya ‘kuimarisha huduma za msaada wa kisheria zenye ubora na zinazozingatia matokeo’, kwamba inakwenda na wakati.

Akizungumzia kanzi data, ambayo imeanzishwa na LSF kwa muda mrefu, alisema inaangalia na kuzichakat kazi, zinazofanywa na wasaidizi wa sheria mmoja moja kwa Tanzania nzima.

Alieleza kuwa, kupitia kanzi data hiyo, imedhihirisha uhitaji mkubwa wa msaada wa kisheria na kufikia watu 200,000 kila mwaka na kufikia watu milioni 7 kwa mwaka wanaohitaji elimu ya sheria.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, akiwasilisha yatokanayo na jukwaa la pili la msaada wa kisheria Zanzibar, alisema ni pamoja na azimio la kuifanyia marekebisho sheria ya Msaada wa kisheria.



Jingine alisema, ni azimio la kuanzishwa kwa mfuko wa msaada wa kisheria, jambo ambalo tayari Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, wameshawasilisha andikoni la kwanza wizarani.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo, ameupongeza uongozi wa taasisi za LSF na UNDP, kwa kuendelea kuinga mkono Idara hiyo, ili kuona jamii inaendelea kupata elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

‘’Kwa hakika, wenzetu hawa wamekuwa wakitubeba kila siku, katika shughuli zetu mbali mbali, na hata kuadhimisha majukwaa kama haya, na sasa tunajivunia kwa jamii,’’alieleza.

Akifungua Jukwaa hilo, Naibu Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Shaaban Ramadhan Abdalla, alisema majukwaa kama hayo, husababisha watoa msaada wa kisheria, kupata nafasi ya kujadili mafanikio na changamoto zao.




Alieleza kuwa, kazi inayofanywa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria na hadi kupelekea kutekeleza majukwaa matatu kwa sasa, imekuwa ndio jambo pana na lenye kutoa wigo, na kujipima kwa watoa msaada wa kisheria.

‘’Kwa hakika majukwaa haya ya msaada wa kisheria, yanatoa dira na mwelekeo kwa watoa msaada wa kisheria, ambao wanakwenda moja kwa moja kuwahudumia wananchi, tena bila ya malipo,’’alifafanua.

Hata hivyo Nibu Mwanasheria mkuu huyo mkuu wa Zanzibar, alielezea kuvutiwa na kusikia kuwa yametekelezwa kwa vitendo maazimio yatokanayo na jukwaa la pili la msaada wa kisheria.

‘’Kwa hakika ni jambo jema, kusikia kuwa rasimu ya msaada ya kisheria imeshapita katika baadhi ya ngazi, kwa ajili ya kuifanyiwa  marekebisho sheria hiyo,’’alifafanua.

Mwakilishi wa kutoka wizara ya Katiba na sheria ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Edith Shekidele, alisema amekuwa akivutiwa mno na kazi inayofanywa na wizara kama hiyo Zanzibar, hasa katika kuwafikia wananchi.




‘’Wananchi wamekuwa wakitutegemea mno katika kuwafikia, hasa eneo la utoaji wa msaada wa kisheria, ingawa kwa hapa Zanzibar kazi inafanywa kubwa mno,’’alifafanua.

Akiwasilisha mada ya bajeti ya msaada wa kisheria, Mkuu wa skuli ya sheria Zanzibar Dk. Ali Uki, alisema bado changamoto ni kuendelea kuwategemea wafadhili, kwa asilimia kubwa kuendeshea asasi.



Akichangia mada hiyo, Mkurugenzi wa Shirika la Msaada wa kisheria na haki za binaadamu Zanzibar ‘ZALHO’ Harusi Miraji Mpatani, alisema juhudi inayohitajika ni wanaasasi, ili kuwa na vyanzo mbadala vya mapato.




Mahafoudhi Shaaban Haji, alisema vikwazo kwa asasi na hasa zile za watoa msaada wa kisheria, ni kukosekana taaluma ya kuibua njia za kupata mapato.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu Tawala za Mikoa na serikali za mitaa, Zainab Khamis Kibwana, alisema lazima matumizi ya rasilimali fedha zitumike, kwa mujibu wa vipaumbele.

Hili ni jukwaa la tatu la msaada wa kisheria, ambapo kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘kuimarisha huduma za msaada wa kisheria zenye ubora na zinazozingatia matokeo’.

Mwisho



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch