Skip to main content

MIUNDOMBINU USHAHIDI WA KIELEKTRONIKI KAA LA MOTO MAHAKAMANI

 


Na Mwandishi Wetu

SHERIA ya ushahidi ya Zanzibar ya mwaka 2016 iliyoanza kutumika Januari 18, 2017, imeanzisha utaratibu maalum wa kisheria wa kupokea ushahidi wa kielektroniki. Sheria inatoa uhakika katika kupokea na kukubali ushahidi wa kielektroniki.


Kifungu cha 71 hadi 73 vya sheria vinaeleza jinsi ushahidi wa kielektroniki unavyoweza kukusanywa na kushughulikiwa.


Uwepo wa sheria hii ni dhahiri kwamba ushahidi wa kielektroniki unaweza kutumika wakati wa uchunguzi wa kesi za udhalilishaji wa kijinsia.


Hata hivyo, utekelezaji unafanywa kwa kiwango kisichoridhisha sana, hali inayosababisha waathirika kutopata haki kwa wakati.


Aidha, wakati sheria inaruhusu wapelelezi kukusanya ushahidi wa kielektroniki, polisi bado hawana ujuzi wa kutosha wa jinsi ya kukusanya ushahidi wa kielektroniki.


Ofisa wa makosa ya mtandao kutoka Jeshi la Polisi Zanzibar, Issa Mohamed Salum, "Hatujapewa mafunzo ya kukusanya ushahidi wa kielektroniki. Bado tunaandika maelezo ya waathiriwa kwenye karatasi.


 Lakini ikiwa waendesha mashtaka wanataka ushahidi wa sauti na picha, tunaweza kukusanya, lakini bado hakuna miongozo.”anasema.


Sara Omar Hafidh, Hakimu wa mahakama ya mkoa wa Vuga anayesimamia kesi za udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, anakiri kwamba sheria ya kukubali ushahidi wa kielektroni, lakini ushahidi wa kielektroniki una mapungufu.


"Inaweza kuwa sauti ya mwathirika, lakini vipi ikiwa mwathirika atasema sauti si yake. Katika hali kama hiyo, hakimu bado asingeweza kutoa uamuzi.”anasema.


Hata hivyo, anakiri kwamba mahakama inaendelea kupokea ushahidi wa kielektroniki ingawa sio kwa kiasi kikubwa lakini kutakuwa na maboresheo kadri changamoto zitakapoibuka.


Wadau wa kupinga udhalilishaji Zanzibar wanaishauri Serikali kukarabati na kuboresha miundombinu ya Mahakama maalum ya kushughulikia kesi za udhalilishaji Zanzibar ikiwa ni pamoja na kuwezesha matumizi ya ushahidi wa kielektroniki ili kuwa rafiki kwa wanaotumia mahakama hizo na kuwezesha upatikanaji wa haki katika mazingira bora.


Wanasema licha ya mahakama hiyo kuonesha mafanikio makubwa ya usikilizaji wa kesi tangu kuanzishwa kwake lakini bado miundombinu yake haitoshi kutokana na kukosekana kwa vyombo vya kisasa vya usikilizaji wa kesi, ikiwemo mifumo ya kidigitali (video conference) na ukosefu wa vyumba maalum vya kuwaweka watoto walioathirika na vitendo hivyo.


Hawra Shamte, anansema TAMWA Zanzibar hivi karibuni ilifanya utafiti Unguja na Pemba ambapo ilibaini ukosefu wa vifaa katika mahakama na miundombinu duni bado ni changamoto, mfano majengo ya Mahakama ya Vuga, Mahonda, Mkoani na Wete Pemba ni ya zamani na karibu kupitwa na wakati wakati jambo linalopelekea ugumu katika uendeshaji wa kesi za udhalilishaji.


Jaji Mkuu wa Zanzibar, Khamis Ramadhan Abdallah, anasema kuwa ushahidi wa kieletroniki unatumika Mahakamani lakini kunachangamoto ikiwemo weledi kwa watendaji katika ushahidi wa kieletroniki.


“Kinachokosekana ni weledi wa kufanya upelelezi wa kiushahidi wa kieletroniki, lakini kukosekana uweledi kwa Polisi ambao ndio wanaosimamia shauri, kwa waendesha mashtaka wanaokuja mahakamani kuja kuthibitisha kosa lakini pia kwa mahakimu na majaji ambao ambao shauri wanalitolea mamauzi”anasema.


Aidha anasema wote hao wanajisomea wenyewe kujiendeleza na hazani kuwa wote hao kama wanaelimu nzuri jinsi ya kuutumia ushahidi wa kieletroniki na mara nyingi wahalifu huwa wapo vizuri.


Anasema kuna haja kusimamia vizuri hilo kuendeleza mafunzo kwa watendaji wote kwa sababu huo ndio uhalifu wa kisasa wa kieletroniki.


Anasema makosa ya udhalilishaji wa kijinsia ni muhanga wa makosa ya kieletroniki na mahakama imejipanga kuwa na vifaa vya kusikiliza ushahidi wa kieletroniki.


“Serikali hii mahakama tumejipanga kuwa na vifaa vya kieletroniki katika usikilizaji wa mashauri, na sisi tukiwa mbele wezetu DPP, ZAECA, POLISI na taasisi zingine ziwezeshwe katika kupata vifaa hivyo”anasema.


Kwa mujibu wa Ofisi ya mtakwimu mkuu wa Serikali Zanzibar kwa mwezi wa Oktoba mwaka huu jumla ya matukio 199 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa, yakiwa na idadi ya waathirika 199 wa matukio hayo, ambapo waathirika wengi wakiwa ni Watoto kwa asilimia 78.9, wanawake 16.1 na wanaume asilimia 5.0.


Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch