Skip to main content

VIZIWI PEMBA WATAKA ELIMU YA UKIMWI KUWE NA WAKALIMANI

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA

WATU wenye ulemavu uziwi kisiwani Pemba, wameomba kuwekewa wakalimani wa lugha ya alama, kila aina ya kipindi au taarifa yoyote, inayohusu elimu ya Ukimwi, ili iwe rahisi kwao kufuatilia kwa ukaribu.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kuelekea siku ya Ukimwi duniani Disemba 1, walisema bado elimu ya kujikinga na vurusi vya ukimwi kwa kundi lao, hijawafikia vizuri.

 

Walisema, tume za Ukimwi ile ya Zanzibar na ya Tanzania bara, hazijaweka kipaumbele juu ya kuweka wakalimani wanaporushwa vipindi, juu ya masuala ya Ukimwi.

 

Mmoja kati ya viziwi hao, Omar Khamis Juma wa Ole, alisema wanakosa elimu kubwa ya kujikinga ama mapambano ya virusi vipya ya Ukimwi, kutokana na kuachwa nyuma.

 

Alieleza kuwa, ijapokuwa kupitia shirika la Utangaazaji Zanzibar ‘ZBC’ kuna baadhi ya vipindi kunawekwa wakalimani, lakini bado sio vipindi vyote.

 

‘’Tunataka kila kipindi, hutuba, tangaazo au wito unaogusa suala la Ukimwi, VVU, unyanyapaa au dawa za kufubaza maisha ARVs basi, kuweko na makalimani ili, kupata elimu hiyo kwa upana,’’alieleza.

 

Khadija Mcha Haji wa Kangagani wilaya ya Wete, alisema hata kwenye makongamano, mikutano na hata kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi, hakujazingatiwa uwepo wa mkalimani.

 

‘’Elimu ya Ukimwi, sisi viziwi kwetu ni shida mno, maana hakuna wakalimani wa lugha yetu ya amala, sasa inakuwa vigumu, kuwa na taarifa kwa upana,’’alieleza.

 

Nae mtoto mweye uziwi Sara Issa Khamis wa Machomane Chake chake, alisema kwa wao wanaoishi kando ya mji, wamekuwa hata mara moja moja, hukosa kuona ukalimani wa elimu ya Ukimwi.

 

Hivi karibuni akizungumza kuelekea siku ya wakalimani, Katibu Mkuu wa jumuia ya wakalimani wa lugha ya alama Zanzibar ’JUWALAZA’ Kheir Mohamed Siamai, aliitaka jamii, kujiunga na jumuiya hiyo, ili kujifunza lugha ya alama, ili kukidhi haki ya mawasiliano, kwa watu wenye ulemavu wa uziwi.

 

Alisema, bado jamii haijaona umuhimu, wa kujifunza lugha ya alama, na kuwasaidia viziwi katika mawalisiliano, hasa juu ya kujikinga na maradhi, kadhaa ukiwemo Ukimwi.

 

Alifahamisha kuwa, kundi la viziwi katika jamii ni sawa na kundi jengine lolote, ambalo linahaki ya kuwasiliana baina yao na kundi jengine, ingawa wao ni kwa kutumia lugha ya alama.

 

‘’Mawasiliano ya viziwa ni maalum, hivyo kila mmoja ana haki ya kuhakikisha anawasiliana nao, ili kutumiza utu na ubinadamu, lakini jambo la kwanza ni kujifunza lugha ya alama,’’alieleza.

 

Kwa upande wake Mjumbe wa Jumuiya hiyo kisiwani Pemba, Asha Suleiman alisema, bado lazima mkazo uwekwe na serikali katika kuona kundi hilo, linapata elimu ya masuala mbali mbali ukiwemo Ukimwi na njia za kujiepusha.

 

Afisa Mdhamini wizara ya Makamu wa Kwanza rais Pemba Ahmed Abubakar Mohamed, amesema marekebisho yajayo ya sheria ya watu wenye ulemavu, yanatarajiwa kulazimisha uwepo wa wakalimani kwa vipindi vyote.

 

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu Ibara ya 21 (b) inaeleza kuwezesha matumizi ya lugha ya alama, maandishi ya braille kuongoza na kuweka mawasiliano mbadala kwa njia nyingine na mfumo wa mawasiliano watakaoamua.

 

Aidha sheria nambari 9 ya mwaka 2016 ya haki na fursa ya watu wenye ulemavu Zanzibar kifungu cha 15, ni lazima mawasiliano kwa watu wenye ulemavu utolewe kwa njia mbali mbali, ikiwemo la nukta nundu na lugha ya alama.

                            mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch