Skip to main content

WATIA NIA UBUNGE, UWAKILISHI CCM PEMBA WANAWAKE 71 KATI YA 270

 

NA WAANDISHI WETU, PEMBA@@@@

WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi CCM, 270 wakiwemo wanawake 71 na wanaume 199, wamejitokeza kuomba nafasi za Ubunge na Uwakilishi katika majimbo 18 kisiwani Pemba.

 

Kati hao 270, walioomba nafasi ya Ubunge wote walikuwa ni 147, kati ya hao wanawake ni 40 na wanaume 107, huku kwa nafasi ya Uwakilishi wote waliomba ni 123, wakiwemo wanawake 31 na wanaume 92.

 

Waandishi wa shirika la Magazeti ya serikali ambao walifika ofisi za CCM za wilaya za Micheweni, Wete, Mkoani na Chake chake, walibaini kuwa, wilaya ambayo wanawake walijitokeza kwa wingi ni wilaya za Micheweni na Mkoani ziliokuwa na watia nia idadi sawa ya 19 kwa nafasi ya Ubunge na Uwakilishi kila wilaya.

 

Wilaya iliyoshika nafasi ya tatu kwa wanawake wa CCM kujitokeza kwa wingi ni wilaya za Wete, iliyoibua wanawake 17, huku wilaya ya Chake chake ikishika nafasi nne kwa watia nia 16.



Aidha wilaya ambayo wanawake waliojitokeza kwa wingi kwa nafasi ya Ubunge ni wilaya ya Micheweni, lililoibua wanatia 11, ambapo hapo wapo wanaume ni 17, kutoka katika majimbo tofauti.

 

Kwa upande wa wilaya hiyo, watia nia wote kwa nafasi ya uwakilishi ni 25, ambapo wanawake ni wanane, huku wanaume wakiwa 17.

 

Wilaya ya Mkoani, yenyewe kwa watia nia ya ubunge ni 41, kati yao wanawake ni tisa na wanaume 32, samba mba na idadi ya 31, wakiwemo wanawake 10 na wanaume 21.

 

Kwa upande wa wilaya ya Chake chake, wapo watia nia 51, kwa nafasi ya ubunge wanawake wakiwa 12 na wanaume 39, huku kwa uwakilishi wakiwa 23 wanawake wanne na wanaume 19.

 

Kwa mujibu wa taarifa, wilaya ya Wete ilikuwa na watia nia 44 kwa nafasi ya uwakilishi, wanawake wakiwa tisa na wanaume 35, huku kwa ubunge wakiwa 27, ambapo wanawake ni wanane na wanaume 19.

 


Katibu wa CCM wilya ya Wete Rished Omar Khalfan aliwataka watia nia wote kuwa watulivu katika kipindi hichi, cha kusubiri mamuzi ya ngazi ya juu ya chama.

 

“Watia nia endeleeni kuwa watulivu ili taratibu za chama zifanyike na kuwarejesha wagombea watatu ambao hao watajinadi na kisha kupigiwa kura na wajumbe,”alisema.

 


Naye katibu wa CCM mkoa wa kusini Pemba Kajoro Vyohoroka aliwataka, watia nia kuto jipitisha pitisha kwa wajumbe, kwani wakati wa kufanya hivyo kwa sasa bao.

 

Zoezi la uchukuwaji wa fomu kwa watia nia kwa nafasi wa CCM mbali mbali, lilianza Juni 28 na kumalizika Julai 2 mwaka huu nchi nzima.

 

                MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...