Skip to main content

WEPO YAUNGANA NA SERIKALI KUPAMBANA NA UKATILI, UDHALILISHAJI

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

MSAIDIZI wa Sheria Jimbo la Wete Pemba Khamis Faki Simai amesema, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzubar zimekuwa zikichukua juhudi mbali mbali katika kuhakikisha vitendo vya ukatili na udhalilishaji vinaondoka nchini, ingawa jamii bado haijawa tayari.

Alisema kuwa, jamii inapaswa kuthamini juhudi za Serikali hizo katika kupambana na janga la udhalilishaji, kwani wanaoumia ni watoto ambao ndio legemeo lao la baadae na taifa kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa mafunzo kwa vijana yaliyofanyika katika Ukumbi wa skuli ya Chasasa Wete, Msaidizi huyo wa Sheria alisema kuwa, watu wamekosa hofu ya Mungu na ndio maana hata hawajali kwamba kufanya udhalilishaji ni kosa.

‘’Watu wamekosa imani na ndio maana haya matendo hayamalizi licha ya kupigwa vita na Serikali pamoja na wadau wengine, hivyo tuendelee kupambana ipo siku wanajamii wataelewa kuwa hili ni jambo baya,’’ alisema mkufunzi huyo.


Akitoa mada msaidizi wa Sheria Said Rashid Hassan alisema, kunapokosekana kwa stadi za maisha ndipo vijana wanapoharibika, hivyo kuna haja ya kupatiwa elimu hiyo ili kupata vijana wenye kujielewa na kufanya mambo ambayo yatawaletea maendeleo.

‘’Ni muhimu sana kijana kupata taarifa sahihi kuhusu mwili wake, mambo yanayoweza kuathiri haiba yake na afya yake, kuepukana na mambo maovu yakiwemo uzinzi, wizi na madawa ya kulevya,’’ alifahamisha muwasilishaji huyo.

Aidha alisema kuwa, wanatakiwa kujifahamu, kujitathmini na kujiamini, wafanye maamuzi sahihi, kujiwekea malengo, kuhimili mihemko, misongo ya mawazo, shinikizo na mawasiliano.

‘’Mutumie muda wenu kufanya vitu vitakavyowapatia faida kwenu na mufuatilie habari mbali mbali zitakazowasaidia kujifunza na kuwa na upeo mkubwa wa kufikiri,’’ alieleza.



Mapema akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi ya Sheria Wilaya ya Wete (WEPO) Hemed Ali Hemed alisema, anaamini kwamba mafunzo hayo yatawasaidia vijana kujipambanua na kuungana pamoja katika mapambano dhidi ya udhalilishaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa WEPO Khalfan Amour Juma aliwataka vijana wafuate maadili ya dini yao ili waepukane na vitendo viovu ambavyo vinaweza kuwasababishia matatizo.



Nae Msaidizi wa Sheria Rashid Hassan Mshamata alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha vitendo vya udhalilishaji vinaondoka katika jamii, hivyo waungane pamoja kudhibiti.

Akitoa shukurani kwa niaba ya washiriki wenzake Saumu Abdi Ali alisema wamejifunza vitu vingi ambavyo vitawasaidia katika maisha yao na kuahidi kutoa elimu hiyo kwa wanajamii, ili kufikia lengo la mapambano dhidi ya udhalilishaji.

                                           MWISHO.   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan