Skip to main content

MAAFISA JESHI LA POLISI WATAKIWA KUHESHIMU HAKI ZA BINAADAMU


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@
KAMISHNA wa Tume ya Haki za Binadamu Zanzibar Khatib Mwinchande amesema, maafisa wa utekelezaji wa Sheria kwa nyakati zote wanapaswa kutimiza wajibu walioekewa kisheria kwa kuhudumia jamii na kulinda watu wote dhidi ya vitendo vinavyoenda kinyume na Sheria, kwa kuzingatia kiwango cha juu cha uwajibikaji kinachohitajika na taaluma yao.

Akizungumza na maafisa wa Jeshi la Polisi Pemba katika mafunzo ya uzingatiwaji wa haki za binadamu na misingi ya Utawala Bora katika mchakato wa uchaguzi mkuu 2025 yaliyofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, kamishna huyo alisema, katika kipindi cha uchaguzi Jeshi la Polisi lina wajibu wa kujiepusha na migogoro isiyo ya lazima na badala yake wahakikishe usalama wa watu na mali zao katika kipindi chote cha uchaguzi.

Alisema kuwa, ni wajibu wa Jeshi la Polisi kusimamia uhuru, haki na amani ili wananchi waweze kutimiza haki yao ya kikatiba katika kuchagua viongozi wao, huku wanapotekeleza majukumu yao wazingatie maadili ya kazi, kuzingatia haki za binadamu na utawala Bora.



"Mafunzo hata yatawasaidia maafisa wa Jeshi la Polisi kutimiza wajibu wao na kuhakikisha haki za binadamu na misingi ya utawala uora inazingatiwa wakati wote wa mchakato wa uchaguzi," alisema Kamishna huyo.

Alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kuongeza uelewa wa maafisa wa Jeshi la Polisi kama maafisa wa utekelezaji wa Sheria kuhusu umuhimu wa kuzingatia haki za binadamu na misingi ya utawala uora katika uchaguzi mkuu 2025," alieleza.

Kamishna huyo alisema, Tume kwa kuzingatia Sheria ina jukumu la kuhamasisha hifadhi ya Haki za binadamu na wajibu kwa jamii pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu haki za binadamu na utawala bora.

Alisema kuwa, ili uchaguzi uwe huru na wa haki kabla, wakati na baada, haki za binadamu zinapaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekeleza kwani uchaguzi ni mchakato muhimu katika nchi inaozingatia misingi ya demokrasia, uhuru, haki na amani, hivyo wananchi hutumia haki yao kushirikia katika shughuli za utawala wa umma moja kwa moja au kupitia wawakilishi waliowachagua.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba SSP Kilogi Warioba aliwataka maafisa hao kuyatumia vyema mafunzo hayo kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zao za kila siku, ili wawe ni wenye kufuata misingi ya Sheria.



"Tujue wajibu wetu ni nini, pia tunaelewa changamoto za utendaji wetu wa kazi nini, tujiepushe kuwa ni sehemu ya uvunjifu wa haki za binadamu, hii itatusaidia sana katika utekelezaji wa majukumu yetu," alisema Kaimu huyo.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo Afisa Sheria kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Pemba, Mohamed Massoud Said alisema, askari Polisi ni wadau muhimu katika ulinzi wa haki za binadamu kwenye jamii, hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa utekelezaji wa majukumu yao unazingatia Sheria, kanunue na muongozo, ili kuepuka uvunjifu wa haki za binadamu.


"Askari Polisi wakati wa chuchaguzi wana wajibu wa kulinda haki za binadamu, wanapaswa kutekeleza majukumu yao bila ya upendeleo wa mtu, kikundi au chama fulani cha siasa na wanapaswa kutoa ulinzi kwa raia wenye sifa za kushiriki katika uchaguzi bila ubaguzi, unyanyasaji wa kimwili, maneno au vitisho," alifafanua.

Akizungumzia manufaa ya Polisi kuheshimu haki za binadamu alisema ni kuboresha ufanisi wa Polisi na ni wajibu kisheria na kimaadili, Tanzania kuheshimiwa kimataifa, kujenga na kuimarisha mfumo wa utekelezaji wa Sheria uliojikita kwenye heshima, taaluma na uhalali, huimarisha ufanisi wa kazi zao pamoja na imani ya umma kuongezeka kwao.

Akitaja madhara na athari za ukiukwaji wa haki za binadamu unaweza kufanya utekelezaji wa Sheria kuwa ngumu, kuunda vizuizi vinavyokwamisha maendeleo ya utekelezaji wa Sheria kwa ufanisi, hudhoofisha heshima na uaminifu wa Serikali kimataifa, huiweka Serikali kwenye shinikizo la kimataifa kujibu mifumo ya ufuatiliaji wa haki za binadamu, kusababisha machafuko ya kiraia pamoja na kuwalazimisha Polisi kuchukua hatua za kukabiliana na matukio badala ya kuzuia.

Nao washiriki wa mafunzo hayo waliiomba Tume kutoa mafunzo hayo pia kwa vikosi vyengine vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi, ili kila mmoja aelewe na kulinda haki za binadamu.
MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...