Skip to main content

LFS, YAWAONESHA NJIA MAAFISA MAWASILIANO WA JUMUIYA ZA WASAIDIZI WA SHERIA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAAFISA mawasiliano na habari wa Jumuia za wasaidizi wa sheria Tanzania zimetakiwa kujenga ushirikiano wa karibu na watendaji wenzao, ili kuhakikisha wanakuwa na mifumo sahihi ya utoaji wa taarifa za jumuia.

Hayo yameelezwa na Mtaalamu wa masoko kutoka LSF Gilsant Mlaseko, wakati akizungumza na maafisa  hao kwenye mkutano wa kujengewa uwezo kwa njia ya kielektroniki.

Alisema bidhaa ya mwasiliano sio haki ya Afisa Mawasiliano na Habari pekee kwenye jumuiya, bali anatakiwa kuwa karibu na wakurugenzi, waratibu na watendaji wengine.

Alieleza kuwa, wakati mwingine ndani ya Jumuiya Afisa huyo anaweza kuwa mwisho katika utoaji wa taarifa na hasa baada ya kuidhinishwa na kuthibitishwa na kamati iliyoteuliwa.

‘’Suala la mawasiliano hasa ya kutoka nje ya Jumuiya, linapaswa watoa taarifa wawe makini na sio jukumu la mtendaji mmoja, bali iwe ni timu ya Jumuiya na kisha muhusika anateuliwa,’’alieleza.

Akieleza umuhimu wa mawasiliano Mtaalamu huyo, alisema ni kuwaonesha wananchi kazi zinazofanywa na Jumuiya, kujenga mustakbali  na mwelekeo wa Jumjuiya pamoja na kuonesha kazi zenu.

‘’Wakati mwingine mawasiliano lazima yaangalie kundi la watu fulani, wakati, aina ya lugha, njia za kuwasiliano nao, eneo husika pamoja na kuhakikisha kupata mrejesho hapo  baadae,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, amwakumbusha Maafisa hao mawasiliano na habari kuwa wanaweza kutumia nji za mawasiliaono kama vile kuandika, kurikodi sauti na picha, vipeperushi, mabango, ujumbe mfupi na picha pekee.

Aidha aliwaeleza maafisa hao mawasiliano na habari, kuwa wanaweza kuitumia mitandao ya kijamii, kuwasilisha taarifa na maelezo yao, kwa jamii ili kupata taarifa kwa haraka.

Aliwanasihi kuwa, katika eneo hilo ni vyema wakawa makini na kujiridhisha kabla ya kuweka taarifa zao, kwani faida yake kubwa ni kuwafikia wengi kwa muda mfupi na ikitokeza kuna mkanganyiko wa taarifa huwafikia wengi.

‘’Mawasiliano ya haraka moja ni eneo la mitandao ya kijamii, iwe face book, twita, Instagram n ahata tovuti na blog, ingawa athari yake kama hakuna taarifa rasmi au ukikosea huwa shida kurudi kwa wafuatiliaji wako,’’alifafanu.

Akijibu baadhi ya mawasiliano, mtendaji wa LSF Victoria Mshana, alizishauri taasisi ziweke utaratibu wa maandishi kutoa taarifa ili kuepusha mkanganyiko kwa wananchi mbali mbali.

Aidha lisema wawe makini namna ya kuchagua majukwaa ya kutoa taarifa na kufikisha ujumbe mahasusi kwa walengwa wa kundi fulani ndani ya jamii au taifa kwa ujumla.

Mmoja wa washiriki hao Abass Famau, alisema mawasiliano ndio kiungo muhimu na cha lazima kwa taasisi kuhakikisha wanakuwa makini wanapowasiliana na wananchi mbali mbali.

‘’Inawezekana kila mmoja anataka aonekane kwenye vyombo vya habari, hivyo mwingine akazungumza hivi na mwingine akazungumza tofauti na mwenzake, na taasisi ikatafsiriwa vyenginevyo,’’alieleza.

Nao Abass Yussuf Makamba, Bahati Issa Jecha na mwenzake Augusta Chasi wamesema, changamoto inayojitokeza ni kwa baadhi ya wakati kutokuwepo kwa mawasiliano na Internet na kusababisha uzoroteshaji wa mawasiliano.

Akiwasilisha kazi za vikundi Shaabani Chande, amesema mafunzo hayo ni muhimu mno kwao, kwani kwa sasa hakuna mtiririko mzuri wa mawasiliano kuanzia ndani ya shirika hadi nje.

Nae Augustino Chipamba, wameomba mafunzo hayo yawe mara kwa mara na kuhakikisha yanakuwa ana kwa ana, ili ufanisi zaidi upatikane kupitia mafunzo hayo.

Kwa upande wake Saleh Juma, alifafanua kuwa mawasiliani ya kielektroniki yanasaidia kuwaunganisha na wafadhili waliono nje sambamba na mafunzo hayo kufanyika kwa njia ya ana kwa ana.

Akiwasilisha mada ya adabu na maadili katika mawasiliano, Afisa Kujengea Uwezo wa Shirika la Legal Service Facility LSF Victoria Mshana, amesema mawasiliano yenye heshima, nidhamu na adabu ni muhimu kwa pande zote.

                                       Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch