Skip to main content

KUMBE LUGHA CHAFU, KEJELI, UBAGUZI, KUITANA MAJINA MABAYA NI UDHALILISHAJI UNAOPUUZIWA

 



NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@

BINAADAMU tumeumbwa na hulika tofauti katika kulipokea jambo na kuishi nalo.

Wapo ambao wanaoweza kukabiliana na taarifa mbaya na bila kuchukua uamuzi mgumu, na wapo ambao mioyo yao haina uwezo kulipokea jambo baya na kuishi nao.

Uwezo wa kupokea taarifa mbaya na nzuri, unaweza kujengwa na kuharibiwa kwa kutumia udhalilishaji wa akili unao fanywa na maneno yanayo weza kutamkwa kwa mtu fulani.

Leo hii kwenye jamii zetu, tunaona aina hii ya udhalilishaji wa maneno umeshamiri kwa kiasi kikubwa, ni aina ya udhalilishaji unaofanywa sana na jamii zetu na kwenye shughuli mbali mbali za kijamii.

Ni kawaida sana kKwa jamii zetu kumuona mama mzazi, akimtusi mtoto wake bila kujua kuwa huo ni udhalilishaji wa maneno, kwa maana unaweza kumuathiri mtoto taratibu kiakili.

 Mwanasaikolojia kutoka hospital ya Kidogo Chekundu Hamida Naufaul Kassim, amesema udhalilishaji wa maneno, umepelekea waathirika wengi kuchukua hatua ya kujiua.

Au wengine kuingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya na wengine hujenga chuki dhidi ya jamii nzima.

"Aina hii ya udhalilishaji umefanya watu wengi hasa mabinti kushindwa kufanya shughuri zao za kiuchumi, kwa kuogopa kufanyiwa vitendo hivi vya udhalilishaji, kwa kutolewa lugha za matusi na hata kuitwa majina yasiofaa.

Anasema kumeza dawa, kujitupa husababishwa na vitu mbalimbali ikiwemo kutoweza kukabiliana na matatizo, ikiwemo maneno makali, mfumo wa ubongo kutofanya kazi uzuri pamoja na kupata magonjwa yasiotarajiwa.

Akaenda mbali zaidi kuwa, mtu anayetumia dawa za kulevya, anaweza kupata athari mbali mbali, ikiwemo kupata magonjwa ya kimwili, kuharibu mfumo wa kupumua na ugonjwa wa akili pamoja na kutokubalika katika jamii.

Asia Hassan Juma (sio jina lake kamili) mwenye miaka 23 ambae ni ulemavu wa uwoni, anasema changamoto mbalimbali ambazo anakutana nazo kutokana na ubaguzi anaokutana nao katika gari za abiria.

‘’Makonda wa dalala wanatabia ya ubaguzi, kwani wakimuona mtu mwenye ulemavu wa uwoni, hawakubali kupanda gari peke yake hadi afuatane na mwezake, jambo ambalo linanikera  katika maisha yangu,’’anasema.

Anasema udhalilishaji mwingine wa maneno ni kuitwa vipofu, wapiga deki na mwendo wa bata jambo ambalo linamfanya ajitenge na wakati mwengine ashindwe kuchangia mada.

Kwa upande wa mtoto Asha Mtumwa wa Vikokotoni, anasema baadhi ya wazazi wanatabia ya kuwatolea maneno makali watoto wao, hadi kuwakatisha tamaa, na kusababisha kuchukua hatua mikononi mwake.

" Nishawahi kugombwa na mama yangu, kunitolea maneno makali na kunikatisha tamaa, nilipatwa na hasira nikamua kuchukua uwamizi wa kumeza dawa, nashukuru jirani yangu alikuwepo na kunichukua kunipeleka hospitali,’’anasema .

Mkuu wa Dawati la Jinsia ya Watoto Inspector Mohamed Mwadini Kificho, anasema wazazi wanatabia ya kuita watoto wao majina makali na kuaza kumuathiri, jina hilo pamoja na kufanya ubaguzi katika malezi ikiwemo kisaikolojia

Anaona jamii haina uwelewa wa kutosha, na ndio maana wale wanaotolewa maneno machafu au ya kukatishwa tamaa, hayaripotiwi sana kuliko matokeo ya ukatili na udhalilishaji ikiwemo ubakaji.

Akawataka wazazi na walezi kutumia lugha nzuri zenye kuleta maendeleo ya mabadiliko ya mtoto wake, ikiwemo kutekeleza yale anayo ambiwa na kuacha anayokatazwa.

‘’Wanaotolewa lugha za vitisho, ukatili, udhalilishaji, matusi ni sehemu ya udhalilishaji, waripoti wanapoona hali hiyo, kwani ni kosa kisheria,’’anafafanua.

Hapa Mkurugezi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Siti Abasi Ali anasema wanatoa elimu mbali mbali katika kila shehia, kwa lengo la kuondoa udhalilishaji pamoja na baguzi, wasisahau kutaja lugha chafu kuwa ni udhalilishaji.



"Tunawaita masheha tunawapa elimu kuhusina na kupiga vita vitendo vya udhalilishaji pamoja na ubaguzi ikiwemo kumtolea mtoto maneno machafu, kuwaita majina mabaya watu wenye ulemavu,’’anabainisha.

Anasema ili kuhakikisha jamii inaelewa kuwa hata lugha chafu ni udhalilishaji, wamekuwa wakitoa elimu katika sehemu mbali mbali ikiwemo skuli na madrassa kwa ajili kumlinda mtoto katika vitendo vya udhalilishaji.

"Tunatoa elimu hadi kwenye vijiwe vya vijana, baraza za wazee, skulini,  kwa lengo la kuwapa nasaha, kutumia kauli sahihi kwa watoto, ili kuweka mlingano sawa ndani ya jamii,’’anafafanua.

Anasema wanapinga vikali kwa baadhi ya waalimu kuwazomewa, kuwaita majina yanayoashiria ufahamu wa akili yake wanafunzi wasiofanya vizuri madarasani, kwani njia hiyo ni udhalilishaji.

Hakuna njia ya kumrekebisha mwanafunzi kwa njia ya kumzomea ama kumuita majina kama ya kizota, nanga, mburura bero, kwamba mitihani ijayo anaweza kufanya vizuri.

Suala la udhalilishaji linahusu pia kada ya sheria, ambayo kupitia kwao haki hutarajiwa kupatikana, kama inavyofanya juhudi Jumuiya ya Wanasheria Wanawake ya Zanzibar (ZAFELA).

Yenyewe iko mbele katika kushiriki kupambana na uovu huu, hivyo Mwanasheria wake, Time Hassan anasema serikali zote mbili zimeweka mazingira mazuri ya kumlinda mtoto.

Kwa Zanzibar, ipo sheria maarufu nambari 6 ya mwaka 2011, iliyoanzisha mahakama maalumu ya kushughulikia makosa ya watoto, na moja ya kosa ambalo linapingwa ni kumdhalilisha mtoto kimaneno.

Hata sheria ya Kanuni ya Adhabu nambari 7 ya mwaka 2018, inayoeleza adhabu kwa makosa yanayohusiana na maadili, kama vile ubakaji, kulawiti, kuingilia kinyume na maumbile na shambulio la aibu.

Ipo sheria ya Mahkama ya Kadhi nambari 9 ya mwaka 2017, iliyoundwa ili kusimamia masuala ya ndoa pamoja na maslahi bora ya watoto, pale inapotokea kutelekezwa na kukosa haki zao za msingi ikiwemo elimu.

 Anafafanua kuwa, jamii ndio tiba ya kwanza, ya tatizo hili la udhalilishaji  wa maneno, maana mzizi wa tatizo hili huanzia kwenye ngazi familia na kisha kusambaa mpaka nje kwenye jamii nzima.

Mzazi Aisha Haji Mkema wa Magomeni, anasema lazima jamii ishirikiane kupinga vita lugha za udhalilishaji kwenye familia, maana ndio kwenye chanzo kikubwa.

Sheikh Said Ahmada kutoka Ofisi ya Mufti Pemba, anase,a dini ya kiislamu inakataza kuitana majina mabaya pamoja na kutumia lugha za udhalilishaji kama vile mzinifu na mlawitiwa.

‘’Uislamu unataka jamii itumia lugha za kiutu, kiungwana, amani na salama hata kama kuna mtu amekutikana na kosa mpaka pale mamla zitakapodhihirisha kosa husika,’’anafafanua.

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema lugha za kibaguzi, udhalilishaji na zinazokiuka haki za binaadamu huwaathiri wanawake na watoto.



‘’Wakati mwingine hata kipindi cha kampeni, wagombea wanawake hufufuliwa makosa yao na kutangaazwa hadharani, au wakati mwingine baadhi ya wazazi kuwapa majina mabaya watoto wao waliofanya makosa ya kijamii,’’anasema.

Hakimu wa Mahkma maalum ya kupambana na udhalilishaji mkoa wa kaskazini Pemba Muumini Ali Juma, anasema zipo kesi chache mno, zinazoripotiwa zikihusisha lugha za udhalilishaji ama vitisho.

‘’Inaonekana jamii haina mwamko mkubwa wa kuripotia kosa la lugha za udhalilishaji, na wanadhani kama vile sio kosa la jinai, na pengine elimu inahitajika,’’anafafanua.

Mwalimu mkuu wa skuli ya sekondari ya Connecting Continent ya Mgogoni Chake Chake Pemb, Mwache Juma Abdalla, anasema kama waalimu watakuwa na utamaduni kuwapa majina ya ubaguzi na udhalilishaji wanafunzi wanaopata alama za chini, wanaweza kuporomosha uwezo wao.

‘’Lazima sisi waalimu tutumie lugha bembelezi, rafiki, laini, shawishi na yenye kumuhamasisha mwanafunzi kupenda kusoma na sio zile za kumkatisha tamaa au udhalilishaji,’’anashauri.

Mjumbe wa Umoja wa Watu wenye Ulembau UWZ Pemba Hidaya Mjaka Ali na Asia Iddi Mahamoud mwenye ulemavu wa viuongo, amevishauri vyombo vya kusimamia haki, kutoa elimu ya athari za kuwaita majina mabaya.

                                     mwisho

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch