Skip to main content

UIMARISHAJI MASLAHI NI HATUA YA KUMUANDAA MSTAAFU MTARAJIWA "GORA"

 


 NA  MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

NAIBU Katibu Mkuu wa Utumishi na Utawala bora Zanzibar Omar Haji Gora, amesema kupandishwa kwa mshahara  kwa  watumishi wa  Umma katika serikali ya awamu ya nane ni miongoni mwa juhudi za serikali za kuwaandalia mustakbali mzuri wa maisha watumishi baada ya kustaafu.

Alisema hayo katika ufunguzi wa mafunzo ya maandalizi ya kustaafu kwa wastaafu watarajiwa watakaolipwa  mafao yao ya kustaafu kazi na mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF, yaliofanyika katika ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake Pemba.




Alisema katika kuhakikisha watumishi wa umma wanakua na mustakbali nzuri wa maisha yao baada ya kustaafu serikali imechukua juhudi kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wa serikali, kupandisha pensheni, pamoja na kutoa mafunzo ya maandalizi kwa wastaafu ili kuweza kupata uelewa  wa namna bora ya kujiandalia mazingira ya kuyakabili maisha baada ya kustaafu.

"Ili kuhakikisha mstaafu anauwezo wa kuyakabili maisha baada ya kustaafu mwaka 2022 serikali iliongeza kiwango cha mishahara kwa watumishi ambapo kwasasa kima cha chini cha mshahara ni shillingi laki tatu, kuongeza pensheni kwa wastaafu kutoka elfu 90 hadi laki 1na 80, pamoja na kuandaa mafunzo ya watumishi ya kujiandaa na kustaafu", alieleza.

Aidha aliwataka wastaafu hao watarajiwa kuwatumia maafisa utumishi waliomo katika taasisi zao katika kuhakiki taarifa zao kabla ya muda husika wa kustaafu ili kuepukana na changamoto mbali mbali zinazoweza kujitokeza, ikiwemo kuchelewa upatikanaji wa mafao yao.



Hata hivyo aliwashauri washiriki wa mafunzo hayo  kuishi katika uhalisia wa maisha yao, pamoja na kujiandaa kiakili,Kimwili na kijamii katika kukabiliana na changamoto za maisha ya kila siku hususan baada ya kustaafu.

Alieleza kuwa wastaafu wanamchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla, ndio maana serikali ikaweka mfuko wa hifadhi ya jamii na kanuni  ya utumishi wa umma inayosisitiza kuagwa kwa wastaafu pamoja na kupewa zawadi, ili kuonesha mchango na thamani zao katika maendeleo ya nchi.



Aidha alisisitiza viongozi wa taasisi kuzitekeleza kanuni hizo kwa vitendo, ili kuenzi na kuthamini michango ya wastaafu katika kipindi chote   cha utendaji wao wa kazi.

"Wastaafu wanamchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla, ndio maana serikali ya awamu ya nane ikaweka mfuko wa hifadhi ya jamii pamoja na kuweka  kanuni  ya utumishi wa umma inayosisitiza kuagwa kwa wastaafu pamoja na kupewa zawadi, ili kuonesha mchango na thamani zao katika maendeleo ya nchi, nasisitiza viongozi wa taasisi kuzitekeleza kanuni hizo kwa vitendo",alifafanua.

Mapema akizungumza katika mafunzo hayo Mkurugenzi Muendeshaji wa Mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF Nassor Shaaban Ameir aliwahakikishia wastaafu watarajiwa  kua, mfuko wa ZSSF uko imara na unafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na kanuni ili kuhakikisha wanachama wananufaika ipasavyo na mfuko huo.

Alieleza utaratibu wa kuwepo kwa mfuko wa hifadhi ya jamii ni utaratibu wa nchi nyingi ulimwenguni, uliokuja kusaidia upatikanaji wa haki za msingi za watumishi baada ya kulitumikia taifa.

Aliongeza kua kwa mujibu wa tathmini iliofanywa na mfuko huo mwaka 2024/2025 inaonesha kua mfuko huo uko imara kwa muda wa miaka 50 ijayo, hivyo aliwataka wanachama wa mfuko huo kuendelea kuwekeza katika ili kujihakikishia maendeleo Zaid.

Akiwasilisha mada kuhusu   matayarisho ya kustaafu Mkufunzi msaidizi wa mafunzo hayo Devid Kitomary aliwataka  wastaafu kua na mpangilio mzuri wa  matumizi ya fedha ili kuweza kuyakabili maisha baada ya kustaafu.

Aidha aliwataka  washiriki wa mafunzo  kuekeza katika maeneo tofauti ikiwemo biashara, ufugaji, maeneo ya kilimo sehemu nyengine zenye tija pamoja na kufuata  ushauri wa kitaalamu katika uwekezaji wao.

Nao washiriki wa mafunzo hayo waliupongeza mfuko wa ZSSF kwa kuandaa mafunzo hayo yaliowasaidia kujifunza kuhusu matayarisho ya kustaafu, na jinsi ya kukabiliana na maisha baada ya kustaafu, ambayo yanaweza kuwasaidia katika kukabiliana na maisha baada ya kustaafu.

Mfuko wa hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) ulianzishwa   chini ya sheria ya mfuko wa Usalama wa Zanzibar Na 2 ya 1998, ikiwa miongoni mwa  kazi zake ni kuhifadhi michango ya wanachama na kutoa mafao kwa wanachama wake, huku fao lake kuu likiwa ni fao la ustaafu  na inafanya kazi  katika visiwa vya Unguja na Pemba.

                                            MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...