Skip to main content

AANGUKA GHAFLA MAHAKAMANI HAKIMU AKIJITAYARISHA KUMSOMEA HUKUMU

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MTUHUMIWA wa ubakaji Mohamed Ali Hassan miaka 19, aliyekataa kusomewa hukumu yake Novemba 21, mwaka huu kwa madai ya kuuguliwa na mzazi wake, juzi tena Novemba 24, mahakama imeshindwa kumsomea, baada ya kuanguka ghafla mahakamani hapo.

 

Mtuhumiwa huyo, alifika mahakamani hapo akiwa mzima, hadi ilipofika wakati wake aliitwa na kupanda juu ya kizimba cha mahakama ya makosa maaluma ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba, ili kusubiri kusomewa hukumu yake.

 

Wakati Hakimu Muumini Ali Juma wa mahakama hiyo, akijitayarisha kuweka mambo sawa na mtuhumiwa huyo akiwa tulia kuangali kinachoendelea, ndipo ghafla alipoanguka.

 

Mtuhumiwa huyo alianza kuelezea kuwa hali yake imeshabadilika ghafla, huku akilalamikia maumivu jambo ambalo liliishughulisha mahakama.

 

‘’Mheshimiwa Hakimu, kwa hakika hali ya afya yangu imeshaharibika na sijiskilii, huku akishikilia baadhi ya viungo vyake, akielezea kupata maumivu makali,’’alilalamikia.

 

Kisha mtuhumiwa huyo, aliangua hadi chini mahakamani hapo, na sasa ikawa kazi kwa baadhi ya waliokuja kusikiliza kesi na watendaji wa mahakama, kumsaidia kumpeleka hospitali ya Chake chake kwa matibabu.

 

Hivyo Mahakama hiyo kwa juzi Novemba 24 mwaka huu, kwa mara ya pili, imeshindwa kumsomea hukumu mtuhumiwa huyo, ambae Novemba 21, pia alikataa kusomewa kwa madai ya kuumiliwa na mzazi wake na yeye mwenyewe.

 

Hivyo Hakimu Muumini Ali Juma, alimtaka mtuhumiwa huyo ambae yuko nje kwa dhamana, kwenda kuhangaikia matibabu na amemtaka arudi tena mahakamani hapo siku tatu zijazo mwaka huu, kwa ajili ya kusomewa hukumu yake.

 


‘’Pamoja na mitihani na dharura unazozipata hapa mahakamani na nje ya mahakama, bado mahakama inakumbuka kuwa imefikia hatua ya hukumu, sasa kwanza katibiwe lakini Novemba 30 uje ili tuendelee,’’alisema Hakimu Muumini.

 

Awali Mwendesha mashataka wa serikali Ali Amour Makame, alimueleza hakimu wa mahakama hiyo kuwa, shauri hilo lipo kwa ajili ya hukumu.

 

Alidai kuwa, baada ya upande wao kufunga ushahidi na mtuhumiwa kujitetea, nae kufunga ushahidi, juzi Novemba 24, mwaka huu, ilikuwa ni siku yake ya kusomewa hukumu.

 

Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, kijana huyo bila ya halali na bila ya ridhaa ya wazazi wa mtoto wa kike, alimbaka mtoto huyo mwenye miaka 16, akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa.

 

Alidai kuwa, siku hiyo mtuhumiwa alimuingilia mtoto huyo katika mwaka 2019, majira ya mchana, jambo ambalo ni kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na kifungu cha 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

(kumradhi: Picha iliyotumima sio halisi)

 

                Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch