Skip to main content

MJASIRIAMALI WA MBAO PEMBA AKERWA KUCHELEWESHEWA KIBALI UKATAJI MITI

 



NA KHADIJA OMAR, PEMBA@@@@

MJASIRIAMALI wa uchongaji na utengenezaji wa bidhaa za miti, Mohamed Hamza Khamis wa Kuyuni shehia ya Ngwachani wilaya ya Mkoani, ameziomba mamla husika kutoa ruhusa ya haraka ya ukataji miti, mara wanapokamilisha taratibu.

 

Alisema, inawezekana kufuata taratibu zote kuanzia kwa sheha hadi Idara ya misitu, kwa ajili ya kukata miti ya mbao ingawa changamoto ni ucheleweshaji wa utaji wa kibali husika.

 

Hayo yamelezwa na mjasiriamali huyo, wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizim kijijini hapo, juu ya changamoto anazopitia katika kazia yake.

 

Alisema, jambo hilo la kucheleweshwa kupewa kibali, humuwawia vigumu na kusababisha migogoro isiyokuwa ya lazima na wateja wake, kwani wanakuwa hawamuelewi.

 

Alieleza kuwa, kufanya hivyo wakati mwingine kunasababisha kumkimbizia wateja kwani, wengi wao hupenda kazi zao zifanywe kwa haraka mno.

 

''Changamoto yangu kubwa ni kucheleweshwa kupewa kibali cha ukataji miti ya mbao, hata kama nimeshakalimisha taratibu zote zikiwemo kulipia ushuru kwa idara husika,’’alieleza.

 

  Akizungumzia kuhusu vifaa anavyotumia, alisema hadi sasa anatumia misumeno ya nguvu, shoka, landa yay a kutumia mokono jambo ambalio humpelekea kuchoka mno.

 

Alifafanyua kuwa vifaa alivyonavyo sio vya kutosha, na kumsababisha wakati mwingine hata kuchelewa kumaliza kazi za wateja wake.

 

‘’Kama kuna mfadhili japo kwa njia ya mkopo naomba, na mimi kupatiwa vifaa vya kukatia na kusafishia bidhaa zangu, maana kwa hakikia napoteza nguvu sana,’’alieleza.

 

 

Kuhusu rasilimali anazozitumilia, alisema anazinunua kutoka miji ya kama vile Kangani, Kengeja ingawa kutokana na gharama ya usafirishaji hupata gharama ndogo.

 

‘’Kwa mfano magogo ninayonunua kwa shilingi milioni 1 na kutengeneza bidhaa kama kabati la milango miwili, gharama zake hadi kukamilika ni shilling 300,000, na kisha kulazimika kuliuza kati ya shilingi 400,000 hadi shilingi 500,000 na kujipatia faida ya shilingi 150,000,’’alifafanua.

 

Hata hivyo alisema anaweza kutengeneza vifaa vyingine kama vile viti, fremu za madirisha, milango na meza ndogo ndogo za chumbani.

 

Kuhusu changamoto anazokumbana nazo, mjasiriamali huyo, Mohamed Hamza Khamis, alisema kuwacheleweshea baadhi ya wateja wake, kutokana na kukosa vifaa vya kileo.

 

‘’Mteja anaweza kutoka masafa ya mbali na kuja kufuata bidhaa zake, lakini akifika akanikuta naendelea kugonga gonga na kuweka urembo sanwa,’’alisema.

 

Mmoja katia wateja wa mjasiriamali huyo , Ali Omar Ali alisema kama atapatiwa vigfaa vya kileo, anaweza kuzalisha bidhaa nzuri zaidi.

 

Alieleza kuwa, amekuwa kila wakati ananunua bidhaa za mbao kwake na wakati mwingine hata kusafirisha kwenda kwa watu wengine, kutokana na ubora wake.

 

‘’Ni kweli mimi ni mteja maarufu wa mjasiriamali huyo, na amekuwa akichonga kitanda, makabati na meza za aina mbali mbali, lakini changamoto yake hadi leo anatumia vifaa vya nguvu kazi,’’alisema.

 

Kiwanda cha kuchongea fanicha mbali mbali kilichopo Kuyuni Ngwachani, mjasiriamali huyo, amekianzishwa mwak 1992 kwa mtaji wa shilling 70.

 

                                        MWISHO

Comments