Skip to main content

WADAU WA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WATAKIWA KUYAIBUA MTUKIO


IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@


WADAU wa kupambana na masuala ya udhalilishaji Pemba wametakiwa kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanafanikiwa kuondosha vitendo hivyo katika jamii.

Akizungumza katika mafunzo ya kupambana na udhalilishaji, Mratibu wa mradi wa Uwezeshaji wa Kisheria na Upatikanaji wa Haki (LEAP II) kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wete, Rashid Hassan Mshamata amesema, lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi yake anasaidia mapambano dhidi ya udhalilishaji.

Alisema kuwa, wamebaini kwamba kuna kesi nyingi hufutwa kutokana na kukosa ushahidi, hivyo kupitia mafunzo hayo yatasaidia makundi ya jamii waliyoyaanzisha, kuiwezesha jamii kujua umuhimu wa kutoa ushahidi kwa ajili ya kupatikana kwa hatia ya kesi hizo.



"Hili sio suala la mtu mmoja bali ni la kila mtu kwa upande wake ahakikishe anapambana na vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na watoto, tushirikiane kuihamasisha jamii kutoa ushahidi ili kesi zipate hatia," alieleza.

Alifahamisha kuwa, makundi hayo ya jamii (CWGS) yatasaidia kuibuka kesi za udhalilishaji na kiziripoti, pamoja na kutoa elimu kwa jamii ili ipate uelewa juu ya masuala hayo.

Kwa upande wake Mjumbe kutoka Jumuiya ya WEPO Said Rashid Hassan alisema, ili kuweza kulimaliza janga la udhalilishaji hawanabudi kushirikiana, kwani kesi nyingi zinafutwa kwa kukosekana ushahidi.

"Kwenye haya makundi yetu kuna wadau mbali mbali wa kupambana na udhalilishaji, hivyo tunatarajia mabadiliko makubwa, tunaamini kwamba jamii itaelewa kasoro ambazo ni kikwazo na nini kifanyike, ili kesi zipate hatia," alifahamisha Mjumbe huyo.

Akiwasilisha mada ya haki za binadamu Hakimu wa Mahkama ya Wilaya Wete Maulid Hamad Ali alisema, watu wote ni sawa mbele ya Sheria, hivyo sio vyema mtu kuvunja haki ya mwenzake kwa namna yeyote ile.

"Kila mmoja anatakiwa ajitahidi kulinda haki za binadamu kwa sababu binadamu wote wamezaliwa wakiwa sawa, hivyo hawapaswi kunyanyaswa wala kubaguliwa," alisema Hakimu huyo.

Kwa upande wake Afisa Sheria kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu Ali Hamad Mbarouk alieleza kuwa, ni haki ya kila mtu kulindwa, kwani anaponyanyaswa na kudhalilishwa ni kosa kisheria na anapaswa kuadhibiwa.



Nao washiriki wa mafunzo hayo wakiwasilisha ripoti ya kesi hizo, walisema matukio bado ni mengi na wanajamii wanaendelea kuyaficha, hali ambayo inawapa nguvu wadhalilishaji kuendelea kuwakatili watoto.

Walisema kuwa, kupitia mradi huo, watahakikisha wanajamii wanapata uelewa zaidi juu ya masuala ya udhalilishaji na kuwa mstari wa mbele katika kutoa ushahidi ili kesi zipate hukumu.

Mafunzo hayo ya siku moja yameandaliwa na Jumuiya ya WEPO wakishirikiana na UNDP chini ya ufadhili wa Irish Embassy ambayo yamefanyika katika Ukumbi wa skuli ya Chasasa Wete.

                        MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...