Skip to main content

HAYA HAPA MAAJABU YA ARV DHIDI YA MTOTO MCHANGA, PINDI UKIFUATA..........

 



NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@

ARV ni dawa zinazopambana na virusi vya VVU kwa mtu anayeishi na maambikizi ya virusi hiyo.

Wataalamu wa afya mwanadamu wanakubali kuwa, dawa hizo zinasaidia mno kumpa uhakika wa kusihi, mtu anayeishi na VV.

Wanakubali kuwa, zenyewe hazitibu VVU, bali huzuia virusi kuongezeka na kulinda kinga ya mwili.

Lengo ni kupunguza virusi hadi kufikia kiwango cha kutogundulika (undetectable).

Wataalamu wa afya wanasema dawa za ARV, zinaingia ndani ya seli za kinga na kuzaliana, na kisha hukatiza hatua za uzalishaji wa virusi kwa njia hiyo.

Kitaalamu kuna madaraja mbali mbali ya ARV, lakini huwa hutolewa kwa pamoja kama mchanganyiko.

 Mfano,T+L+D huu ni mfumo wa kitaalamu ambao ni mchanganyiko wa kidonge kimoja chenye dawa tatu, ambapo daktari huchagua dawa kulingana na afya ya mgonjwa.

 

Daktari Khamis Hamad Ali ambae ni Mratibu wa kitengo cha maradhi ya Ukimwi, homa ya Ini, Kifua kikuu na Ukoma Pemba, anasema moja ya faida za matumizi ya ARV ni kupunguza kiwango cha virusi (viral load).

Anasema hii ni kulinda na kurudisha kinga ya mwili kupanda kwa seli za CD4 kupunguza hatari ya kuambukiza wingine.

MAAJABU YA MINGINE YA ARV

Mratibu huyo anasema, tafiti mbali mbali zilizofanywa na wataalamu wa afya na hata kuthibitishwa na WHO, kwamba sasa dawa hizo ni kinga ya VVU kutoka kwa mama kwenda mtoto.

 

Haya yatawezekana ikiwa mjamzito mwenye VVU atafuata maelekezo ya wataalamu wa afya, yakiwemo ya matumizi sahihi ya dawa za ARV.

 

Anathibitisha kuwa, dawa hizo sio tu kuwa na uwezo wa kumkinga mtoto, bali hata mama mwenyewe kufubaza (kupunguza) na hata wakati mwingine kutoonekana kwa virusi mwilili.

 

Kumbe ARV zikitumika vyema na chini ya uangalizi wa daktari, uwezekano wa kuzaliwa mtoto akiwa salama ni mkubwa kwa asilimia zaidi ya 90.

 


Anasema sio tu ARV zinamkinga mtoto huyo anapokuwa na maisha ya tumboni, bali hata wakati wa kuzaliwa na kunyonyeshwa.

 

Ili kumkinga mtoto huyo pamoja na mama kutumia dawa za ARV, wanahakikisha wakati anajifungua damu zao hazichinganyiki wawili hao.

 

Daktari Khamis anasema mara baada ya kuzaliwa kwake mtoto huyo, hufanyiwa vipimo, ili kugundulika ikiwa ana VVU au laa.

 

‘’Lengo ni kugundua afya, na ikiwa ameambukizwa haraka kuanzishiwa dozi ya ARV, yenye lengo la kupunguza makali na ikiwa hana, anaweza kurejeshwa tena kwa uchunguuzi,’’anasisitiza.

 

Akawakumbusha mama wenye VVU kuhakikisha wanawanyonyesha watoto wao chini ya maelekezo ya wataalamu wa afya, na sio zaidi ya miezi sita.

 

‘’Ikimalizika miezi sita, mama huyo hutakiwa kumuanzishia vyakula vya lishe, ambayo vitakavyosaidia kuimarisha afya na makuzi yake,’’anasema.

 

Shuhuda wa hili ni Maryam Salim wa Chake chake, ambae anaishi na VVU kwa zaidi ya miaka 17 sasa, amepitia hatua hii ya kupata watoto bila ya maambukizi.

 

‘’Ni kweli ninao watoto wanne, ni mmoja tu mwenye VVU kwa kule kunyanyapaliwa, nilikosa matumizi sahihi ya ARV na kumuambukiza,’’anasema.

 


Anakiri kuwa, mimba zake nyingine baada ya kukubali ushauri wa wataalamu wa afya, aliwabebea mimba na kuwanyonyesha na hadi sasa wako salama.

 

‘’Matumizi ya ARV kama utayafuata kama wataalamu wanavyotaka, mbona ni kinga tosha ya kutomuambikiza mtoto na VVU,’’anakiri.

 

Kumbe nae anakiri kuwa, miezi sita ilitosha kwa kila mtoto wake kumnyonyesha, na kisha kuwaanzishia mlo kamili, uliojenga afya zao.

 

Muume wa Maryam Sabri Issa Mbega, ambae hadi sasa yuko salama, anakiri kuwa ARV ndio mwarubaini wa kuwa na watoto watatu bila ya VVU.

 

‘’Kwanza nilikuwa nafikiria tu kwamba ARV ni kwa ajili ya kupunguza makali kwa mke wangu mwenye maradhi ya Ukimwi, lakini kumbe ni kinga kwa watoto wangu,’’anasema.

 

JAMII

Issa Ali Khamis wa Wete, anasema wamekuwa na woga kufunga ndoa na kuzaa na wanawake wenye VVU, kwa hofu ya kuambukizwa wao, na watoto wao.

 

‘’Mimi ninachokifahamu kuwa ARV ni kwa ajili ya kufumbaza makali ya VVU, lakini kumbe sasa watalaamu wamebaini, ni kwa kinga ya mtoto ni jambo jema,’’anasema.

 

Wahida Omar Haji wa Wawi, anaona kama kivuli anaposikia ‘ARV’ kuwa sasa zimekuwa kinga ya ‘VVU’ kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,’’anaeleza.

 

Mchanga Said Kombo wa Chake chake, anakiri kuwa hata jirani yake, ameshazaa watoto wawili na kuwanyonyesha miezi sita sita na sasa wako salama.

 

TUME YA UKIMWI

Ali Mbarouk Omar ambae ni Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba, anasema ARV sasa ni zaidi ya dawa ya kufubaza makali ya ukimwi, kwani imegeuka kinga ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

 

‘Tunawahimiza wajawazito wenye maambukizi ya VVU, kutuma dawa kwa usahihi, ili kujenga afya yake na magonjwa mingine nyemelezi, na kumkinga mtoto aliyeko tumboni,’’anasema.

  

TAKWIMU

Wapo watoto 500 tayari wameshazaliwa wakiwa hawana maambukizi ya VVU kutoka kwa mama, ambao wanaishi na maradhi hayo.

Idadi hii iliyothibitishwa na Mratibu Khamis Hamad Ali ni kwa mwaka 2024 kutoka wilaya nne za Pemba.

Anasema wote hao wazazi wao walikubali kufuata kikamilifu ushauri, maelekezo na miongozo ya watalaamu wa afya.

Ingawa kwa kipindi hicho pia, wapo wingine saba ‘7’ ambao wazazi wao walikuwa wagumu kwanza, kutumia ARV, na ushauri mwingine na hatimae kuwaambukiza wakati wa kujifungua au kuwanyonyesha.

WHO

Shirika la Afya Duniani (WHO) na mashirika mingine ya afya yalipendekeza, mama mwenye VVU kunyonyesha mpaka mtoto atakapofika miezi sita 6 au chini ya hapo.

Kwenye mataifa yanayoendelea Tanzania ikiwemo, familia zisizokuwa na kipato kikubwa, zinaweza kuhitimisha miezi sita na kisha kuwaanzisha vyakula vya lishe.

WHO inakiri kuwa faida mojawapo kubwa ya kunyonyesha mtoto ni kumpatia kinga imara, kupitia katika maziwa ya mama ili kupambana na vimelea mbalimbali vya magonjwa.

MITANDAO YA KIJAMII

Katika taarifa mpya ya BAN matokeo yanaonesha kwamba hatari ya maambukizi ya VVU huongezeka mara mtoto anapoacha kunyonya akiwa na miezi sita.

Katika kukabiliana na hili, Shirika la Afya Duniani linapendekeza kwa mama mwenye maambukizi ya VVU kuendelea kumnyonyesha mtoto wake mpaka atakapofikisha mwaka mmoja.

Katika tafiti hii ambayo ilifanyika nchini Malawi katika kipindi cha mwaka 2004/2010, daktari. Denise J. Jamieson, kutoka kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa, (CDC) cha huko Atlanta, nchini.

Hitimisho katika tafiti hiyo ilikuwa kwamba kumuachisha mtoto kunyonya maziwa ya mama mapema siyo njia salama na sahihi, kwani mikakati ya kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa watoto.

WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya ya Tanzania  imefanya juhudi kubwa kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, na kiwango cha maambukizi kimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2010 hadi asilimia 8.1 kwa mwaka 2023.

Wizara imeanzisha kampeni za uhamasishaji ili kuongeza ufahamu kuhusu umuhimu wa kapimana magonjwa kadhaa kwa wajawazito.

Hii inasaidia kuhakikisha kuwa wanawake wanaoishi na ugonjwa huo, wanapata amatibabu sahihi ili kuzuiya maambukizi kwa watoto wao.

Ushirikiano na washirika wa maendeleo,Wizara inashirikiana na mashirika kama USAID na tume ya taifa kudhibiti ukimwi (TACAIDS), ili kuimarisha mikakati ya kupambana na vvu.

Kiwango cha maambukizi ya VVU, kutoka kwa mama kwenda kimepungua kwa zaidi ya asilimia 95 ya watoto waliozaliwa na bila maambukizi.

MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...