Skip to main content

KONGAMANO SIKU 16: ZLSC CHASIKITISHWA BABA, WAJOMBA KUWABAKA WATOTO WAO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kimesikitishwa na kitendo cha baadhi ya baba wazazi, walezi na waalimu wa madrassa, kuwafanyia vitendo vya ukatili na udhalilishaji watoto walio na mamlaka nao.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Kituo hicho Harusi Miraji Mpatani, kwenye maelezo yake yaliotolewa na Mratibu wa kituo hicho Pemba Safia Salehe Sultan, kwenye kongamano la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili, lililofanyika Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake.

Mkurugenzi huyo alisema, katika utafiti wa miezi tisa, uliofanywa na Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, watu 182 walifanyia usaili ili kupata taarifa hizo.



Alisema, kati ya watu hao wanawake 115 na wanaume walifikiwa 67 kutoka kisiwa cha Unguja na Pemba, ambapo moja ya malengo ya utafiti huo ni kufichua kesi zilizo jificha kutokana na muhali na mkwamo katika ngazi za chini mpaka kufikia muafaka wa kesi husika.

 

Alieleza kuwa, ameshtushwa na kubainika kwa baba wazazi 13, waliowafanyia ubakaji watoto wao wa kuwazaa, ambapo kati ya hao tisa (9) Unguja na watatu (3) wakiripotiwa kisiwani Pemba.

 

Mkurugenzi Harusi alieleza kuwa, jengine ambalo ZLSC katika siku hizi 16 za kupinga ukatili linawasikilitisha ni kuwepo kwa akina baba walezi na kambo 25, Unguja wakiwepo 13 na Pemba 12 waliowaba watoto wao wa kuwalea.

 


‘’Elimu inatolewa na serikali na hasa tasisi ZLSC, ZFELA na TAMWA na nyingine, lakini sasa ninapoona matokea ya utafiti huu wa miezi tisa uliofanywa na wenzetu TAMWA, inauma sana,’’alisema Mkurugenzi.

 

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo wa ZLSC ameendelea kuitahadharisha jamii, kuwatumia wanganga wa tiba za asili ambao, kwani baadhi yao hukosa uaminifu wakati wanapoendesha tiba zao.

 

‘’Hata kwenye utafiti huu, jumla ya matukio 10 ya udhalilishaji yaliripotiwa kufanywa na waganga wa kienyeji, ambapo Unguja yalikuwa sita (6) na Pemba manne (4), wakifanyiwa watoto,’’alieleza.

 



Aidha Mkurugenzi huyo wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC Harusi Miraji Mpatani, amewatadharisha wasaidizi wa sharia waliomo majimboni, kutojiingiza kwenye sulhu ya kesi hizo.

 

Mratibu wa ZLSC Pemba Safia Saleh Sultan, alisema Kituo kitaendelea kutoa elimu ya umuhimu wa kufika mahakamani kutoa ushahidi, ili jamii ionea faida.

 

‘’Mahakama inawategemea wananchi waliosikia, kuona au kuambiwa jambo wafike mahakamani kutoa ushahidi, sasa kama bado wanakimbia, hakuna kesi itakayotiwa hatiani,’’alieleza.

 

Hata hivyo Mratibu huyo, aliendelea kuisisitiza jamii kuzitumia siku 16 za ukatili, ili kujua wajibu wao hasa yanapotokezea matendo hayo, ndani ya jamii husika.

 




Kwenye kongamano hilo Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji Muumii Ali Juma, alisema wakati umefika sasa kwa jamii kufanya uamuzi wa kuyatokomeza matendo hayo.

Akifungua kongamano hilo, Msaidizi Kamishna wa Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba Cyprian Mushi, alisema kila mmoja akitekeleza wajibu wake, matendo hayo yatakoma.

Mwenyikiti wa kamati ya kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji Nassor Bilali Ali, alisema lazima jamii ikae chini na kufikiria upya, suala la kuwa na malezi ya ushirikiano.

Alieleza kuwa, kama yapo mambo jamii wanashirikiana mfano harusi, msiba na hivyo hivyo utamaduni huo uhamishiwe kwenye malezi ya pamoja.

Wakichangia kwenye kongamano hilo, washiriki hao akiwemo sheikh Abdalla Nassor Mauli, alilipongeza Jeshi la Polisi, kwa kubadilika katika utendaji wao wa kazi.

Nae Fatma Maulid Kassim kutoka kituo cha mkono kwa mkono wilaya ya Chake chake, alipendekeza kuwa, kama wapo wazazi, walezi na watu wengine wanakataa kutoa ushahidi, sheria ichukue nafasi yake.

‘’Hiwezekani serikali na wanaharakati hawalali usiku na mchana katika mapambano ya ukatili na udhalilishaji, kisha mwengine anaejua kila jambo, ashindwe kuvisaidia vyombo vya sheria,’’alieleza.

Kongamano hilo, ni sehemu ya shamra shamra za kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, ambapo makongamano kama hayo yamefanyika wilaya zote za Pemba.

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ambacho kimeanzishwa mwaka 1992, malengo yake makuu ni pamoja na kutoa msaada wa kisheria, kwa wazanzibar bila malipo, ushauri, na elimu ya kisheria kwa watu hasa maskini.

                                         Mwisho  

 

 

                                       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch