Skip to main content

WAZIRI PEMBE" SIJARIDHISHWA UJENZI UWANJA WA SOKA KANGANI

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar Riziki Pembe Juma, amesema hajaridhishwa na kasi ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu uliopo Kangani wilaya ya Mkoani Pemba.

Alisema, sababu ambazo zilizotolewa za kuzorotesha ujenzi wa uwanja huo, hazijamridhisha na kuwataka wajenzi wa uwanja huo, kuzidisha kasi ya ujenzi.

Waziri Pembe, aliyasema hayo jana uwanjani hapo, kwenye ziara ya siku tatu, aliyoambatana na Katibu Mkuu wake, Mattar Zahor Massoud, ya kuvitembelea viwanja kadhaa kisiwani humo.

Alieleza kuwa, sababu ya uhaba wa tendaji, kuadimika kwa saruji na kuchelewa kuvipokea baadhi ya vifaa vya ujenzi huo, wala sio sababu za msingi.



Alieleza kuwa, viwanja hivyo vinasubiri kwa hamu na wananchi na wanamichezo ili wavitumie, hivyo lazima kampuni ya Reform Sports kutoka Uturuki, inayojenga viwanja hvyo kuzidisha kasi.

Alieleza kuwa, serikali imeamua kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya viwanja hivyo, ni lazima waliokubali kuchukua kazi hiyo, waiharakishe.

‘’Baada ya maelezo yenu, kwa hakika sababu za uhaba wa watendaji, mara saruji kuadimika, mara mvua ilinyesha jana na jioni au kuchelewa kupokea vifaa ni sababu nyepesi,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine Waziri huyo wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar Riziki Pembe Juma, alisema Dk. Mwinyi ameamuwa kujenga viwanja hivyo ikiwa ni hatua ya kuibua vipaji.

Alieleza kuwa, vipaji hivyo kisha vinaweza kuzaa ajira, kwani, kwa sasa michezo ni sehemu ya maendeleo kwa vijana mbali mbali.



‘’Dk. Mwinyi amekuwa akihakikisha anaweka miundombinu ya viwanja hivi, tena vya kisasa, lengo ni kuibua vipaji, na kisha kiviendeleza ili vijana hao waweze kupata ajira kupitia sekta hiyo,’’alifafanua.

Akiwa katika ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Ukutini, Waziri huyo aliitaka kampuni inayojenga uwanja huo, kuzidisha kasi kwa haraka.

Mapema Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mattar Zahor Massoud, alisema michezo ni eneo moja wapo, linalokusanya idadi ya watu wingi, tena kwa wakati mmoja.

Alifafanua serikali ya awamu ya nane, kwa kujali umuhimu huo, ndio maana imekuwa ikitumia fedha nyingi kuhakikisha inajenga viwanja mjini na vijijini.



Alieleza kuwa, kilichobakia kwa wananchi na hasa vijana kuvitumia viwanja hivyo, kwa mambo kadhaa ikiwemo kujega afya, umoja na kuwa sehemu ya ajira.

‘’Niwaombe sana wananchi, viwanja hivyo tuvienzi na kuvitunza maana ni sehemu ya kujenga umoja na kubwa zaidi ni kuona vijana wanafika mbali kimichezo,’’alifafanua.

Kwa upande wake Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba Mfamau Lali Mfamau, alisema ujenzi wa viwanja hivyo ni sehemu ya mpango mkuu wa wizara.



Kwa upande wake Mshauri Elekezi Fesal Soud, alisema ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Kangani, kwa sasa umeshafikia asilimia 92, na wakati wowote utakamilika.

Alieleza kuwa, ujenzi wake ulianza mwanzoni mwa mwezi huu, ingawa kutokana na sababu kadhaa, ikiwemo kuchelewa kwa vifaa na hali ya hewa, umechelewesha.

Wakati huo huo, wananchi wa Ukutini pamoja na sheha wao Ali Hussein, waliipongeza wizara hiyo, kwa hatua ya kupata ajira za muda.



Katika ziara hiyo, Waziri huyo na ujumbe wake, ulivitembelea viwanja wa mpira wa miguu Kangani, Ukutini, viwanja vya mchezo wa kikapu Tenis Chake chake na Kangani, pamoja na wakala wa uchapaji.

              Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...