Skip to main content

JUKWAA LA TATU LA MSAADA WA KISHERIA ZANZIBAR, WAZIRI HAROUN AAMSHA SHANGWE UKUMBINI 'SOMA HIYOOO'.....LSF WASEMA JAMBO

     


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

NOVEMBA 20 na 21 mwaka huu, ilikuwa siku nyingine adhimu na adimu, kwa wadau wa haki jinai Zanzibar.

Siku hii, ambayo kila mwaka hujitokeza mara moja, ni kwa ajili ya kuwakutanisha wadau wa haki jinai na washirika wao, kujadili mafanikio, changamoto za utoaji wa msaada wa kisheria.

Kwa jukwaa hili la tatu la mwaka huu, ambalo lililfanyika Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja, kama kawaida wadau wa haki jinai, kutoka kuona zote Tanzania, walihudhuria.

Hapa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, iliyochini ya Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria na Utawala Bora ikishirikiana kwa karibu na wadau wake LSF na UNDP, iliwavuta washiriki kutoka Pemba na Tanzania bara.

Wenyeji waliopo Unguja, ndio waliokuwa na kazi ya kuwakaribisha wageni wao, kutoka maeneo mbali mbali, na si haba jukwaa, lilifana.

YALIOJIRIA KATIKA JUKWAA LA TATU LA MSAADA WA KISHERIA 2023

Jukwaa hili, lilifunguliwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Shaaban Ramadhan Abdalla, ingawa kabla ya hutuba yake, iliyowavutiwa wengi kulitanguliwa na yatokanayo na jukwaa la mwaka 2022.

Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Abdalla, ambae kiprotokoli ndie mwenye jambo lake, aliyasoma maazimio hayo.

Kwanza akaeleza kuwa, majukwaa hayo yamekuwa na tija mno katika kuweka mazingira rafiki, kwa watoa msaada wa kisheria pamoja na wasaidizi wa sheria.

Akisema kuwa, kinachoaahidiwa kupitia majukwaa hayo, yamekuwa yakitejelezwa, akitolea mfano yale yalioahidiwa mwaka 2022, kwenye jukwaa la pili la msaada wa kisheria.

Lakini kwanza Mkurugenzi huyo, akaelezea malengo ya jukwaa la tatu la Msaada wa kisheria, akisema moja ni kuimarisha ufanisi na uweledi wa utendaji wa majukwaa ya watoaji wa msaada wa kisheria.

‘’Kuwezesha upatikanaji wa sera na sheria mpya, zinazokidhi mahitaji ya jamii, katika upatikanaji wa huduma za kisheria, kuanzisha upatikanaji wa sahihi wa taarifa za utoaji wa huduma za msaada wa kisheria,’’alitaja maazimio.




Akafafanua kuwa, lengo jingine ni kukuza ubunifu na kuimarisha uwezo wa watoaji wa msaada wa kisheria, katika kuendeleza majukumu yao ya kazi za kila siku.

Mkurugenzi Hanifa akaweka wazi kuwa, lengo jingine ni kuwaunganisha watoa msaada wa kisheria na taasisi nyingine, ili kuwawezesha kufanyakazi kwa ufanisi.

Baada ya kueleza dhamira ya jukwaa la tatu, sasa Mkurugenzi huyo, akawakumbusha washiriki hao kuwa, kwa yale maazimio ya Disemba 13 na 14, 2022, nayo yameshatekelezwa.

Hapa akatoa mfano wa machache, ni pamoja na kutakiwa kuifanyia marekebisho sheria ya Msaada wa kisheria ya mwaka namba 13 ya mwaka 2018 pamoja na sera yake, sambamba na kuweka mfuko wa msaada wa kisheria.

Akisema kuwa, kazi hiyo ilipewa Idara yake pamoja na Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibara, na tayari andiko la kwanza limeshapelekwa wizarani.

‘’Kwa hili, tayari rasimu ya sera ya msaada wa kisheria imeshaandaliwa, na hili ni baada ya kukukusanywa maoni, ya wadau wa Unguja na Pemba na uanzishwaji mfuko limezingatiwa,’’akafafanua.

Azaimio jingine ambalo limseshatekelezwa ni kuitaka Mahkama na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria, kushirikiana na wasaidizi wa sheria katika utoaji wa elimu ya kisheria.

‘’Na hili tayari Mahkama ililitekeleza, maana ilishirikiana nao, katika shehia za Kidombo, Gamba, Mcheza shauri na Tumbatu kwa Unguja kutoa elimu ya sheria,’’anafafanua.

Serikali kuzingatia nafasi za ajira kwa watu wa wenye mahitaji maalum, limeshatekeleza kwani wapo watumishi watatu, wameshaajiriwa.



Suala la kuweka wakalimani wa lugha ya alama, katika vituo vya Polisi, kwa sasa tayari watendaji kadhaa wa Jeshi la Polisi, wako masomoni, kusomea lugha ya alama.

LSF

Kisha zamu ikawa ni ya mwakilishi kutoka taasisi za LSF Wakili Alphonce Gura, akisema kwa sasa Zanzibar, imekuwa sehemu ya kujifunzia katika utoaji wa msaada wa kisheria, kwa nchi za Afrika Mashariki.

Anasema hayo yamejitokeza tokea lilipomalizika jukwaa la pili la Msaada wa kisheria mwaka 2022, lililofanyika Zanzibar, na kuibuliwa maazimio, 13 yaliyotekelezwa.

Wakili huyo, anasema kwa nchi za Ruwanda, Burundi, Uganda, Kenya na hata Tanzania bara, Zanzibar imekuwa kinara na sehemu ya kujifunzia, utoaji wa msaada wa kisheria.

‘’LSF, tunaridhishwa na tunapongeza mno, kazi inayofanywa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, kwa kuongeza wigo na kusababisha kuchukua nafasi ya kwanza, kwa utoaji wa msaada wa kisheria,’’anafafanua.




Gura, amevutiwa mno na kaulimbiu ya mwaka huu, juu ya ‘kuimarisha huduma za msaada wa kisheria, zenye ubora na zinazozingatia matokeo’, kwamba inakwenda na wakati.

Akizungumzia kanzidata, ambayo imeanzishwa na LSF mwaka 2013, inayoangalia na kuzichakata kazi, zinazofanywa na wasaidizi wa sheria, mmoja mmoja kwa Tanzania.

Kupitia kanzidata hiyo, imedhihirisha uhitaji mkubwa wa msaada wa kisheria na kufikia watu 200,000 kila mwaka na kufikia watu milioni 7 kwa mwaka, wanaohitaji elimu ya sheria Tanzania.

Jukwaa hilo la tatu la mwaka 2023, lilifunguliwa na Naibu Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Shaaban Ramadhan Abdalla, akasema majukwaa hayo, husababisha watoa msaada wa kisheria, kupata nafasi ya kujadili mafanikio na changamoto zao.




Kazi inayofanywa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria na hadi kupelekea kutekeleza majukwaa matatu kwa sasa, imekuwa ndio jambo pana na lenye kutoa wigo, na kujipima kwa watoa msaada wa kisheria.

‘’Kwa hakika majukwaa haya, yanatoa dira na mwelekeo kwa watoa msaada wa kisheria, ambao wanakwenda moja kwa moja kuwahudumia wananchi,’’anafafanua.

Alielezea kuvutiwa mno kusikia kuwa, yametekelezwa kwa vitendo maazimio yatokanayo na jukwaa la pili la msaada wa kisheria.

‘’Ni jambo jema, kusikia kuwa rasimu ya msaada ya kisheria imeshapita katika baadhi ya ngazi, kwa ajili ya kuifanyia  marekebisho sheria hiyo,’’anafafanua.

Mwalika kutoka wizara ya Katiba na Sheria ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Edith Shekidele, nae akavutiwa mno na kazi inayofanywa na wizara kama hiyo Zanzibar, hasa katika kuwafikia wananchi.




‘’Wananchi wamekuwa wakitutegemea mno katika kuwafikia, hasa eneo la utoaji wa msaada wa kisheria, ingawa kwa hapa Zanzibar kazi inafanywa kubwa mno,’’anafafanua.

Mmoja wa wawasilisha mada kwenye jukwaa hilo, Mkuu wa skuli ya sheria Zanzibar Ali Uki, kwenye mada yake ya bajeti ya msaada wa kisheria, akasema bado changamoto ni kuendelea kuwategemea wafadhili, kwa asilimia kubwa kuendeshea asasi.

‘’Lazima asasi ziangalie uwezekano wa kuibua njia mbadala za vyanzo vyengine vipya vya mapato, badala ya kutegemea wafadhili wa nje pekee,’’anafafanua.



Akichangia mada hiyo, Mkurugenzi wa Shirika la Msaada wa kisheria na haki za binaadamu Zanzibar ‘ZALHO’ Harusi Miraji Mpatani, anasema juhudi inayohitajika ni wanaasasi, kuwa na vyanzo mbadala vya mapato.

Hata Mahafoudhi Shaaban Haji mwakilishi wa asasi za kiraia Zanzibar, anasema vikwazo kwa asasi na hasa zile za watoa msaada wa kisheria, ni kukosekana taaluma ya kuibua njia za mapato.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu Tawala za Mikoa na serikali za mitaa, Zainab Khamis Kibwana, anasema lazima matumizi ya rasilimali fedha zitumike, kwa mujibu wa vipaumbele.

Kwa siku ya pili, katika jukwaa hilo kulikuwa na mada mbili, moja wapo ni mifumo ya ufuatiliaji na tathmini na matokea, katika sekta ya sheria, iliyotolewa na Saada Mkwangwa.

Ni Afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka taasisi ya LFS, ambae anasema ufuatiliaji mzuri ni ule ambao utakuwa na takwimu na kuonesha uhitaji wa wateja.

Mada nyingine ambayo iliwasilishwa ni uunganishaji wa mifumo ya ufuatiliaji na tathmini, iliyotolewa na Rukaiya Khamis Othman, Mkuu wa Divisheni ya Ufanisi na uchambuzi wa mifumo.

Kisha Waziri wa Nchi, Ofisi yaa Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman, alilighairisha jukwaa hilo na kutamka rasmi kufuta ada ya usajili kwa wasaidizi wa sheria.

‘’Naelewa vyema kuwa, wasiaidizi wa sheria, mnalipa ada ya shilingi 20,000 ingawa kila baada ya miaka miwili, lakini kuanzia sasa natangaaza kuifuta ada hiyo,’’alibainisha huku akishangiliwa.




Waziri Haroun akasema, ufutaji huo kwa sasa unawahusu wale watoa msaada wa kisheria wanaojisajili mmoja mmoja, akiwemo msaidizi wa sheria, mavakili, wanasheria na hata mawakili wanaojisajili kama watoa msaada wa sheria.

Upande mwingine, akaweka wazi kuwa hapo baadae, wizara itangaalia uwezekano kuondoa ada hiyo na hata kwa tasisi zinazotoa msaada wa kisheria.

Jingine alilopendekeza Waziri huyo ni kuangalia uwezekano wa kubadilisha neno ‘jukwaa’ na kuangalia jina jingine kama vile baraza la watoa msaada wa kisheria.

‘’Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, tafuteni jina mwafaka la kuita lakini sio ‘jukwaa’ nahisi linaleta tafsiri ya kujibagua, ili mwakani tuwe na jina jingine,’’alipendekeza.

Alienda mbali zaidi Waziri Haroun akaishauri kuwa, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, kuwapeleka ziara za kujifunza wasaidizi wa sheria, ili kuongeza wigo mpana wa kazi zao.

Lakini kabla ya hutuba hiyo, Mkurugenzi wa Idara hiyo Hanifa Ramadhan Said, alisoma maazimio tisa (9) ya jukwaa la tatu, likiwemo kuhakikisha katika jukwaa lijalo, kuwashirikisha washiriki kutoka nje ya Tanzania.

Jingine ni wahusika wa sekta ya sheria kuundwa kikosa kazi na kufanya ushawishi katika uidhinishaji wa bajeti na uingizaji wa fedha, ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya msaada wa kisheria kwa ufanisi zaidi.

Azimio namba tatu ni wizara inayohusika na msaada wa kisheria, kusimamia uandaaji na utekelezaji wa mpango kazi wa pamoja wa watoa huduma msaada za kisheria.

‘’Wahusika wa msaada wa kisheria watahamasisha baadhi ya taasisi kama vyama vya wafanyakazi kuwa na utaratibu wa kutoa huduma za msaada wa kisheria, kwa wanachama wake, na kuweka wataalamu wa sheria katika maeneo yao,’’anafafanua.

Mkurugenzi huyo alitaja azimio jingine kuwa ni, vyama vya Wanasheria na Mawakili, wakishirikiana na wahusika wa msaada wa kisheria watawahamasisha mawakili katika uwakilishi mahakamani.

Skuli ya sheria Zanzibar, itaweka ulazima kwa wanafunzi wanaosomea uwakili, kuvitumia vituo vya msaada wa kisheria, kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo.



‘’Wizara husika ya Katiba na Sheria itaanzisha kanzidata ya kitaifa na mfumo jumuishi wa kidigitali wa ukusanyaji taarifa za msaada wa kisheria, kwa kushirikiana na wahusika wa msaada wa kisheria,’’anaongeza.

Hili ni jukwaa la tatu la msaada wa kisheria, ambapo kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘kuimarisha huduma za msaada wa kisheria zenye ubora na zinazozingatia matokeo’.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch