Skip to main content

UWT YAWAALIKA WANAWAKE KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA

 



BAKARI KHAMIS NA MOZA SHAABAN, PEMBA

MAKAMu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainab Khamis Shomari, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni.

Aliyasema hayo ofisi ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya Mkoa iliyopo Chake chake kisiwani Pemba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea zoezi la uchukuaji wa fomu za lililoanza janaJuni 28.

Alisema ni vyema wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo, kutokana na kuwepo kwa mazingira rafiki yanayowawezesha, kushiriki zoezi hilo bila kikwazo chochote.

Alisema ushiriki wa wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni miongoni mwa matakwa ya ilani ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’, ambacho kipo madarakani, ambayo imeeleza kipaumbelechake cha uwepo wa wawakilishi wanawake kwa asilimia 50 katika vyombo vya kutunga sheria.

Alieleza kwamba Umoja wa Wanawake Tanzania, umekua ukifanya jitihada mbali mbali katika kulitimiza takwa hilo, ikiwemo kufanya hamasa kwa wanawake kugombea nafasi hizo kwa kuwajengea uwezo na kuwaungamkono.

"Sisi ‘UWT’ tumekua tukifanya jitihada mbali mbali katika kuhamasisha wanawake kushiriki katika kugombea nafasi za uongozi, pamoja na kuwaungamkono wale waliohamasika ili tupate kwa vitendo ile asilimia 50 kwa 50, tunayoitaka ya  wawakilishi wanawake,"alieleza.

Alisema kwasasa wanawake wamekua wakifanya vizuri kiungozi, pale wanapopata nafasi mbali mbali ya kutumikia taifa, kutokana na uwezo wa kisaikolojia walionao.

Aliongeza kua kwa mara ya kwanza, Tanzania inatarajia kuandika historia ya kua na Raisi mwanamke, atakaepatikana kwa kupigiwa kura na wananchi, hivyo ni vyema kwa wanawake wingine, kuungamkono azimio hilo kwa kujitokeza katika kuchukua fomu za kugombea.

Alisema UWT imejipanga kutoa ushirikiano kwa wanawake katika kugombea nafasi hizo, huku akiwaomba wanaume kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wanawake, kwa kuwashajiisha na kuwapa moyo.

" Tunataka kuuthibitishia umma kwamba, dhana ya adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake sio sahihi, hivyo sisi UWT tutahakikisha tunawaungamkono wanawake watakaojitokeza kuchukua fomu za kugombea na wanaume tunaomba muunge mkono hili,"alifafanua.

Hata hivyo Makamu huyo Mwenyekiti wa UWT, aliwataka wanawake bila kujali itikadi za vyama vyao, waache kuwa maadui kwa wanawake wenzao.

Wakati huo huo, amevitaka vyombo vya habari kutumia vizuri kalamu zao, juu ya kushajiisha wananchi kuhusu  umuhimu wa kutunza amani iliopo nchini.

Awali akizungumza hivi karibuni, kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi, amewakumbusha wananchi, kuwachagua viongozi wenye nia ya kuwaletea maendeleo.

Zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, limeanza jana likitarajiwa kumalizika Julai 2, mwaka huu majira ya saa 10:00 jioni.

 

                                                         MWISHO

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...