.....BADO wanamtaka, bado wanamtamani, bado wana hamu nae katika safu ya uongozi.
Maana wanasema, ameyatekeleza aliyoaahidi, maana wanasema kweli ni mtetezi wa wananchi.
Ni Mgombea Uwakilishi Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Bahati Khamis Kombo, anaewania tena nafasi hiyo kwa mara ya tatu,
hapa anaesema kama akipata tena ridhaa, kundi la wanawake wajane
na vijana, atawaimarishia miundombinu ya kujiwezesha kiuchumi.
Akizungumza na
waandishi wa makala hii, mara baada ya uzinduzi wa kampeni eneo la Dodo Pujini,
alisema kupitia Ilani ya CCM, mikakati yake, ni kuona na kundi hilo
analiwezesha.
Alisema, ndani
ya jimbo hilo, anajua kuwa wapo vijana wasiokuwa na ajira na wale wajane
walionyimwa haki zao kwa njia moja ama nyingine, hivyo nia yake ni kuwawezesha.
Alieleza kuwa
moja ya mbinu atakazotumia ni kuwapa taaluma ya ujasiriamali na kuwatafutia mikopo,
ambayo itakuwa chachu ya kuendesha maisha yao.
Alisema njia
nyingine ni kuwawezesha kwa kazi za mikono, kama kufuma na kushona, ili iwe
njia sahihi ya kufikia ndoto zao.
‘’Hapa ninacho
hitaji kutoka kwa wananchi wa jimbo hili, kwanza waweke kando tofauti za vyama,
wanipe kura ili niendeleze mbinu za kuling’arisha jimbo letu,’’alifafanua.
Aidha mgombea
huyo, aliwataka wanachama wa vyama vingine, kuendelea kubakia na vyama vyao,
hadi miaka 100 ijayo, ingawa anachotaka ni kura za za ndio.
‘’Suala la
vyama kwa kila mmoja na chake hakuna shida, maana ndio demokrasia, lakini
ninachoomba waniazime kura, niwalipe maendeleo,’’alieleza.
Katika hatua
nyingine, mgombea huyo uwakilishi, alisema ahadi nyingine kwa wananchi wa jimbo
hilo, ni kuimarisha huduma za kijamii, ikiwemo maji safi na salama kwa vijiji
vyenye changamoto.
‘’Inawezekana
bado kuna vijiji kutokana na chakavu wa miundombinu huduma ya maji ni
changamoto, nipeni tena ridhaa kumaliza tatizo hilo,’’alifafanua.
Hata hivyo, alisema
kama akipata ridhaa, ataendelea na utamaduni wake wa kusaidia kambi za wanafunzi
wanaojiandaa na mitihani ya taifa, ikiwa ni njia moja wapo ya kuimarisha elimu.
‘’Pamoja na sekta ya elimu, nitaangalia kwa vile vijiji ambavyo hata barabara ya kifusi ni changamoto, ingawa naelewa kasi ya Dk. Mwinyi, haijakiacha hata kijiji kimoja,’’alifafanua.
Katua nyinginem anasema wakati umefika kwa wapiga kura
kuwaamini, ili kuliimarisha jimbo hilo.
Alieleza
kuwa, wananchi wa Chambani kwa kila mwenye macho kamili, atakubali kuwa sasa
jimbo hilo, limepiga hatua ikiwemo huduma za afya, elimu, barabara, huduma ya maji
safi na salama.
‘’Mimi
niwasihi wananchi wa Jimbo la Chambani wakichague Chama cha Mapinduzi na
wagombea wake wote, ili kuliendeleza jimbo hili, vyenginevyo watakuja juta,’’alisema.
Mapema Mwenyekiti
wa CCM wilaya ya Mkoani Ali Juma Nassor, alisema CCM imefikiwa vyema ndani ya
wilaya ya Mkoani, kwa kuwepo miundombinu kamili ya huduma za kijamii.
Kuhusu
uimarisha na matawi ya chama, alisema kwa sasa yaliomo jimbo la Chambani ni ya
kisasa na watendaji wanafanyakazi, kwenye mazingira bora.
Baadhi ya wananchi
wa Chambani, waliwataka wagombea hao kutokuwa na hofu ya kura zao, kwani
wanayakumbuka mazuri waliowatendea miaka mitano, iliyopita.
Hassan Juma
Mohamed, alisema zipo alama zilioachwa na Mwakilishi wao, ikiwemo ujenzi wa
skuli za maandalizi, ukarabati wa vyumba vya madarasa.
Nae Hussan
Haji Kombo, alisema katika eneo la shehia ya Ukutini, hadi leo wanaendelea
kutumia huduma ya maji safi na salama, baada ya kuchimbiwa kisima cha kisasa.
Kwa upande
wake Subira Mohamed Makame, alisema skuli ya maandalizi iliyopo Chumbageni,
wanaendelea kujivunia ikiwa ni ahadi, iliyotekelezwa na Mwakilishi wao.
NYARAKA ZINASEMAJE
Taarifa ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC, inafafanua kuwa, kwa uchaguzi wa 2020, wanaume walioteuliwa na vyama kugombea kuingia katika Baraza la Wawakilishi walikua 190 na walioshinda ni 42 wakati wanawake walikuwa 61 na walioshinda ni wanane (8).
Taarifa za Shirika la Wanawake la Umoja wa Mataifa (UN Women) na Umoja wa Mabunge (IPU) za 2017 zimeonesha kuwepo ongezeko dogo la viongozi wanawake katika serikali na mabunge.
Maana katika majimbo 50 ua uchaguzi ya Zanzibar, wanawake katika baraza la kutunga sheria, wanane hii ni saw ana asilimia16, wabunge ni wannne kwa asilimia 8, mawaziri ni sita sawa na asilimia 33 na Makatibu Wakuu ni saba sawa na asilimia 39.
Katiba ya Zanzibar ya 1984, kwenye kifungu cha 11 na cha 14, vimeweka wazi kuwa kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu.
Aidha Dira ya Zanzibar ya 2050 imeelezea jinsi gani masuala ya usawa wa jinsia juu ya kuondoa unyanyasaji na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake.
Sera ya jinsia inaeleza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi, katika ngazi zote ni mdogo na kwa hivyo serikali, kwa kushirikiana na wadau wengine, itafanya juhudi kuona makundi yote na yaliyopembezoni.
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC) ambayo mkataba wake ulitiwa saini mwaka 2008 inaeleza, kutaka kuondoa utafauti na kuwatenga wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo na kusaidia kuwepo usawa wa kijinsia katika nchi wanachama na kufikia asilimia 50/50 kwenye maamuzi.
Makubaliano yanayojulikana kama ‘Itifaki ya Maputo’ ambayo yalifanyika Msumbiji mwaka 2003, inacho kipengele kinachoonyesha haki ya wanawake, kushiriki katika siasa na mchakato wa vyombo vya kutoa maamuzi.
Mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi, (CEDAW) wa mwaka 1979 ambao unapinga aina zote za udhalilishaji na kusisitiza, ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.
Ibara 12, inasisitiza ushiriki sawa wanawake na wanaume kufikia asilimia 50/50 kwenye nyanja za maamuzi, serikalini na taasisi binafsi.
Aidha jukwaa la Mpango wa Utekelezaji wa Beijing mwaka 1995, ibara ya 7 kinataka ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia kwenye ngazi zote za uongozi.
WANAHARAKATI
Kaimum Maratibu wa TAMWA-Pemba Amina Ahmed Mohamea, anasema wamekuwa na miradi kadhaa, kwa ajili ya kuwajengea uwezo wanawake, ili waingie kwenye safu ya uongozi.
eneo jingine anasema ni kuwajengea uwezo, waandishi wa habari, ili kuwaibua viongozi wanawake waliofanya vyema, na kuwa mfano kwa wingine.
Tatu Abdalla Msellem, anasema bado changamoto iko kwa jamii, kuwaamini wanawake kama wanaweza kuongozo na kutekeleza ahadi ambazo huwa wanaaziweka.
''Lakini kwa wananchi ambao wanataka ushuhuda waende Jimbo la Chambani Mwakilishi wao anaewania tena Bahati Khamis Kombo, amefanya vizuri katika historia ya jimbo hilo,''anasema.
Hata Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake CHAPO Mohamed Hassan Abdalla, aliwataka wananchi wa Jimbo la Chambani, kumrejesha tena Mwakilishi wao Bahati Khamis Kombo, ikiwa wanataka maendeleeo.
''Kweli wanawake wanaweza, maana Jimbo la Chambani kwa sasa limebadilika kimaendeleo, mfano elimu, huduma ya maji safi na salama, amefanya vizuri sana yule mama,''anasema.
Mwisho

Comments
Post a Comment