Skip to main content

WAANDISHI WA HABARI WASHAURIWA KUJIFUNZA LUGHA ZA ALAMA

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WAANDISHI wa habari wameshauriwa kujifunza lugha za alama ili kuhakikisha uwepo wa  uandishi  jumuishi katika kazi zao.

Wito huo umetolewa na Mratibu Baraza la Taifa la Watu wenyeulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini  Chake chake Pemba.

Alisema  ili kuhakikisha watu wenyeulemavu wa uziwi wanapata nafasi ya  kutoa taarifa kuhusu mafanikio na changamoto mbali mbali walizonazo ni muhimu kujifunza lugha ya alama ili kurahisisha mawasiliano baina yao.

Alieleza kua, suala la kutoa na kupata taarifa ni haki ya kila mmoja katika jamii, lakini bado inaonekana ni changamoto hususani kwa watu wenye ulemavu wa uziwi, kutokana na kukosa fursa hiyo, kutokana na baadhi ya waandishi kutokujua namna bora ya kufanya nao mawasiliano.

" Kwavile kutoa na kupokea taarifa ni haki ya msingi ya kila mtu, ni vyema waandishi wa habari kujifunza na kuijua lugha ya alama, ili kurahisisha upatikanaji wa haki hiyo kwa watu wenyeulemavu wa uziwi", alisema.

Alisema kua, watu wenye ulemavu wa uziwi ni sehemu ya jamii, ambapo wanakua na changamoto na masuala yao mbali mbali wanayotamani yasikike katika vyombo vya habari kwa lengo la kuataka ufafanuzi, au msaada lakini  changamoto zinabaki katika njia za mawasiliano, hivyo uelewa wa lugha ya alama kwa waandishi wa habari itasaidia katika ujumuishi wao.

Alisisitiza kua,  lengo la uandishi habari jumuishi halitafikiwa iwapo hakutokua na miundombinu rafiki ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kuwasiliana vizuri na waandishi wa habari.

Aliongeza kua,  ipo haja kwa waandishi kujifunza lugha hiyo ili kuungamkono sera, sheria, katiba na mikataba mbali mbali ya haki za watu wenye ulemavu ya kuhakikisha wanajumuishwa katika sekta zote nchini.

Aidha alitoa wito kwa watu wa karibu wa watu wenye ulemavu wa uziwi kutoa ushirikiano wa kutosha  kwa waandishi wa habari pale inapohitajika, kwa  kuwakalimania ili kuhakikisha saiuti za watu hao zinasikika na kufanyiwa kazi.

Kwa upande wake  Naibu  Katibu  Mkuu Jumuiya  ya Viziwi Zanzibar (JUVIZA)  Yahya Hamed Seif alisema, kutokujua lugha ya alama kwa baadhi ya waandishi wa habari ni changamoto inayokwamisha ujumuishi wao.

Alieleza kua, hali hii inawakosesha ushiriki wa moja kwa moja katika kuwasilisha maoni yao katika vyombo mbali mbali vya habari, na kupelekea kutopaza sauti zao ipasavyo.



" Wapo waandishi wanaozungumza na sisi kupitia ujumbe mfupi wa maandishi au kukalimaniwa na watu wetu wa karibu, hiii inatunyima ushiriki wa moja kwa moja katika mijadala au mazungumzo ya kuwasilisha maoni yetu, hasa ukizingatia wao ni sauti ya wasio na sauti", alieleza Yahya.

Aidha alitoa wito kwa waandishi na taasisi nyengine zinazosimamia haki za watu wenyeulemavu kujifunza lugha ya alama ili kujiongezea maarifa na kuhakikisha ujumuishi wa mazungumzo yao ya kila siku.

Kwa mujibu wa kifungu cha 28(1) (d) cha sheria cha Sheria ya watu wenyeulemavu ya Zanzibar ya mwaka 2022 kinaeleza kua watu wenyeulemavu wanahaki ya kupata habari na mawasiliano kwa kuzingatia aina ya ulemavu.

                                                                   MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...