Skip to main content

TUME YA UTAANGAZAJI YAWAPA 'DILI' WAMILIKI WA REDIO

 

NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


TUME ya Utangaazaji Zanzibar ‘TUZ’, imewataka wasimamizi na wamiliki wa vituo vya redio nchini, kukubali kubadilika kwa haraka, na kutoka mfumo wa sasa wa kidijitali na kuacha mafumo wa zamani wa analogia, kwani jamii imehamia huko.

 

Hayo yameelezwa jana, na Afisa kutoka Tume hiyo Zanzibar, Abubakar Mohamed Chwaya, alipokuwa akitowa mafunzo kwa wadau wa  vituo vya radio katika ukumbi wa Shirika la Utaanzaji Zanzibar ‘ZBC’ Mkoroshoni Chake chake Pemba.

 

Alisema mfumo mpya wa kisasa ‘digital’ utawawezesha wasambazaji hao, kurahisisha kuondosha muingiliano ya miundo mbinu ya sauti na  kazi zao, baina ya kituo kimoja na chingine.


Alieleza kuwa, kutumia mfumo huo utaondosha matumizi makubwa ya gharama katika urushaji wa maudhui ‘content’ na utarahisha na matumizi madogo ya miundombinu.



"Mfumo mpya wa kisasa ya kidigitali, utawawezesha wasikilizaji wako, kujua mapema kupitia kioo cha radio kupata kujua jina la radio, pamoja na kujua masafa yako yaani ‘frequency, "alifafanua.


Afisa huyo alifahamisha kuwa, chombo chochote kitafanya kazi kwa mujibu wa sheria, na Tume itaendelea kusimamia na kufuatilia kazi zao, ili kuhakikisha hakuna uvunjifu wa maadili.

 

 Alisema kuwa hawatolazimishwa sana kutumia mfumo mpya wa kisasa ‘digital’ kutokana na miundo mbinu yao, lakini pia mwenye uwezo wa kutumia mfumo wake wa zamani hatokatazwa.

 


Kwa upande wake Issa Suleiman Othman kutoka Tume hiyo, alisema kupitia mfumo mpya wa kisasa, itapelekea kuchakatwa kwa sauti, katika mfumo ulio bora na mzuri na kumrahisishia msikilizaji kufaidika.


Alisema kuwa kupitia mfumo huo, utapelekea madhui na dhamira ya chombo chochote kufikia, mbali na kuwa ni rahisi kuwafikia wasikilizaji wao.


Alifafanua kuwa changamoto nyingi zinazojitokeza kupitia mfumo wa ‘FM’ ina gharama kubwa na masafa marefu ya kusafirishia mawimbi ya sauti.


Mratibu kutoka Tume ya Utangazaji Pemba Adam Ramadhan Kombo, aliwataka wadau wa vyombo vya Radio, kuwa ipo haja ya kubadilika pamoja na kwenda na wakati, ili kurahisisha kazi zao.


Alisema ni wajibu wao kuwaelimisha kutoka katika mfumo wa zamani kuingia katika mfumo wa kisasa, ili kuingia katika kasi mpya itakayoleta maendeleo kwa wasikilizaji.



Nao wadau wa vyombo hivyo, ameipongeza Tume ya Utangazaji kwa kuiondoshea gharama kubwa za kiutendaji wao kwani, Tume hiyo imekuwa ikileta msaada mkubwa kwa wadau hao.


Aliongezea kusema kuwa, kupitia mfumo huo ipo haja ya kueka gharama ndogo za ulipaji wa mfumo huo, kupitia leseni zao.

 
 MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...