Skip to main content

MZEE 'SODA' MIAKA 76, ATUNDIKWA MIAKA 10 CHUO CHA MAFUNZO KWA UBAKAJI PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

HATIMAE mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji Mkoa wa kusini Pemba, imemswekwa chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 10, mshitakiwa Khamis Juma Chumu ‘soda’ (76) mkaazi wa Mtoni Chake Chake, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 13.

 

Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, alisema kati ya adhabu hiyo, mshtakiwa atatumikia chuo cha mafunzo miaka 10 kwa kosa la ubakaji wa mtoto huyo.

 

Akisoma hukumu hiyo, alisema upande wa mashtaka ulifanikiwa kuwasilisha mashahidi watano kwenye kesi hiyo, akiwemo mtoto mwenyewe, ambae alitosha kwa kiwango kikubwa, ushahidi wake kuishawishi mahakama.

 

Alisema, mtoto ndio shahidi mkuu anayepaswa kuihakikishia mahakama kuwa, alibakwa na kutorosha ama laa, na sio mtu mwengine yeyote.

 

Hakimu huyo akiendelea kusoma hukumu hiyo alisema, wakati mtoto huyo wa miaka 13 anatoa ushahidi wake mahakamani hapo, akiongozwa na wakili wa serikali Ali Amour Makame, alieleza kwa kina, namna alivyobakwa na mzee ‘soda’.

 

Alisema katika ushahidi wake kuwa, kwanza aliitwa ndani ya babu huyo, kwa lengo la kumtuma dukani, ingawa kumbe dhamira ilikuwa ni kumbaka.

 

Mtoto huyo alisema, alitii agizo la kwenda ndani ya nyumba anayoishi mzee huyo, kwani ni mtu aliyemzoea na hakuwa na wasi wasi wowote.

 


‘’Alinibaka juu ya kitanda anacholala na kisha alivaa taula baada ya kuniabaka babu Khamis soda (mshitakiwa),’’ndivyo hakimu alivyonukuu sehemu ya ushahidi mkuu wa mtoto huyo.

 

Hata hivyo Hakimu Muumini Ali Juma, alisema hata ushahidi wa askari mpelelezi wa kituo cha Polisi Madungu Chake chake, ulikuja kuunga mkono ushahidi wa mtoto huyo, na haukuacha chembe cha shaka.

 

 Katika hatua nyingine Hakimu huyo alisema, ushahidi wa upande wa utetezi, haukuvuruga wala kutia doa ushahidi uliowasilishwa wa upande wa mashtaka.

 

Kabla ya hukumu hiyo, wakili wa utetezi Abied Mussa Omar, aliomba mahakama hiyo kuzingatia umri wa mzee huyo, na kumpunguzia adhabu.

 

Alisema mzee huyo, anafaa kupunguziwa adhabu kwanza umri wake, pili bado anayofamilia kubwa inayomtegemea, ili kuiendeleza kihuduma.

 

Ingawa upande wa mashataka uliokuwa ukiongozwa na wakili wa serikali Ali Amour Makame, aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali, kwa mshtakiwa huyo.

 

‘’Makosa haya kwa watoto sasa yamekuwa janga, ndani ya jamii, hivyo sasa tayari kila upande umeshatekeleza wajibu wake, ni kazi ya mahakama kutoa adhabu kwa mujibu wa sheria,’’aliomba. 

 

Awali ilibainika mahakamani hapo kuwa, mtuhumiwa huyo Khamis Juma Chumu ‘soda’ (76) mkaazi wa Mtoni wilaya ya Chake chake, alimtorosha mtoto wa kike miaka 13, wakati akienda kuchota maji mferejini, na kumpeleka nyumbani kwake.

 

Kufanya hivyo ni kosa, kinyume na kifungu 113 (1) (a) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

 

Kosa la pili ni la ubakaji, ambalo alilifanya Mei 15, mwaka huu, ambapo alimmbaka mtoto huyo ndani ya nyumba anayoishi majira ya saa 4:15 asubuhi, eneo la Mtoni wilaya ya Chake chake.  

 

Kufanya hivyo ni kinyume, na kifungu 108 (1), (2) (e) na kifungu cha 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

                Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...