Skip to main content

CHAMBANI, WAZINDUZI KAMPENI BAHATI AAHIDI NEEMA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Uwakilishi wa Jimbo la Chambani kwa tiketi ya CCM Bahati Khamis Kombo, amesema kama akipewa tena ridhaa ya kushika nafasi hiyo, atahakikisha anaendeleza alipoishia kwa miaka mitano iliyopita.

Mgombea huyo uwakilishi aliyasema hayo leo Septemba 29, mwaka huu uwanja wa mpira wa Dodo Pujini jimboni, kwenye uzinduzi wa kampeni kwa jimbo hilo, wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa Ilani ya CCM.

Alisema aliamua kuomba tena nafasi hiyo, baada ya kuona bado anadeni la maendeleo kwa wananchi wa Jimbo la Chambani, katika huduma mbali mbali za kijamii.


Alisema, CCM kila baada ya miaka mitano, imekuwa ikiwaletea Ilani, ambayo ndio mpango kazi mkuu wa utendaji wa kazi, na inatoa dira ya miradi kadhaa inayokusudiwa kutekelezwa.

‘’Hivi sasa CCM, imeshaleta tena Ilani kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2025/2030 na ndani yake yamo miradi ya maendeleo, na ndio maana, naomba tena ridhaa kuyaendeleza hayo,’’alifafanua.

Nae Mbunge mteule nafasi za wanawake mkoa wa kusini Pemba Maryam Azam Mwinyi, amesema wagombea wote walioteuliwa na CCM, wanatosha kuwaletea heshima ya maendeleo wananchi.

‘’Kwa hakika, wagombea kuanzia wale wa wadi, majimbo na ngazi ya urais, wanayoheshima na uhakika wa kuwaletea maendeleo wananchi bila ya ubaguzi,’’alifafanua.

Mapema Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mkoani Ali Juma Nassor, alisema chama kimerudi tena kwa wananchi, kuwaomba ridhaa, ili kuendeleza maendeleo.

Alieleza, CCM imewaletea madiwani, wawakilishi, wabunge na ngazi ya urais, ili kuendelea kuzitatua changamoto za wananchi katika sekta mbali mbali.

Nae mjumbe wa Baraza kuu la UWT taifa Leila Mohamed Mussa, amesema ndani ya CCM vitendo vinatosha na sio porojo, kama vilivyo baadhi ya vyama.

Aidha alisema vipo vyama vimekuwa na maneno mazuri ambayo, hayana msingi wala dira, na kuwaomba wananchi kuwapigia kura wagombea wote wa CCM.

Akizungumzia Mgombea uwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, alisema amekuwa mweledi wa kudai haki za wananchi, bila ya ubaguzi.   


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa UWT taifa Zainab Khamis Shomari, aliwashauri wananchi wa jimbo hilo, kuwachagua viongozi wote CCM, ili kuendelea kulibadili jimbo la Chambani kimaendeleo.

‘’Leo tukilizungumzia Jimbo la Chambani, lenyewe linabadiliko, maana viongozi wanaoliongoza wanakubalika kwani  wanafanyakazi kwa nia thabiti,’’alifafanua.

Akiwanadi wagombea ubunge, uwakilishi na madiwani wa Jimbo la Chambani Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa, Massoud Ali Mohamed, amesema kura sio anasa bali ni kazi.

‘’Kama ni kazi, basi wanaoiweza ni wagombea wa Jimbo la Chambani pekee, na hivyo kura zenu msizitupe kwa kuwapa wagombea, ambao kisha wanayahama majimbo yao,’’alisema.

Hata hivyo, aliwashauri wagombea wa vyama vyingine, kushindana kwa sera, na sio matusi wala kashfa, kwani watanzania hawahitaji malumbano.


Mgombea ubunge wa Jimbo la Chambani Mohamed Abrhaman Mwinyi, amesema anahitaji ushrikiano wa dhati kutoka kwa wananchi, ili kufanikisha ndoto za wananchi.

                       mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...