Skip to main content

WAZIRI PEMBE ATOA MWEZI MMOJA NA NUSU UJENZI VYOO UWANJA WA TENIS CHAKE CHAKE

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Riziki Pembe Juma, ametoa mwezi mmoja na nusu, kuanza ujenzi wa vyoo vya wanawake na wanaume, katika uwanja wa mpira wa kikapu Tenis Chake chake.

Alisema, haiwezekani kama wafadhili wamesaidia kujengja uwanja huo, kisha kuwasubiria kujenga na vyoo, hivyo ni vyema, jambo hilo likaratibiwa na wizara husika kwa haraka.

Waziri Pemba, alitoa agizo hilo jana, wakati alipofika uwanjani hapo, kukagua uwanja huo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu kisiwani Pemba, tokea alipochaguliwa.

Alisema, anataka kuona ndani ya mwezi mmoja na nusu, iwe harakati na maandalizi ya vyoo hivyo umeshaanza kwa kasi, ili kuona wapi wamekwama na kusaidia.

Alieleza kuwa, kama taasisi ya kimataifa ya ‘GIZ’ imeshasaidia kujenga viwanja vya aina hiyo Unguja na Pemba, na kama hawakufanikiwa kujenga vyoo, wizara hiyo ifanye.



Waziri Pemba, alifafanua kuwa mwezi mmoja na nusu unatosha kwa wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba, kuviendeleza vyoo vilivyopo.

‘’Kama vipo vyoo ambavyo walikuwa wakitumia wale waliokuwa wakijenga uwanja huu, ni wakati sasa kwa wizara hii Pemba, hilo kulifanyia kazi,’’alifafanua.

Aidha Waziri Pembe, alisema uwepo wa vyoo hivyo utasaidi kuimarisha kwa wanamichezo wakiwemo wanawake na wanaume, kupata pahala pa kujistiri.

Wakati huo huo Waziri huyo, alipongeza ushirikiano uliopo ndani ya wizara hiyo, na kufanikisha ujenzi wa viwanja kadhaa vya michezo.

Mapema Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba, Mfamau Lali Mfamau, alimueleza Waziri huyo kuwa, walikuwa wanafuatilia kwa ‘GIZ’, juu ya ujenzi wa vyoo hivyo.

Alieleza kuwa, wako kwenye mazungumzo ya muda mrefu, na kwa vile eneo hilo la Tibirinzi ilikuwa sio ujenzi wa moja kwa moja, bali ni ukarabati.



Kamisha Idara ya Michezo Zanzibar Ameir Mohammed Makame, alifahamisha kuwa, ukarabati kama huo, pia umefanyika eneo la skuli ya Regeza Mwendo.

Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mattar Zahor Massoud, alisifu umoja na mshikamo wa watendaji wa wizara hiyo, unaofanikisha miradi kadhaa.

Alieleza kuwa, wizara hiyo imekuwa tegemeo kwa wananchi, katika kuendeleza, michezo, utamaduni na Sanaa kwa maslahi mapana ya taifa.

Aidha, alimueleza Waziri huyo, wazo la kujenga wenyewe choo katika uwanja huo wa Tenis, ni jema na watalifanyiakazi.

Awali Sheha wa shehia ya Kichungwani wilaya ya Chake chake, Yussuf Saleh Salim, alisema uwanja huo umekuwa msaada mkubwa kwa vijana, katika kukuza vipaji vyao.

Hata hivyo, alimuomba Waziri huyo kuujengea kinga uwanja huo, ili usitumike hovyo, na watoto ambao hupitisha baiskeli na kupiga miserereko.

 Katika ziara hiyo, Waziri Pembe na ujumbe wake, walitembelea ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Ukutini, Kangani, Gombani na Wakala wa Uchapaji ofisi ya Pemba.

                  mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...