Skip to main content

WIZARA YA HABARI, MKANDARASI WALIFELISHA ENEO KISHINDENI UJENZI UWANJA WA SOKA PEMBA

                                               

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@

WIZARA ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, imeshauriana na kukubaliana na kampuni ya Reform spots, kwamba sasa uwanja wa mpira wa mkoa wa kaskazini Pemba, uhamishiwe eneo la Kinyikani, badala ya Kishindeni.

Hayo yalifahiamika jana, kwenye ziara ya Waziri wa huyo, Riziki Pembe Juma na Katib Mkuu wake Mattar Zahor Massoud, baada ya kutembelea ujenzi unaozorota wa uwanja wa mkoa huo, eneo la Kishindeni.

Akiwa eneo hilo, Waziri huyo na ujumbe wake, walieleza kushangaazwa kwao, na kuzorota kwa ujenzi wa uwanja huo.

Waziri Pembe, alisema haiwezekani uwanja huo kuwenda mwendo wa kusuasua ujenzi wake, ingawa baada ya kuelezwa sababu, alishauri kuhamishiwa ujenzi wake.

Alisema, kama inawezekana, kusiwe na gharama za nyongeza kwa ujenzi wa eneo la Kishindeni, kutokana na uwepo wa hatarishi ya eneo hilo kuvamiwa na maji.

Alifafanua kuwa, kama wizara inalo eneo la Kinyikani na ni tambarare, ni vyema ujenzi wa uwanja huo, sasa kuhamishiwa hapo.



‘’Nashauri, kama hapa Kishindeni inabidili ili kujengwa uwanja wa mpira wa miguu, mjenzi aongezewe gharama, ni vyema tutafuta eneo mbadala,’’alifafanua.

Waziri huyo pamoja na ujumbe wake, baada ya kulitembelea na kujionea eneo la Kinyikani, na kisha kushauriana na kampuni, wazo lilipita kuhamishia eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kushauriana na kampuni ya ujenzi wa uwanja huo ya Reform Spotrs, Waziri Pembe, alisema sasa uwanja huo utajengwa eneo hilo.

‘’Niwambie wananchi na wapenda michezo, sasa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa mkoa wa kaskazini Pemba, utajengwa Kinyikani na sio tena Kishindenei,’’alifafanua.

Waziri huyo aliongeza kuwa, sababu ya hayo yote, ni kuepusha ujenzi wa gharama kubwa, wakati eneo lenye gharama nafuu lipo, linalomilikiwa na  serikali.

‘’Hata eneo hili la Kinyikani nalo ni serikali, na liko tambarare, sasa tumeshakubaliana kuwa, ujenzi wa uwanja wa mkoa utahamishiwa hapa Kinyikani,’’alifafanua.

Wakati huo huo, Waziri Pembe, alisema maandalizi ya ujenzi huo, alitaka uanze kuanzia leo Disemba 17, mwaka huu na kumtaka Afisa Mdhamini kupita kila wakati.



Mapema Katibu Mkuu wizara hiyo, Mattar Zahor Massoud, alisema serikali haipendi kutumia gharama kuwa, ikiwa uwezekano wa gharama ndogo upo.

Katika hatua nyingine, Katib Mkuu huyo aliwataka wanachi kuendelea kushirikiana, na wajenzi, pindi ujenzi utakapoanza.

Alieleza kuwa, Rais wa Dk. Mwinyi amekuwa mwanamichezo mkubwa, na kupelekea kuhakikisha, anasambaaza viwanja vya kisasa ngazi ya mkoa na wilaya.



Kaimu sheha wa sheha ya Kinyikani Othman Maalim Othman, ameishukuru wizara, kwa uamuzi wake, wa kuhamishia ujenzi wa uwanja huo, shehiani humo.

‘’Sisi serikali ya shehia, tumefurahi mno, kuona sasa mradi mkubwa wa ujenzi wa uwanja huu wa mkoa, wa kaskazini Pemba, utajengwa eneo hili,’’alifafanua.



Kijana wa eneo hilo Hamad Khatib Salim, alisema ujio wa uwanja huo shehiani mwao, itawapa ari na hamu zaidi sasa ya kupenda michezo.

‘’Kwanza hatunabudi kumshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa kasi yake ya ujenzi wa viwanja vya michezo kadhaa,’’alifafanua.



Mapema Mshauri Elekezi kwenye mradi wa ujenzi wa viwanja hivyo, Fesal Soud, pamoja na Meneja wa mradi kutoka kampuni ya Reform Sprts, Mohammed Oobbsoglu, wamekubaliana na ushauri wa wizara hiyo.

Meneja huyo, alisema eneo hilo ambalo ni tambarare, ni zuri zaidi, hasa kwa vile hata gharama yake itakuwa nafuu.

‘’Eneo la Kishindeni linahitaji kwanza, liwekewe kifusi ili kupatikana tambarare, maana linakabiliwa na uwezekano wa kuingia maji ya mvua kwa wingi, tofauti na hapa,’’alifafanua.


Waziri huyo wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo pamoja na ujumbe, wake walitembelea ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu, Micheweni, Mchanga mdogo, Kinyikani, Pandani na kuzitembelea Idara zilizochini yake.

          Mwisho  



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...