Skip to main content

MGOMBEA UWAKILISHI CCM CHAMBANI KUWAWEZESHA WAJANE, VIJANA AKIPATA RIDHAA

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Uwakilishi Jimbo la Chambani wilaya ya Mkoani, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Bahati Khamis Kombo, amesema kama akipata tena ridhaa, kundi la wanawake wajane na vijana, atawaimarishia miundombinu ya kujiwezesha kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya uzinduzi wa kampeni eneo la Dodo Pujini, alisema kupitia Ilani ya CCM, mikakati yake, ni kuona na kundi hilo analiwezesha.

Alisema, ndani ya jimbo hilo, anajua kuwa wapo vijana wasiokuwa na ajira na wale wajane walionyimwa haki zao kwa njia moja ama nyingine, hivyo nia yake ni kuwawezesha.

Alieleza kuwa moja ya mbinu atakazotumia ni kuwapa taaluma ya ujasiriamali na kuwatafutia mikopo, ambayo itakuwa chachu ya kuendesha maisha yao.

Alisema njia nyingine ni kuwawezesha kwa kazi za mikono, kama kufuma na kushona, ili iwe njia sahihi ya kufikia ndoto zao.

‘’Hapa ninacho hitaji kutoka kwa wananchi wa jimbo hili, kwanza waweke kando tofauti za vyama, wanipe kura ili niendeleze mbinu za kuling’arisha jimbo letu,’’alifafanua.

Aidha mgombea huyo, aliwataka wanachama wa vyama vingine, kuendelea kubakia na vyama vyao, hadi miaka 100 ijayo, ingawa anachotaka ni kura za za ndio.



‘’Suala la vyama kwa kila mmoja na chake hakuna shida, maana ndio demokrasia, lakini ninachoomba waniazime kura, niwalipe maendeleo,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, mgombea huyo uwakilishi, alisema ahadi nyingine kwa wananchi wa jimbo hilo, ni kuimarisha huduma za kijamii, ikiwemo maji safi na salama kwa vijiji vyenye changamoto.

‘’Inawezekana bado kuna vijiji kutokana na chakavu wa miundombinu huduma ya maji ni changamoto, nipeni tena ridhaa kumaliza tatizo hilo,’’alifafanua.

Hata hivyo, alisema kama akipata ridhaa, ataendelea na utamaduni wake wa kusaidia kambi za wanafunzi wanaojiandaa na mitihani ya taifa, ikiwa ni njia moja wapo ya kuimarisha elimu.

‘’Pamoja na sekta ya elimu, nitaangalia kwa vile vijiji ambavyo hata barabara ya kifusi ni changamoto, ingawa naelewa kasi ya Dk. Mwinyi, haijakiacha hata kijiji kimoja,’’alifafanua.



Nae Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo Mohamed Abra-haman Mwinyi, alisema wakati umefika kwa wapiga kura kuwaamini, ili kuliimarisha jimbo hilo.

Alieleza kuwa, wananchi wa Chambani kwa kila mwenye macho kamili, atakubali kuwa sasa jimbo hilo, limepiga hatua ikiwemo huduma za afya, elimu, barabara, huduma ya maji safi na salama.

‘’Mimi niwasihi wananchi wa Jimbo la Chambani wakichague Chama cha Mapinduzi na wagombea wake wote, ili kuliendeleza jimbo hili, vyenginevyo watakuja juta,’’alisema.

Mapema Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mkoani Ali Juma Nassor, alisema CCM imefikiwa vyema ndani ya wilaya ya Mkoani, kwa kuwepo miundombinu kamili ya huduma za kijamii.





Kuhusu uimarisha na matawi ya chama, alisema kwa sasa yaliomo jimbo la Chambani ni ya kisasa na watendaji wanafanyakazi, kwenye mazingira bora.

Baadhi ya wananchi wa Chambani, waliwataka wagombea hao kutokuwa na hofu ya kura zao, kwani wanayakumbuka mazuri waliowatendea miaka mitano, iliyopita.




Hassan Juma Mohamed, alisema zipo alama zilioachwa na Mwakilishi wao, ikiwemo ujenzi wa skuli za maandalizi, ukarabati wa vyumba vya madarasa.

Nae Hussan Haji Kombo, alisema katika eneo la shehia ya Ukutini, hadi leo wanaendelea kutumia huduma ya maji safi na salama, baada ya kuchimbiwa kisima cha kisasa.

Kwa upande wake Subira Mohamed Makame, alisema skuli ya maandalizi iliyopo Chumbageni, wanaendelea kujivunia ikiwa ni ahadi, iliyotekelezwa na Mwakilishi wao.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...