Skip to main content

JAMII YATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI KUKABILIANA NA HAKI YA TABIA ZA NCHI

 



NA SALMA OMAR, PEMBA @@@

ANGOZA kwa kushirikiana na Mashirika ya kiraia pamoja na serikali, zimeiasa  jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na changamoto za haki ya tabia ya nchi.

Hayo yamesemwa katika mkutano wa mafunzo na majadiliano yaliyoshirikisha jamii na taasisi mbalimbali zikiwemo asasi za kiraia, pamoja na wawakilishi kutoka serikalini katika ukumbi wa Samail Gombani Chake chake Pemba.



Mwenyekiti wa ANGOZA Hassan Khamis Juma, amesisitiza jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na haki za tabia ya nchi, ikiwemo kujiepusha na uharibifu na uchafuzi wa mazingira.

Alieleza kua kwani, kufanya hivyo kunaweza  kupelekea athari kubwa katika jamii na kusababisha maafa baadae, na jamii kuishi katika mazingira magumu.

‘’Niwaombe sana wanajamii, kwanza waziunge mkono asasi kama ANGOZA, maana zinakuwa na wajibu wa kuhakikisha wanawakinga wananchi na majanga kadhaa, yakiwemo ya athari za mazingira,’’alisema.


Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Jumuiya ya Community Forest Pemba, Omar Mtarik, amesema utunzaji wa misitu na mali asili katika jamii, ni muhimu kuzingatiwa kwa kina.



Alifahamisha kuwa, kwani zinaleta tija na faida kubwa za kiuchumi na kimaendeleo, katika jamii  na taifa kwa ujumla, ikiwemo utunzaji wa mikoko na bahari na hata utengenezaji wa bidhaa kama viungo.

 Nae mwakilishi kutoka serikailini alieshiriki katika majadiliano huo, Ali Said Awesu amesema serikali, imejipanga kikamilifu katika kuhakikisha inashirikiana na asasi za kiaraia na jamii kwa ujumla.

 Alisisitiza kuwa, hata ndani ya Ilani ya chama cha mapinduzi CCM ya mwaka 2025/2030 katika kukabiliana na haki ya tabia za nchi, katika kuandaa mazingira mazuri kwa jamii ikiwemo kuwapatia fedha wajasiriamali wadogowadogo, hasa akinamama na watu wenye mahitaji maalum na vijana.

 Katibu Mkuu wa klabu ya waandishi wa habari Pemba, PPC Ali Mbarouk Omar, alisema jamii yenyewe inatakiwa kuwa mstari wa mbele, katika kuhakikisha  uharibifu na uchafuzi wa mazingira hautokei.


Alifahamisha kuwa, kwani wao ndio chanzo cha uharibifu wa mazingira, kwa kuwepo tabia za baadhi ya watu, kwa ukataji wa  mikono, uchimbaji wa mawe na matofali pamoja ukataji wa misitu ya juu.

 Mshiriki Kauthar Is- Haka, ameushukuru uongozi mzima wa ANGOZA kwa kushirikiana na COMMON WEALTH FOUNDATION kwa kuandaa mafunzo hayo, yanayohusu mabadiliko ya haki ya tabia za nchi, kwa kuwajengea uwezo wanawake katika kuwaongoza na kuwasimamia katika kazi zao za kila siku.

 Aidha aliishukuru serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, katika kuwasaidia wanawake suala la kukabiliana na mabadiliko ya tabia za nchi, kwa kufanyakazi pamoja kwa kushirikiana na asasi za kiraia katika kuiendeleza jamii iliyo bora.

                          mwisho 



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...